Je, Balali karejeshwa nchini kwa siri?

Ngereja

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
798
333
ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali amedaiwa kurejeshwa nchini mwa siri kutoka nje ya nchi.
Habari zimedai kuwa Ballali aliingizwa nchini Juma lililopita akishukia Zanzibar na kupelekwa jijini Dar es Salaam kwa boti maalum.
Chanzo chetu cha habari kutoka serikalini, kilidai kuwa mara baada ya Gavana huyo wa zamani kufikishwa katika Pwani ya Dar es Salaam kwa boti hiyo maalumu majira ya jioni, alichukuliwa kwa gari maalumu hadi Ofisini kwa Waziri Mkuu.
Kwa mujibu wa chanzo chetu hicho, Ballali alirejeshwa nchini akiwa chini ya ulinzi mkali na kwamba haukufahamika alikopelekwa baada ya kutoka katika Ofisi ya Waziri Mkuu.
Source:Changamoto,Tuesday, 04 March 2008http://changamoto.co.tz/index.php?option=com_content&task=view&id=1246&Itemid=2

Wenye taarifa zaidi watuhabarishe kuhusu hili
 
If it is true, then it is a good moovie which we have been looking for.
 

ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali amedaiwa kurejeshwa nchini mwa siri kutoka nje ya nchi.
Habari zimedai kuwa Ballali aliingizwa nchini Juma lililopita akishukia Zanzibar na kupelekwa jijini Dar es Salaam kwa boti maalum.
Chanzo chetu cha habari kutoka serikalini, kilidai kuwa mara baada ya Gavana huyo wa zamani kufikishwa katika Pwani ya Dar es Salaam kwa boti hiyo maalumu majira ya jioni, alichukuliwa kwa gari maalumu hadi Ofisini kwa Waziri Mkuu.
Kwa mujibu wa chanzo chetu hicho, Ballali alirejeshwa nchini akiwa chini ya ulinzi mkali na kwamba haukufahamika alikopelekwa baada ya kutoka katika Ofisi ya Waziri Mkuu.


Source:Changamoto,Tuesday, 04 March 2008http://changamoto.co.tz/index.php?option=com_content&task=view&id=1246&Itemid=2

Wenye taarifa zaidi watuhabarishe kuhusu hili

Imekaa kama movie za makachero, nimependa gari maalumu, boti maalumu...!!soon tutasikia anakaa kwenye nyumba maalumu na anaku chakula maalumu.
 
hii nayo ni non issue

kwani kulikuwa na mipango ya yeye kupekewa na ngoma?

Yes, it is a non issue kwa kuwa wewe umeweka/umetafsiri kigezo cha jinsi atakavyopokea na sio kama karudishwa bongo au la. Lakini kwangu it is an issue kama kweli karudishwa, bila kujali kama kapigiwa sindimba airport au kaletwa na ungo.
 
Kurejea kwa Balali bila kujali anapokewa kwa mtindo upi ni jambo la muhimu kwani yeye ni shahidi muhimu sana katika Suala la EPA, na hapa JF na watanzania wote tunataka kusikia sauti yake kuhusu suala hili. Hivyo, suala hapa ni kufahamu je ni kweli amerejea? Taarifa ya gazeti la changamoto kwa jinsi ilivyoandikwa inaonyesha kutokuwa na uhakika,yaani bado ni kama vile tetesi tu.Tuendelee kuchimba!!!
 
Whether Balali karudishwa au hajarudishwa (Sindimba or not) is not only an issue, it is a very big issue given what he knows.Any sane person interested in the BOT fiasco must know that.What needs to be probed some more is the authenticity of the story.

Whether karudishwa in secrecy or not is also a big issue, because it is about transparency in this whole saga, if for example, the story is true and with this sort of transparency is how they start, then how can we expect the government to be transparent in bigger issues in the scandal?
 
Kama kweli Balali amerudishwa basi Serikali itakuwa imerudisha goli moja na kufanza matokeo kuwa:

Balali 2 Serikali 1 na Wananchi 1

Bado mpira unachezwa!
 
Kabla ya kujadili hii story ya kurudishwa kwa Ballali kwanza mwenye kujua mmiliki wa gazeti la Changamoto, maana!!! Hebu fikiria Ballali aingie Zanzibar, ambayo ukikohoa kila mtu anajua, halafu akapitishiwa Zanzibar (Hajasema kwa ndege maalumu) na kisha akaja Dar es Salaam ka boti maalumu (sijui kama zipo na huwa zinapaki wapi) na baadaye gari maalumu (nadhani angalao hilo linaweza kuwapo) Hata Sheikh Ponda Isa Ponda nakumbuka alisafirishwa toka Kigoma kwa gari la JWTZ hadi Mwanza akapanda Precision Air (si maalumu) lakini Dar alipandishwa gari maalumu, Benzi mbovu ya CID na ulinzi hadi Central police, sasa huyu, ukishaweka kila kitu maalumu, ungekwisha kusikia hapa.
 
Back
Top Bottom