Source:Changamoto,Tuesday, 04 March 2008http://changamoto.co.tz/index.php?option=com_content&task=view&id=1246&Itemid=2ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali amedaiwa kurejeshwa nchini mwa siri kutoka nje ya nchi.
Habari zimedai kuwa Ballali aliingizwa nchini Juma lililopita akishukia Zanzibar na kupelekwa jijini Dar es Salaam kwa boti maalum.
Chanzo chetu cha habari kutoka serikalini, kilidai kuwa mara baada ya Gavana huyo wa zamani kufikishwa katika Pwani ya Dar es Salaam kwa boti hiyo maalumu majira ya jioni, alichukuliwa kwa gari maalumu hadi Ofisini kwa Waziri Mkuu.
Kwa mujibu wa chanzo chetu hicho, Ballali alirejeshwa nchini akiwa chini ya ulinzi mkali na kwamba haukufahamika alikopelekwa baada ya kutoka katika Ofisi ya Waziri Mkuu.
Wenye taarifa zaidi watuhabarishe kuhusu hili