Je APP Mpya Itakuwa ni Dawa Ya Wadaiwa Sugu

Tatu

JF-Expert Member
Oct 6, 2006
1,100
313
Katika harakati zangu katika mtandao wa Google Play wa kutafuta dawa ya baadhi ya watu ambao ni wadaiwa sugu na wamekuwa wakinipiga chenga kwa ahadi za uongo kila kukicha, nimefanikiwa kupata app inayoitwa YOMM iliyotengenezwa na kampuni ya ZaidiSoft. Hii app inamuwezesha mtumiaji kuweka kumbukumbu ya madeni anayodai au anayodaiwa na malipo katika madeni hayo.

Kilichonifurahisha zaidi kuhusu hii app ni kwamba, kama mtu asipolipa deni, unaweza KUMUANIKA kwa maana ya kwamba mtumiaji yeyote anaweza kufanya search kwa jina au location na kujua kama mtu fulani ana deni. Kwa hiyo kama una hii app halafu rafiki, ndugu, mwanafunzi au mfanyakazi mwenza, au mtu yeyote anataka kukopa hela, unaweza ku-search kabla hujafanya uamuzi wa kumpa au la.

App ni kwa watumiaji wa simu za Android (sina uhakika kwa watumiaji wa iPhone au BlackBerry) na ipo kwa Kingereza. Natumaini itakuwa ya msaada kwako na wale wenye biashara ya kukopesha mikopo midogo midogo kwa watu. Hii app itakuwa dawa ya matapeli na wale wanaopenda kuwarusha watu.
 
Katika harakati zangu katika mtandao wa Google Play wa kutafuta dawa ya baadhi ya watu ambao ni wadaiwa sugu na wamekuwa wakinipiga chenga kwa ahadi za uongo kila kukicha, nimefanikiwa kupata app inayoitwa YOMM iliyotengenezwa na kampuni ya ZaidiSoft. Hii app inamuwezesha mtumiaji kuweka kumbukumbu ya madeni anayodai au anayodaiwa na malipo katika madeni hayo.

Kilichonifurahisha zaidi kuhusu hii app ni kwamba, kama mtu asipolipa deni, unaweza KUMUANIKA kwa maana ya kwamba mtumiaji yeyote anaweza kufanya search kwa jina au location na kujua kama mtu fulani ana deni. Kwa hiyo kama una hii app halafu rafiki, ndugu, mwanafunzi au mfanyakazi mwenza, au mtu yeyote anataka kukopa hela, unaweza ku-search kabla hujafanya uamuzi wa kumpa au la.

App ni kwa watumiaji wa simu za Android (sina uhakika kwa watumiaji wa iPhone au BlackBerry) na ipo kwa Kingereza. Natumaini itakuwa ya msaada kwako na wale wenye biashara ya kukopesha mikopo midogo midogo kwa watu. Hii app itakuwa dawa ya matapeli na wale wanaopenda kuwarusha watu.
hiyo app ni nzuri, nafikiri pia soko lake kubwa litakuwa ni taasisi zote za kifedha hasa zinazokopesha fedha.
 
if u are related to it, usisite kuitangaza coz hakuna malipo, huwa nakuwa proud kuona tunatengeneza vitu vyetu, but tuna katabia fulani ka kutokujiamini, yaani ujanja ujanja tu hata sehemu ambazo hazihitaji ujanja ujanja huo. nilivosoma hii post yako ni dhahiri unahusika na hiyo application.
if so kuwa huru tu kuitangaza, but kama hauhusiki basi samahani nimeelewa vibaya
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom