Hamna kitu hapo..Wananchi wa Iran wana hali mbaya kama kawa..
Mtindio:
1) Jibu swali - "Huu ni Ukweli Kuhusu Rais Ahmedinejad wa Iran?"
2) Baada ya hapo, tuongezee hayo unayoyadai kama unazo data au picha zake. Usisahau kutuwekea 'Source' - Nsololi katupa ni FoxNewsTV (USA)
3) Hali mbaya ya wananchi hata Marekani ni hivyo hivyo. Uliziona picha na mambo ya kusikitisha wakati wa Katrina? Hadi leo baadhi ya "wapiga-miyao" bado hawajapata maskani ya kuishi ambapo Bush ndio anapeta na mabilioni ya dola za kustaafu na kuiacha dunia inalalama na eti 'greatest depression'!!
4) Kwa wale tuliopita Iran na kumwona MAN (Mahmoud Ahmad Nejad) ana kwa ana, hizo picha zimechapishwa chache tu katika maajabu anayoonyesha kwa kuishi maisha ya mtu (MAN) wa kawaida! Lakini Mtindio hawezi kuyasoma au kuyasikia hayo kwani yeye wakweli ni bbc, cnn, voa au dw..
5) Tunamwombea Mungu ailinde nchi yake asishambuliwe kwa kuendeleza nuclear technology ambayo Wayahudi tayari wanayo lakini hawashutumiwi ..
Kweli kazi ipo - double standards everywhere!
Ndugu Kjnne46,
Ahsante ufafanuzi uliompa ndugu Mtindiowaubongo.
Muhimu ni haya yalioandikwa ni kweli au siyo????
Kuhusu kupeleka mapesa kwenye miradi ya kununua ugonvi si kweli kwani miradi hiyo ilianzishwa na serikali iliyopita yeye ameikuta tu. Ila la msingi ameunga mkono na kuendeleza miradi hiyo. Tena zuri zaidi rais aliyemtangulia hakuwa wa mlengo wa siasa sawa na huyu wa sasa.
Pia kuhusu technnology ya Nuclear, watu wasisahau kuwa kuna nchi kama India na Pakstani wanaendeleza miradi hiyo na haohao Wamarekani wanafanya urafiki nao.
Sasa kwa nini iwe tu kwa Irani??? naomba ieleweka hapa watu tutoe maoni pasipo kuweka motives za dini mbili hizi Ukristo na Uislam.
Ndg Nsololi,
....Miradi kama hii ni ya gharama kubwa na mbaya zaidi ni kuwa kama makusudio ya miradi hayajakubaliwa na 'wakubwa' ....