Je Elimu yako Imekusaidia? Je Elimu ya Siasa IMEKUSAIDIA???

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Naomba ufikirie kama elimu yako imekusaidia na zaidi elimu ya siasa kama imetoa tija/gawio kwa taifa.

Elimu ya Mzungu kwa manufaa ya mzungu au na wadandiaji tumo? ninakufundisha kupikia gesi sio ili kazi yako ipungue ktk kupikia kuni bali ili unipikie vizuri, ni mfano tu, Nakufundisha kiingereza sio ili uende kuishi uingereza, nooo ni uweze kusaini mikataba feki, niweze kukutuma kwa kiingereza kwenda kuniwakilisha kwenye mikutano ambayo ninahujumu maslahi ya wengi wa nasaba yako etc

Utamaduni wa Kizungu kwa manufaa ya mzungu au na wadandiaji tumo?

Fedha za Mzungu kwa manufaa ya mzungu au na wadandiaji tumo? bila fedha ufisadi ungekuwepo??? kiwango gani?
Saa ya Mzungu kwa manufaa ya mzungu au na wadandiaji tumo? Nani alibuni Sekunde, Dakika, Saa, Siku? kwa manufaa ya nani?? Luch time saa 7 mchana, hadi serikali imechuka hilo je tulitafiti vya kutosha???

Uchumi huria ni lazima kwanza uwe holela. ni lazima. harafu nakudanyanga eti kuna regulatory authority, nani anaiunda kwa masilahi ya nani??? mafuta bila EWURA bei ilikuwa chini sana, walipoanza kupanga bei imeng'ang'ania 2250TZ wakati ilikuwa 1250TZS!!!!!! say hata kwa sasa ingekuwa 1500TZs

Sio kila kitu kilichorahisisha mambo ni kwa faida ya UMMA, angalia tena sio kila kitendea kazi ni cha manufaa.

Samahani nipe maoni yako.
 
If you judge a fish by its ability to climb a tree, it will live its whole life believing that it is stupid, Je are we judged in the same way the fish is judged? why the blacks feel less as compared to the whites every time there is an encounter??

Kielimu, Kiutamaduni, Kisiasa, Kiuchumi, Kisayansi, Kiteknolojia, Kimaadili etc
 
Mkuu,nanyon'gonyea ghafla,ila elimu kisiasa imenikomboa kwa kutompa kura yangu kiongozi mchumia tumbo hasa waccm,nimetambua ni wao wametufikisha hapa(mikataba feki,uongozi mbovu),pia natambua chanzo ni katiba isiyokidhi maslahi ya wananchi-mfano tume ya uchaguzi kuteuliwa na rais-ibadirishwe
 
Kapo Jr, unadhani ni viongozi wametufikisha hapa? sio kwamba hata wale ambao sisi tunaona ni viongozi wameingizwa kwenye mtego ule ule ambao waongozwaji tumo??? Jiulize elimu unayosoma nani kabuni na kuleta nchini au duniani? mbona mwafrika hayupo??? Sio kwamba tunapewa elimu itakayosaidia wazungu kututawala vizuri??? maana ndo matokeo yake hayo eti kiongozi anasaini mkataba mbovu, nani kampa mkataba mbovu, nani kaandaa mazingira ya kiongozi wetu kusaidini mkataba feki??? nani kasema tutumie fedha za noti kuuza na kununua, kwa manufaa ya nani??? Uchumi ni nini? mbona wa mwafrika tu ndo uko duni?? vipimo vya kuashiria uduni wa uchumi nani kaviweka??? ile hoja ya samaki na mti inafika.

Tumedang'anywa kiasi cha kuamini kama hukusoma elimu ya kizungu eti formal education huna akili??? samaki na jitihada za kupanda mtini.

TUKUMBUKE Kuwambia wenzetu mazingira na mfumo wa dunia uloundwa na wazungu ni kwa ajili ya wazungu, mwafrika mtanzania fikiria upya; Je UN, WB, IMF ni zako?? tumeona wanavyofanya kwa baadhi yetu, huku wakilinda maslahi ya Weupe.
 
Back
Top Bottom