Je alikuwa ni mama...?


Najaribu kufikiria, kuna akina mama wangapi wanaoweza kumkubali mtoto wa mwanamke mwingine kama alivyo? Ni wachache kupindukia. Wengi juhudi yao siku zote ni kuona watoto wa kambo wanakorofishana na baba zao, wanateswa na kutupwa nje ya familia. Lakini ni kwa faida ya nani? Siku zote ni kwa hasara zao. Huja kugundua wamepata hasara wakiwa wamechelewa uzeeni. Ninampenda na nitampenda kuliko mtu mwingine yeyote, mama yangu ambaye amenionesha maana ya kweli kuhusu maisha. Amenifundisha kwamba, suala siyo mama wa kambo, bali ubinadamu, kujua kupenda.

Alikuwa ni mama………………

Simuliza yako imenigusa sana, na nafikiri imemgusa kila mwenye nia njema na jamii iliyomzunguka. Daaa, natamani kama wenye familia wote hususan akina mama wangekuwa na mioyo kama ya huyu mama!

Ushauri wangu, kwa kila aliyesoma uzi huu, nafikiri bado tuna muda na nafasi ya kutosha kufanya mabadiliko ndani ya familia na jamii iliyotuzunguka. Kuna wale mnaoishi na yatima na watoto wa ndg zenu, Mungu awatie nguvu muwapende kama watoto wenu kabisa wa kuwazaa. Kuna wale ambao mnauwezo kimaisha, na mna ndg wasio na uwezo. Hawa wanaweza kuchukua hii kama changamoto kuwasaidia hao wasio na uwezo. Pia wapo wenye uwezo na wasio na ndg, nafikiri hawa nao wanaweza kutusaidia kwa ishu ya watoto wa mitaani ... Kwa wale wenye uwezo wa kutosha, tafadhali na tujitahidi kuzisaidia familia pamoja na jamii iliyotuzunguka wakiwemo watoto wa mitaani.

Natamani tuwe na mioyo ya huruma na upendo kufikia level hii ...
Mungu na atubariki, Mungu na utukirimie roho za huruma na upendo, Mungu na atuondolee roho za choyo, wivu na manyanyaso na ubinafsi.

Amina.
 
Mtambuzi ahsante kwa simulizi nzuri iliyojaa mafunzo mengi ya maisha; moja lililojitokeza katika simulizi hii ni jinsi gani ushirikina unaweza kuathiri upendo katika familia!! Baba mtu kwa kuwaamini waganga wa kienyeji akamchukia mwanae bila sababu za msingi!!
 
Kwa mara ya kwanza leo mzee mwenzangu Mtambuzi umenikamata! Ntakunywa biya kwa afya yako leo.

Kumbe ndo maana wazungu walisemaga imani zetu ni za kishenzy. Hapana walikosea, si za kishenzy bali za kimahanatha!!

Ngoja nikazimue. Yummy, cacico BADILI TABIA na gfsonwin please come this way... Niko na hommie Kaizer tunajadili huu mswada.
 
