Naomba kujua ABCs za biashara ya vyombo vya nyumbani(jikoni)

Alvin Slain

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
6,375
3,654
Jf nadhani hamshindwi jambo lolote ikiwemo pamoja maoni mbalimbali nataka kuanza biashara ya kuuza vyombo vya nyumbani mtaji wangu ni m3 sehemu ya kuuzia ninayo lakini naona ni bora nitafute kitu cha kuchanganya hapo angalau kila siku nipate elf50
================================
Wadau wenye kujua biashara hii naomba watujuze undani wake, naona inawatoa watu wengi.
Kuna vitu vya lazima vinunuliwe mf. Glass, vikombe, vijiko, sahani, masufuria, mabeseni, ndoo, majagi n.k

Naomba kufahamu yafuatayo:
Je mtaji wake ni kiasi gani?
vitu vinavyotoka sana ni vp?
Vitu gani vya kuzingatia ili uifanye biashara hii kwa ukamilifu?
Asanteni

==========================================
MAJIBU
==============================

Mm nimefungua duka la vyombo huu ni mwaka wa tatu sasa ni biashara ambayo inauzika mda wote na ina faida kubwa ingawa ina changamoto zake kwa sasa hadi inafanya nianze kuiogopa.

Ina vitu vingi vya kuvunjika hivyo yakupasa kuwa mwangalifu sana ktk usafirishaji na upangaji wake, mizigo yake ni mikubwa ambayo inaumiza sana ktk transport unaweza safirisha mzigo wa thamani ndogo kwa bei kubwa kutegemea na ulivyokaa, mfano majaba, box za chupa ya chai, ni biashara ambayo ina lazima shamba uwe na store kwayo kama biashara yako haitembei sana utatumia pesa nyingi ktk kulipia fremu, kujaa kwa vyombo feki hasa vya plastic wachina,na wakenya wameteka bidhaa za plastic ambazo ni feki kwayo ukidill nazo ujue kila siku utapokea kesi, pia sasa na chupa za chai

Na wateja wakubwa wa vifaa vya jikoni mtumba ni middle class wa TZ,maskini wananunua vyombo made in TZ brand za CELLO na plastic products zilizotengenezwa tanzania.

Sababu kubwa ni kuwa vitu vya mtumba vina ubora,vitadumu muda mrefu etc.
binafsi sifagilii vitu vya mtumba kwani vinashusha UTU kiaaina,natumia vitu used kwa lengo la kuunga mkono Recycling for the environment.

Mtoa Mada, nenda mwenge kuna maduka ya vitu used vya jikoni. Watakupa muongozo.ila nahisi ulaya wanavichukua bure kwa lengo la kutoa misaada Africa
 
mkuu.... good idea , house wares itakulipa especially ukiweza kuwa na good quality. .. natafuta blender nzuri?
 
3 L's to consider; location, location, location. mkuu tafuta location nzuri..... ipo makini
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Wana jfs,

Naomba ushauri wenu nimejaribu kuchunguza nikaona kuna biashara ya vyombo vya mitumba watu wanafanya...swali ni hili kwa yeyote mwenye upeo na hii biashara je natakiwa niwe na mtaji wa sh ngapi na je vinapatikanaje huko bandarini au kuna mtu anajua vinakouzwa..nikisema vyombo naongelia vyombo vyote vya jikoni majumbani kwetu...ambayo ni second hand...

Nawakilisha...
 
bakuli, vijiko, sufuria mtumba? karibu africa!
Na wateja wakubwa wa vifaa vya jikoni mtumba ni middle class wa TZ,maskini wananunua vyombo made in TZ brand za CELLO na plastic products zilizotengenezwa tanzania.
sababu kubwa ni kuwa vitu vya mtumba vina ubora,vitadumu muda mrefu etc.
binafsi sifagilii vitu vya mtumba kwani vinashusha UTU kiaaina,natumia vitu used kwa lengo la kuunga mkono Recycling for the environment.

Mtoa Mada, nenda mwenge kuna maduka ya vitu used vya jikoni.watakupa muongozo.ila nahisi ulaya wanavichukua bure kwa lengo la kutoa misaada Africa
 
Wadau wenye kujua biashara hii naomba watujuze undani wake, naona inawatoa watu wengi.
Kuna vitu vya lazima vinunuliwe mf. Glass, vikombe, vijiko, sahani, masufuria, mabeseni, ndoo, majagi n.k

Naomba kufahamu yafuatayo:
Je mtaji wake ni kiasi gani?
vitu vinavyotoka sana ni vp?
Vitu gani vya kuzingatia ili uifanye biashara hii kwa ukamilifu?
Asanteni
 
Habari wakuu,

Nataka kuanza hii biashara nina kibanda sehemu fulani nauza bidhaa fulani sasa natakavkuongezea vyombo vya nyumbani vya plastic mostly lakini na vya udongo kidogo,nataka kujua faida yake ni asilimia ngapi ya bei ya manunuzi na wapi exactly nitaweza pata kwa bei nzuri ya jumla.

Ahsanteni kwa taarifa nzuri nitakazopata.
 
Me mwenyew naipenda sana hi biashara kwa kuanzia na vyombo vya plastic na majaba ya maj pamoja na mabeseni.

wadau tunawasubri mtupe maujanja ya kumake pesa
 
wakuu mi pia kuna jamaa angu anaifanya aliniambia kuwa faida ipo 20 to 50 percent ya selling price lakini inaweza ikawa chini au juu ya hapo kidogo inategemea unapata vyombo kwa bei gani na unauzia akina nani....yeye anazungusha majumbani na anakopesha sana,nafikiria kuifanya pia ngoja nitamuhoji maswali zaidi na ikiwezekana nitarudi humu kuweka taarifa zitusaidie wote
 
Wadau wenye uzoefu na biashara hii. Nataka kuanzisha biashara ya vyombo vya majumbani Kibaha kwa wadau wenye uzoefu naomba ushauri wenu hasa wapi pa kupata mzigo na changamoto ninazoweza kukumbana nazo .Naplan biashara iwe ya jumla na rejareja

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Nataka kuuza vyombo vya nyumbani vya hali ya juu yaani high quality- vya ceramic na vya plastic kama sahani, bakuli, glass, thermos nk. Importers na wholesalers wa Dar wanitafute. 0754380094 au 0715380094.
 
Mwenye uzoefu wa biashara ya kuuza vyombo naomba anijulishe juu ya mazingira yapi yanafaa, bidhaa za kuanzia faida na changamoto pia.

Asanteni.
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom