Je, Bunge litamfukuza Zitto kwa "kutokuhudhuria" vikao; hasaini kupokea posho!?

SubiriJibu

JF-Expert Member
Jun 26, 2009
1,803
1,863
Wakuu,

Wala sina mpango wa kubadili headline kwa sababu wanaokumbuka akiwemo Zittto mwenyewe wanajua kuwa niko sahihi kabisa!

Sakata la kufukuzwa Zitto Kabwe linaanzia kwa msimamo wake binafsi aliouanzisha bungeni. Yeye hakutaka kuzama zaidi kwenye malumbano ya kwamba ama posho ni sahihi au si sahihi. Zitto aliamua kukataa kuchukua posho ile.

Mtego uliotaka kumnasa Zitto ni ule utaratibu kwamba attendance form ndiyo inayotumika kulipa wabunge posho zao (seating allowances).

Bado hili halikuwa kikwazo kwa Zitto na mwishowe akaamua kuacha kusaini kabisa forms hizo ili kukwepa kuingizwa katika list ya wachukua posho.

Spika Anne Makinda alikuja na kauli kwamba kwa attendance form ndiyo ushahidi wa mhudhurio ya mbunge basi Zitto akikosekana mara tatu basi atakuwa amejifukuza ubunge kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Ni kweli Katiba ya nchi Ibara ya 71(1)(c) inasema hivi:

Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake katika Bunge ikiwa Mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika

Sijasikia Anne Makinda au bunge zima likisema limeacha kutimiza mpango wa kumfukuza Zitto ubunge. Hivyo, binafsi nimekuwa nikifanya countdown na hatimaye muda uumefika.

Zitto alianza kuacha kusaini mahudhurio kwenye Session/Mkutano wa NNE. Mkutano wa SITA unaanza Tuesday, January 31, 2012. Matokeo yake ni nini?

Matokeo yake ni kwamba siku bunge linaahirishwa basi Zitto Kabwe atakuwa amekamilisha MIKUTANO MITATU huku karatasi ya mahudhuriao haionyeshi jina lake!

Kama alivyoeleza Spika, basi Spika huyohuyo Anne Makinda itabidi atimize kauli yake kutekeleza kifungu cha katiba kinachomtaka Zitto afukuzwe ubunge.

Sijajua bunge linaloanza wiki ijayo litaisha lini. Lakini tunatarajia kuwa saa ya kuliahirisha yaani kuuahirisha MKUTANO WA SITA basi ndiyo saa ya kutangaziwa pia kufukuzwa kwa Zitto kabwe ubunge wake.

Hatuhitaji kujua Makinda atatumia ushahidi gani wakati yeye mwenyewe alinukuliwa akifafanua kuwa kutosaini attendance form kunamfanya Zitto mbunge yeyote akabiliwe na adhabu ya kufukuzwa ubunge.

Nafahamu kuwa kuna thread humu Zitto mwenyewe alieleza kwamba process ya kumfukuza anataka aone itakuwaje, kwa sababu ni kweli attendance forms hajazi lakini TV zinamuonyesha yumo bungeni, hansard zinamuonyesha anashiriki vikao.

Je, wadau mna la kuongeza?

Wasalaam.
 
Mwanzoni nlidhan umekurupuka kama MS,kumbe uko right,ni uchambuz mzuri wenye kujenga hoja,well done!
 
Mbona Zitto alishalisemea hili. Alisema karatasi pekee siyo inayoonyesha kuwa mtu amehudhuria bungeni. Kuna hansard ambazo huandika matukio ya bungeni na hivyo anajitahidi kuchangia mara nyingi ili awemo kwenye hansard. Hapa zitto atakuwa amekizunguka hicho kifungu cha katiba.
 
umetumwa kutubeep? kabla hatujaenda mbali aulizwa spika na zitto tutapata majibu sahihi badala ya hisia. Tafsiri za kisheria ni pana kwa kila sentensi
 
Mkuu uliyeleta mada endelea ku 'subiri jibu', maana umejitahidi kweli kweli kuandika.
 
Mama naye mbona anawakomalia wabunge wachukuwe posho hata kama hawataki, tatizo liko wapi kama wengine hawataki.. nilisikia hata mh january nae hataki posho! yeye vp anasaini kwny daftari? na kwa upande wa cdm ni mh zitto peke yake ndiye hasaini kwny daftari?
 
umetumwa kumtengenezea kesi Makinda ili aonekane anataka kupunguza upinzani bungeni, kama ni kweli sheria na kanuni zitachukua mkondo wake na Zitto kama hakujua hili basi hayuko smart enough kumalizwa kirahisi hivyo. chadema ina wanasheria kama Lissu, Safari na marando kama hawakumpa ushauri wa kulaumiwa sio Spika
 
Hansard zitawaaibisha. Karatasi la mahudhurio si ushahidi pekee kuwa mbunge kahudhuria vikao. This will shake the intergrity of the Speaker and National Assembly/Perliament as a whole
 
suala la posho kama limekaa kisheria linatakiwa kumalizwa kisheria sio kisiasa, ukichanganya sheria na siasa ni hatari
 
Ansard zitawaaibisha. Karatasi la mahudhurio si ushahidi pekee kuwa mbunge kahudhuria vikao.
This will shake the intergrity of the Speaker and National Assembly/Perliament as a whole
 
Sidhani kama orodha ya malipo bungeni tu ndio kigezo cha kujulikana kama upo?
kwakua Zitto ni mtu makini tayari anajibu la hilo
 
Makinda kama anataka kuhakikisha kuwa mapenzi ya watanzania yako kwa ccm au upinzani ajaribu kufanya hicho kitu.
 
Ivi msimamo wa shibuda ukoje hadi sasa kuhusu posho.bado anataka ziongezwe hadi laki tano au ameridhika. na je vp msimamo wa cdm kuhusu huyu jamaa.atapigwa chini au ndio nipotezee kiaina.
 
Eh roho yangu ungoje burudani pale mjengoni, mama Makinda akiwa kanuna pale kati anatamani kumfukuza Zitto ila hansard zinambana, Lisu anazunguka zunguka kwenye kiti mdogo mdogo, awesome view
 
Back
Top Bottom