Last edited by a moderator:
Mzee mtambuzi ,huwa nashikwa nashauku fulani hivi nikiona post zako leo nimejikuta nasema oh !afadhali! Tena kwa sauti maana hunipa utulivu kwa kiasi flani na concentration sana,asante sana.ninasikitika kusema kwamba binadamu wengi kwa sasa wamepoteza ile childish heart mtambuzi,hasa sisi wanawake tu wanyama na tena watu wengine hudiriki kutuita mashetani ni sawa kabisa penye ukweli lazima niseme mtanisamehe ,kuna watu wan roho mbaya sana mfano:iliripotiwa yule mwanamke aliyemnywesha wifi yake maji aliyosagia vipande vya chupa vilivyomsababishia kukosa hajakubwa alafu akamwagia maji moto sekemu za siri huu ninini kam sio ushetani jamani,unamkuta mama anamtesa mtoto wa kambo anamfanyisha kazi,wakwake wanakaa sebuleni chakula nacho anakuwa wamwisho inshort mtambuzi watoto wanateseka kuliko watu wazima hapa tanzania sio mjini hata vijijini ,hasa mama wa kambo.ninafurahi binafsi kusema hivi sikupewa roho ya unyanyasaji kabisa,namshukuru mungu childish heart haijatoweka n ninaishi kwa misingi hii mikuu miwili niliyoipata kutokana na experience yangu ya miaka inayozidi 25 kwamba hapa duniani ninapita tuu siishi milele,na ninaamini ngome yangu ikianguka nyingine itasismama ambayo nitakuwa sina maamuzi nayo,kwa hiyo ninaishi relax sana ,ninaishi nandugu wengi katika familia na pi mtoto wa kambo ninaye siwezi mnyanyasa kabisa na mungu anisaidie.
Pia wanawake wengi hawaitambui siri ya urembo ukitaka mwanaume azidi kukupenda sana mpende mtoto wake kama wako hata vikipita visweta mnunulie wake yule wako mwache utaona jambololote jema kama huwezi kuwafanyia watoto wote mtangulize wakambo kwanza utaona fuata huu ushauri wangu,.
Nina mfano huu:kuishi na watu vizuri nilijifunza kutoka kwa mama yangu japo sio kwa kiasi kikubwa marehemu mama yangu alikuwa ni mke wandoa wa baba yangu ila baba yangu alikuwa na mke mmja wakisomali na alizaanaye mtoto mmjamwaka 74, mama yetu alimpenda sana kaka yule na tuliishi wote ,mama yakle alikuja kukaa kwa bibi .mamayetu wakati anafariki alimwita huyu kaka yetu akatukabidhi kwake ,baada ya muda baba akahama home yule kaka yetu alitutunza sana ada ya shule matumizi ukiishiwa unamwambiaetc,alitubeba mpaka tukamaliza form six wote tukaenda chuo kikuu nasasa hivi wote tumemzidi elimu maana alishindwa kuenda mbele akitusaidia tunyanyuke sisi.mpaka leo sijawaza nitampa nini ktk maisha yangu mama aliona mbali sana ,nahisi tungeishia mtaani wote ,asanteni
 
Duh!! Mtambuzi unazitoleaga wapi hizi simulizi? Huyo mama tayari ana pepo yake inamsubiri.
 
Last edited by a moderator:
Kwa mara ya kwanza leo mzee mwenzangu Mtambuzi umenikamata! Ntakunywa biya kwa afya yako leo.

Kumbe ndo maana wazungu walisemaga imani zetu ni za kishenzy. Hapana walikosea, si za kishenzy bali za kimahanatha!!

Ngoja nikazimue. Yummy, cacico BADILI TABIA na gfsonwin please come this way... Niko na hommie Kaizer tunajadili huu mswada.

Niko njiani naja mpenzi,naomba 'MNIPOKEE' kwa mahaba yooote.... Erickb52 funga macho na bakuli lako(nimekuonya mapemaaaa)
 
Last edited by a moderator:
Mzee mtambuzi ,huwa nashikwa nashauku fulani hivi nikiona post zako leo nimejikuta nasema oh !afadhali! Tena kwa sauti maana hunipa utulivu kwa kiasi flani na concentration sana,asante sana.ninasikitika kusema kwamba binadamu wengi kwa sasa wamepoteza ile childish heart mtambuzi,hasa sisi wanawake tu wanyama na tena watu wengine hudiriki kutuita mashetani ni sawa kabisa penye ukweli lazima niseme mtanisamehe ,kuna watu wan roho mbaya sana mfano:iliripotiwa yule mwanamke aliyemnywesha wifi yake maji aliyosagia vipande vya chupa vilivyomsababishia kukosa hajakubwa alafu akamwagia maji moto sekemu za siri huu ninini kam sio ushetani jamani,unamkuta mama anamtesa mtoto wa kambo anamfanyisha kazi,wakwake wanakaa sebuleni chakula nacho anakuwa wamwisho inshort mtambuzi watoto wanateseka kuliko watu wazima hapa tanzania sio mjini hata vijijini ,hasa mama wa kambo.ninafurahi binafsi kusema hivi sikupewa roho ya unyanyasaji kabisa,namshukuru mungu childish heart haijatoweka n ninaishi kwa misingi hii mikuu miwili niliyoipata kutokana na experience yangu ya miaka inayozidi 25 kwamba hapa duniani ninapita tuu siishi milele,na ninaamini ngome yangu ikianguka nyingine itasismama ambayo nitakuwa sina maamuzi nayo,kwa hiyo ninaishi relax sana ,ninaishi nandugu wengi katika familia na pi mtoto wa kambo ninaye siwezi mnyanyasa kabisa na mungu anisaidie.
Pia wanawake wengi hawaitambui siri ya urembo ukitaka mwanaume azidi kukupenda sana mpende mtoto wake kama wako hata vikipita visweta mnunulie wake yule wako mwache utaona jambololote jema kama huwezi kuwafanyia watoto wote mtangulize wakambo kwanza utaona fuata huu ushauri wangu,.
Nina mfano huu:kuishi na watu vizuri nilijifunza kutoka kwa mama yangu japo sio kwa kiasi kikubwa marehemu mama yangu alikuwa ni mke wandoa wa baba yangu ila baba yangu alikuwa na mke mmja wakisomali na alizaanaye mtoto mmjamwaka 74, mama yetu alimpenda sana kaka yule na tuliishi wote ,mama yakle alikuja kukaa kwa bibi .mamayetu wakati anafariki alimwita huyu kaka yetu akatukabidhi kwake ,baada ya muda baba akahama home yule kaka yetu alitutunza sana ada ya shule matumizi ukiishiwa unamwambiaetc,alitubeba mpaka tukamaliza form six wote tukaenda chuo kikuu nasasa hivi wote tumemzidi elimu maana alishindwa kuenda mbele akitusaidia tunyanyuke sisi.mpaka leo sijawaza nitampa nini ktk maisha yangu mama aliona mbali sana ,nahisi tungeishia mtaani wote ,asanteni

Daaah aiseee sijui hata nikwambie nini mdogo wangu,story yako imenisikitisha maskini pole sana. Cha msingi mumuheshimu sana huyo kaka yenu na isipite siku bila kumuombea Mungu ampe miaka mingi yenye raha na amani ili aje kula matunda yenu mliyoyachuma kutokana na juhudi zake. Duniani huku kuna mapito na majaribu ya kila namna yani leo moyo wangu unaumia nnaposoma post kama hizi.
Hapo kwenye red Mungu atakusaidia tu mpendwa,na uendelee kuwa na moyo huo huo.
 
Ahsante Mtambuzi kwa stori nzuri. Imenigusa sana hii stori. Hakika huyo alikuwa ni mama zaidi ya mama yako. Alikjua huna nguo, akaja na nguo, alibeba machozi yako, akabeba huzuni yako, na muhimu zaidi, alibeba future yako.

Mimi yangu ni tofauti kidogo, alinitesa sana nikiwa mdogo, lakini siku moja sikuamini alibadilika ghafla na kunipenda na kunijali kuliko hata mwanae. Ninampenda na nina mjali sana.
 
Umeandika kwenye heading, 'Je alikuwa ni mama........................?'

Mi nasema alikuwa ni mama zaidi ya mama yako. Pole kwa kumpoteza mama toka ukiwa mdogo.
 
"Ninampenda na nitampenda kuliko mtu mwingine yeyote, mama yangu ambaye amenionesha maana ya kweli kuhusu maisha. Amenifundisha kwamba, suala siyo mama wa kambo, bali ubinadamu, kujua kupenda."
Hapo tu mzee Mtambuzi umemeliza kazi
 
Last edited by a moderator:
Kwa mara ya kwanza leo mzee mwenzangu Mtambuzi umenikamata! Ntakunywa biya kwa afya yako leo.

Kumbe ndo maana wazungu walisemaga imani zetu ni za kishenzy. Hapana walikosea, si za kishenzy bali za kimahanatha!!

Ngoja nikazimue. Yummy, cacico BADILI TABIA na gfsonwin please come this way... Niko na hommie Kaizer tunajadili huu mswada.
Asprin nimefika, leo ndani nipo na thong tu, kazi iwe rahisi kwako! mzima weye? mi mithd u kha!
 
Last edited by a moderator:
For sure nimeguswa sana...dah kuna watu ni zaidi ya binadamu..nahisi ni malaika ambae Mungu alimleta ili ahakikishe lile lengo Mungu alilokupangia hapa duniani linatimia! Inafaa kuwa kitabu ambacho naamini jamii yetu itajifunza! Mungu akubariki sana mkuu kwani ni zaidi ya somo! Wengi wataguswa, na wengi watabadilika kwa huu ushuhuda!
 
uuuwi nimelia jamaniiiiii............aah(sob sob sob)
kweli wanawake tuna changamoto ya kufanya watu wabadilike.....huh!!!
 
asante kaka mtambuzi kwani hii stori inaelimisha,inahusunisha na kuwafunza wanawake kuwa mtoto si lazima awe uliyemzaa wewe hata mtoto wa mwenzako ni mtoto wako. ni wanawake wachache sana kwenye hii dunia ndio bado wana upendo kama huo asante mtambuzi kwa stori nzuri real you made my day.
 
Mtambuzi, story nzur na yenye ujumbe kwa jamii i.e wanawake sisi. ni wachache sana wenye moyo kama huuo wa huyo mama.
wito kwetu kinamama,tuwapende watoto wa wenzetu/waume zetu hata kama kacheat akakuletea mtoto hana makosa!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom