- Thread starter
- #21
wanafanyia wapi kale kamchezo?
Burn swali lako linafurahisha kweli,nami pia nilimwuliza na mkitaka kukutana huwa mnakutana wapi akaniambia siku za kwanza jamaa alikuwa anampeleka Guest amempeleka guest kama mara 2 nikamwambia na baada ya hapo ikawaje akasema kuwa alipoona hivyo na alikuwa anakereka sana akaamua akimwambia wakutana anakataa na akamweleza live hawezi kwenda guest alipomwambia hivyo siku nyingine jamaa akamwita nyumbani alipofika nyumbani jamaa akataka kufanya nae kamchezo kwenye chumba cha houseboy anasema alikasirika sana na akaktaa kufanya chochote,anasema akaendelea kwenda kila alipokuwa anamwita alikuwa anaenda lakini anamgomea kufanya nae chochote kwa hiyo wanaongea hapo sitting room then anaondoka na mara kadhaa jamaa amemshawishi wafanye mapenzi sitting room. kwa kweli aliponieleza nilichoka nikasema mmhhh kumbe kwenye ulimwengu wa mapenzi kuna watu wengine wanakumbana na mambo ya ajabu sana.