Salaam wana jamvi. naomba kujuzwa, mara nyingi nistukapo usiku huwa nakuta jamaa kachachamaa sana (kasimama) wakati wala sijafikiria wala kuota ndoto nyevu!! je hii ni kawaida? na ni kwa nini iwe hivi? ahsanteni.
Mkuu,
jee unapostuka huwa unajisikia kwenda kujisaidia haja ndogo?
Kama kibofu cha mkojo kimejaa huwa kinahitaji kihudumiwe, kipunguziwe mzigo, basi huenda ndio sababu ya jamaa kuchachamaa.
Kama si hivyo basi watakuja wataalamu na maelezo zadi!
Kwa hivyo, wasaidie kwa kujibu hilo suali nililokuuliza.
Siyo mara zote mkuu, ndiyo mara ingine huwa najisikia kwenda haja ndogo.