Kwa muda mrefu tangu nakua nimekuwa niksikia watu wengi wanapozungumza kiswahili hupenda kuweka neno "ga" mwisho wa neno..mfano Alikwenda wao husema "Alikwendaga" sasa hapo nimekuwa nikijiuliza je ni kiswahili sahihi au la? na swali langu lingine ni hili.. hivi nikifika dukani na ninapotaka kuulizia kitu ipi ni lugha sahihi kati ya hizi, mfano 1. bei gani?? au 2. kiasi gani? naomba msaada jamani.