Iron Lady
JF-Expert Member
- Mar 4, 2008
- 4,071
- 1,363
tumeshuhudia jinsi ukoloni mambo leo unavyotutafuna na kutumaliza kidogo kidogo, baadhi ya nchi kama marekani na mataifa fulanifulani ya ulaya yamekuwa yakishinikiza sera mbalimbali za kutumalizia mali zetu na kuuzorotesha uchumi wetu.baadhi yetu tumekuwa tukiwaelewa kuwa ni wanyonyaji wakubwa na baadhi wamekuwa wakiendelea kuamini kuwa ni wasaidizi wa maendeleo ya nchi zetu masikini.sasa hivi sisi ni dampo la bidhaa feki na original za nchi za watu,sisi ndio eneo la kujaribia biashara na kujizolea mali na kuondoka haya yanafanywa na nchi nyingi za kigeni.
china inakuja kwa kasi katika uchumi wa dunia,imekuwa ikizitumia ipasavyo sera za soko huria bila kutumia nguvu za mapigano ikiwa inaendeleza urafiki wa kihistoria kwa baadhi ya nchi kama tanzania na kuujenga mpya katika mataifa mengine ya kiafrika kiasi cha kuonekana mwema na rafiki mzuri, lengo je ni kusaidia nchi za kiafrica au ni mnyonyaji yule yule wa lengo lilelile isipokuwa style tu?
china inakuja kwa kasi katika uchumi wa dunia,imekuwa ikizitumia ipasavyo sera za soko huria bila kutumia nguvu za mapigano ikiwa inaendeleza urafiki wa kihistoria kwa baadhi ya nchi kama tanzania na kuujenga mpya katika mataifa mengine ya kiafrika kiasi cha kuonekana mwema na rafiki mzuri, lengo je ni kusaidia nchi za kiafrica au ni mnyonyaji yule yule wa lengo lilelile isipokuwa style tu?