Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
[h=6]Maslahi ya taifa ni nini basi? ni kwa CCM kuondolewa madarakani na sera na mifuko yake iliyotufikisha hapa kuvunjwavunjwa na kutupiliwa mbali kwenye shimo la usahaulifu la historia. SIYO maslahi ya taifa kuona CCM inajaribu tena kutawala vizuri. Mpinzani anayejaribu kuisaidia CCM 'ijitahidi' au itawale vizuri kwa sababu ni 'maslahi ya taifa' sidhani kama ameelewa vizuri dhana hii ya 'maslahi ya taifa'. It is to the interest of the nation for CCM to be removed from power; nothing more, nothing less.[/h]
Maslahi ya taifa ni zaidi ya watu kujitahidi kutawala vizuri; ni watu sahihi kutawala vizuri. Ni makosa makubwa kufikiria kuwa CCM sasa hivi inaweza kutawala vizuri zaidi ya ambavyo imekwishatawala kwa miaka hamsini iliyopita. Swali hata hivyo ambalo litapaswa kujibiwa ni je CCM inaweza kutumainiwa kuleta utawala bora miaka miwili na nusu iliyobakia? Je yawezekana kweli CCM ikabadili sera zake zilizoshindwa na ikaanza kuja na sera mpya ambazo zikabadilika the trajectory of leadership in the country?
Je CHADEMA inaweza kutoa ushauri mzuri kwa CCM kuweza kutawala vizuri halafu CDM ifurahie kuwa "tumeisaidia serikali na sasa inatawala vizuri"? Je, ni maslahi gani CDM au chama kingine chochote cha upinzani inayo kwa CCM kujaribu kutawala vizuri zaidi? Je siyo maslahi ya chama cha upinzani kuidhoofisha serikali ya chama tawala iliwa wananchi waikatae?
Maslahi ya taifa ni zaidi ya watu kujitahidi kutawala vizuri; ni watu sahihi kutawala vizuri. Ni makosa makubwa kufikiria kuwa CCM sasa hivi inaweza kutawala vizuri zaidi ya ambavyo imekwishatawala kwa miaka hamsini iliyopita. Swali hata hivyo ambalo litapaswa kujibiwa ni je CCM inaweza kutumainiwa kuleta utawala bora miaka miwili na nusu iliyobakia? Je yawezekana kweli CCM ikabadili sera zake zilizoshindwa na ikaanza kuja na sera mpya ambazo zikabadilika the trajectory of leadership in the country?
Je CHADEMA inaweza kutoa ushauri mzuri kwa CCM kuweza kutawala vizuri halafu CDM ifurahie kuwa "tumeisaidia serikali na sasa inatawala vizuri"? Je, ni maslahi gani CDM au chama kingine chochote cha upinzani inayo kwa CCM kujaribu kutawala vizuri zaidi? Je siyo maslahi ya chama cha upinzani kuidhoofisha serikali ya chama tawala iliwa wananchi waikatae?