Je alichotabiri Nyerere tayari kinatokea sasa?

"Dola lazima isimamie sheria ili kulinda haki na kuhifadhi amani. Wajibu huu usipozingatiwa, wataibuka manabii wenye kuihubiri haki kwa kuwahukumu wengine. Hamtabaki salama mkifikia hapo"

J.K. Nyerere

Mbona jamaa wanaenda mbali na off point wakati issue ni staright forward?

Nadhani madhumuni yalikuwa kulinganisha utabiri huo wa Mwalimu na hali ilivyo sasa. Hebu sasa angalieni issue ya Mengi na Rostam. Wote hawa wamekuwa manabii wenye kuhubiri haki kwa kuwahukumu wengine. Sababu yake? Dola haikusimamia sheria ili kulinda haki na kuhifadhi amani i.e. kama wote, mafisadi papa na mafisadi nyangumi wangechukuliwa hatua za kisheria, hali hii isingejitokeza.

Hali hii ikiendelea na wakiibuka manabii wengi zaidi, hatutabaki salama. Watu watachapana mitaani.
 
FMES,
Mkuu swala la kuanzisha vyama vingi halihusiani na nguvu ya mtu bali nguvu ya hoja...

- Ni nguvu ya hoja ya Mwalimu, ndiyo iliyounda vyama vingi, ikampa urais Mwinyi, ikampa urais Mkapa, na ikampa kiburi Salmin na kuiba uchaguzi, sasa unaona nguvu ya hoja inakuwa juu ya sheria? Matokeo yake ndio haya tuliyonayo, Waziri Mbilinyi alituhumiwa na Mrema kwamba ni mla rushwa, kamati ya bunge ya Masilingi na Idd simba ikakubali kua ni kweli, badala ya kumfikisha kwenye sheria akapelekwa CC ambako iti took mstaafu Kawawa kumuondoa uwaziri, ghafla Idd simba na Masilingi wakawa mawaziri!

- Sheria iko wapi Bob hapo? yale yale ya huyu ni mwenzetu forget about the law of the land, ndio maana leo bongo tunashangaa jinsi wanasheria walivyo matajiri wa ajabu, wengi tumewabatiza majina ya wazungu wa unga maana sio utamaduni wetu kuona wanasheria wakishamiri kimaisha, wakati huko dunia nzima wanasheria walikuwa ndio watu, unakumbuka jinsi Mwanasheria Njonjo alivyotutesa na EAC? Tulikuwa tunasubiri Mwalimu aseme nguvu ya hoja badala ya sheria, au CC kama sio NEC!

Bob ndio maana tumekwama, taifa lisilo heshimu wala kuwa na sheria na haki hata vitabu vya dini viko very clear na hilo kwamba matokeo yake yatakuwa kama haya tuliyonayo bongo, hakuna cha ajabu maana bado tunasubiri nguvu ya hoja! Mkapa alisema tena kwa kiburi kikubwa sana nitawa suprise wa-Tanzania kwa kuwapatia rais wasiyemtegemea, can you imagine Obama aseme hivyo mwisho wa term yake? Lakini bongo hii ya Sodoma hakuna noma ni sawa tu!

Respect.

FMEs!
 
"Dola lazima isimamie sheria ili kulinda haki na kuhifadhi amani. Wajibu huu usipozingatiwa, wataibuka manabii wenye kuihubiri haki kwa kuwahukumu wengine. Hamtabaki salama mkifikia hapo"

J.K. Nyerere
- Hakuna aliyetoka nje ya mada, labda wewe tu mkuu ndiye unayezunguka zunguka, cha msingi katika hiyo hoja ya Mwalimu kwa moni yangu ni hayo juu, dola lazima isimamie sheria na kulinda amani, wajibu huu usipozingatiwa hamtabaki salama as if tuliwahi kua salama kutokana na dola kusimamia haki na sheria, tulikuwa na amani ya uongo, tulikuwa na sheria za kinafiki za kushika wadogo tu masikini wauza sabuni mtaani huku wezi wakubwa wakipeta tu matokeo yake wananchi wengi wakawa wanasubiri zamu yao ambayo ndio hii sasa tulipo imefika Mwalimu the law of land hayupo tena, nani wa kumkemea mwingine?

- Rostam na Mengi wote wameshiriki kuiweka serikali ya sasa, kwa sababu ni taifa lisilokuwa na sheria toka zamani ingekuwepo hawa matajiri wasingeweza, sasa kama wameiweka serikali kwa nini wasituamulie na sheria pia, ni wajibu ambao haukuzingatiwa na Mwalimu mwenyewe na sasa we are paying for, ingawa pia na sisi tuliobaki tuna our part lakini nani atamvika kengele mwenziwe? Wakati wote hatujui sheria na haki? Sasa eti it takes a genius kujua toka enzi za Mwalimu kwamba kuna siku wangekuja kutokea manabii tulionao sasa?

Respect.

FMeS!
 
- Ni nguvu ya hoja ya Mwalimu, ndiyo iliyounda vyama vingi, ikampa urais Mwinyi, ikampa urais Mkapa, na ikampa kiburi Salmin na kuiba uchaguzi, sasa unaona nguvu ya hoja inakuwa juu ya sheria? Matokeo yake ndio haya tuliyonayo, Waziri Mbilinyi alituhumiwa na Mrema kwamba ni mla rushwa, kamati ya bunge ya Masilingi na Idd simba ikakubali kua ni kweli, badala ya kumfikisha kwenye sheria akapelekwa CC ambako iti took mstaafu Kawawa kumuondoa uwaziri, ghafla Idd simba na Masilingi wakawa mawaziri!

- Sheria iko wapi Bob hapo? yale yale ya huyu ni mwenzetu forget about the law of the land, ndio maana leo bongo tunashangaa jinsi wanasheria walivyo matajiri wa ajabu, wengi tumewabatiza majina ya wazungu wa unga maana sio utamaduni wetu kuona wanasheria wakishamiri kimaisha, wakati huko dunia nzima wanasheria walikuwa ndio watu, unakumbuka jinsi Mwanasheria Njonjo alivyotutesa na EAC? Tulikuwa tunasubiri Mwalimu aseme nguvu ya hoja badala ya sheria, au CC kama sio NEC!

Bob ndio maana tumekwama, taifa lisilo heshimu wala kuwa na sheria na haki hata vitabu vya dini viko very clear na hilo kwamba matokeo yake yatakuwa kama haya tuliyonayo bongo, hakuna cha ajabu maana bado tunasubiri nguvu ya hoja! Mkapa alisema tena kwa kiburi kikubwa sana nitawa suprise wa-Tanzania kwa kuwapatia rais wasiyemtegemea, can you imagine Obama aseme hivyo mwisho wa term yake? Lakini bongo hii ya Sodoma hakuna noma ni sawa tu!

Respect.

FMEs!


Endelea kulonga. Nchi iliongozwa kwa kudumisha fikra sahihi za mwenyekiti.
 
Mnamlaumu Mwalimu kwa lipi? Je hicho alichokisema si ndicho kinatokea sasa?

Palipo na haki na uongozi wa sheria huwa hapatokei vurugu; kinachotokea sasa ni kwasababu viongozi tulio nao hawatoi haki sawa kwa watu wote na sheria za nchi hazifuatwi.

Mwalimu alikuwa kichwa kweli kweli!
 
Mnamlaumu Mwalimu kwa lipi? Je hicho alichokisema si ndicho kinatokea sasa?

Palipo na haki na uongozi wa sheria huwa hapatokei vurugu; kinachotokea sasa ni kwasababu viongozi tulio nao hawatoi haki sawa kwa watu wote na sheria za nchi hazifuatwi.

Mwalimu alikuwa kichwa kweli kweli!

Challenges walizo viongozi wa sasa ni tofauti alizokuwa nazo Nyerere. Nyerere alituchagulia framework ya sisi tuichi na dola ilitumika kulinda framework hiyo (Ujamaa).

Mtanzania gani sasa hivi atakubali kuishi katika u-primitive wa ujamaa?
 
FMES,

"Dola lazima isimamie sheria ili kulinda haki na kuhifadhi amani. Wajibu huu usipozingatiwa....

Hapana mkuu wangu unapotosha...tumeishi kwa sheria za Kikomunist chini ya mwalimu na kulindana ni Ilani kubwa ya Ukomunist...NI SHERIA kwa sababhu mtu huyo anasimama nyuma ya malengo ya chama..Serikali nzima ya CCM bado imekumbatia Ilani hiyo na wala sii kwamba aliiweka Nyerere.. Ndio mfumo wa Kijamaa unavyokwenda kisheria...Serikali chini ya Ujamaa ilitegemea zaidi ilani ya Huyu ni mwenzetu.. hata vijiweni tuliishi hivyo hivyo, huwezi kujiunga Saigon kama sii mwenzao wala usitegemee kulindwa..Marekani vile vile walikuwa na wenzao na wakalindana hadi leo...Ndivyo ilivyokuwa ktk siasa na maisha ya wakati wa mwalimu..

Sasa mkuu unamleta Mbilinyi ambaye aliiiba wakati wa Mkapa (awamu ya tatu) akiwa waziri bado unataka kusema Ni Nyerere aliyemwekea kinga? - Ebu nambie Nyerere alifanya nini Salmin akaiba kura...Hivi kweli wewe unaamini Wana Mapinduzi wangetaka kweli Sharif Hamad awe rais wa Zanzibar!.. mkuu wangu siasa za Zamzibar huzielewi kabisa..CUF haikutakiwa kuihsinda wakati wowote ule hata kama angesimama mtu mwingene kinyume cha Salmin bado serikali ya Mapinduzi ingefanya kila mbinu kuhakikisha wanashinda...Kumbuka mwalimu alitaka Salim A Salim ashike kiti (rais wa Tanzania) baada ya Mwinyi, Baraza la Mapinduzi wakamtolea nje..Kifupi MPEMBA hawezi kukaa kiti cha IKULU yao..iwe kwa hoja ya Nyerere au Obama..hoja ni hoja tu mkuu wangu nguvu wanayo wenyewe.

Unakumbuka wakati wa Mkapa, Nyerere aliwahi kwenda Ikulu akamkuta Mkapa Nyakanyaka akiambaa na ukuta na hakufanya kitu kwa sababu mwenye nguvu ni Mkapa leo uje na hizo za Mbilinyi?...Duh!

Kitu kimoja tu mkuu, Hoja za mwalimu zilikuwa na maana, Ni yeye aliyetuingiza ktk soko huiria baada ya kukubali kushindwa..We F... Up! period.

Bado tunaendekleza KULINDANA hiyo central government ni kubwa kuliko kazi zilizopo..

Vurugu za ndani ya CCM sijui Mtandao (Progressive), na hao jadi (Conservatives)..wanamalizana wenyewe wala sii kazi ya mwalimu isipokuwa maneno yake yametimia..
 
Zakumi,
Mkuu bado tu..hivi kweli tungekuwa Mabepari unaelewa kingetokea kitu gani?... wakati mwalimu anachukua nchi tulikuwa na wasomi wangapi?..tena basi wengi wao kama wapo walisomeshwa na wazungu, wahindi au waarabu kutokana na mshikamano wa wazazi wao na watu hawa..Unayajua haya au unasema tu maadam kulaumu.
Hakuna Mtanzania aliyeweza kujisomesha Chuo kikuu..Ungekuwa wapi wewe mkuu wangu leo hii kama sii kuokota makopo!

Sema wewe una matatizo na Ujamaa lakini hoja ya mtu haiwezi kupotea kwa sababu tu alikuwa mjamaa.. hata Hitler kuna maneno alisema yenye Upeo mpana zaidi na as a fact ndiye mtu wa kwanza kusema Wayahudi watakuja itawala dunia kiuchumi kama tusipoangalia.. Na utabiri huo umekamilika!..
 
Zakumi,
Mkuu bado tu..hivi kweli tungekuwa Mabepari unaelewa kingetokea kitu gani?... wakati mwalimu anachukua nchi tulikuwa na wasomi wangapi?..tena basi wengi wao kama wapo walisomeshwa na wazungu, wahindi au waarabu kutokana na mshikamano wa wazazi wao na watu hawa..Unayajua haya au unasema tu maadam kulaumu.
Hakuna Mtanzania aliyeweza kujisomesha Chuo kikuu..Ungekuwa wapi wewe mkuu wangu leo hii kama sii kuokota makopo!

Sema wewe una matatizo na Ujamaa lakini hoja ya mtu haiwezi kupotea kwa sababu tu alikuwa mjamaa.. hata Hitler kuna maneno alisema yenye Upeo mpana zaidi na as a fact ndiye mtu wa kwanza kusema Wayahudi watakuja itawala dunia kiuchumi kama tusipoangalia.. Na utabiri huo umekamilika!..

Mkandara:

Unaboronga kama Campanero. Kusomeshwa na ujamaa ni vitu viwili tofauti. Hata mkiritimba Kamuzu Banda alisomesha watu. Tena ujamaa ndio umeboronga sana katika kusomesha watu. Watu wengi waliosomeshwa katika kipindi cha Nyerere unayaona matunda yao.

Tukirudi kwenye mada. Nchi ni lazima i-move forward na katika kufanya hivyo wapo watakaotoka nje ya mistari, watakuwa mafisadi lakini ni watatokea braves na kurekebisha mambo.

Haya mambo ya Nostragia ya Nyerere alisema hivi alisema vile, wakati aliyoyasema sio mapya duniani.
 
Zakumi,
Unaboronga kama Campanero. Kusomeshwa na ujamaa ni vitu viwili tofauti. Hata mkiritimba Kamuzu Banda alisomesha watu. Tena ujamaa ndio umeboronga sana katika kusomesha watu. Watu wengi waliosomeshwa katika kipindi cha Nyerere unayaona matunda yao.
sasa haya matusi!.. unaposhindwa kwa hoja mkuu usije na vioja! tena hasa wewe uliyesomeshwa!.. na nani vile mzungu au? Lol..
Tukirudi kwenye mada. Nchi ni lazima i-move forward na katika kufanya hivyo wapo watakaotoka nje ya mistari, watakuwa mafisadi lakini ni watatokea braves na kurekebisha mambo.
Hii ni ndoto, Somalia wana miaka mingapi wauana! na waliokuja wanaitwa braves hao..
 
Zakumi,

sasa haya matusi!.. unaposhindwa kwa hoja mkuu usije na vioja! tena hasa wewe uliyesomeshwa!.. na nani vile mzungu au? Lol..

Hii ni ndoto, Somalia wana miaka mingapi wauana! na waliokuja wanaitwa braves hao..

Watu mnam-miss Nyerere. Mnashindwa ku-move on. Wakati sisi waMarekani tunatumia our constitunal values kuonyesha haki hazitendeki au watu wanaboronga. Nyie mnatumia utabiri wa Nyerere baadaye sheikh Yahya Hussein.

Kama Nyerere angekuwa mtabiri mzuri, kwanini hakutuachia katiba ya maana?
 
hivi enzi za utawala wa nyerere kulikuwa na yoyote yule aliyewahi kushtakiwa kwa kupelekwa kesi yake mahakamani? (au enzi zake kulikuwa hakuna wakosa? au kulikuwa hakuna mahakama?)
 
hivi enzi za utawala wa nyerere kulikuwa na yoyote yule aliyewahi kushtakiwa kwa kupelekwa kesi yake mahakamani? (au enzi zake kulikuwa hakuna wakosa? Au kulikuwa hakuna mahakama?)

hoja yako haijaeleweka kabisa, hunataka kutuambia kwamba kulikuwa hakuna kesi zilizokuwa zinaendeshwa mahakamani wakati wa nyerere? Au kesi za namna gani ambazo unataka kuzizumngumzia?
 
Mnamlaumu Mwalimu kwa lipi? Je hicho alichokisema si ndicho kinatokea sasa?

Palipo na haki na uongozi wa sheria huwa hapatokei vurugu; kinachotokea sasa ni kwasababu viongozi tulio nao hawatoi haki sawa kwa watu wote na sheria za nchi hazifuatwi.

Mwalimu alikuwa kichwa kweli kweli!

- Tunamlaumu Mwalimu kwa kupanda mahindi na kutegemea kuvuna korosho, wote hatujui sheria wala haki, ndio maana Marahemu Ditopile, alipoachiwa kwa dhamana Mtikila alipotaka kumfungilia mashitaka tukatokea wananchi wa dini yake na kumuonya sana Mtikila aache kujifanya anajua sana sheria na kwamba anaichukia dini ya Ditopile sio makosa yake, sisi wananchi wa dini yake hatuwezi kunyamaza kimya na kuona ndugu yetu anaonewa!

- Tizama wote kuanzia viongozi mpaka wananchi hatujui sheria wala haki, ndio maana sasa ni zamu ya manabii kutusaidia sheria, ubovu nyumba siku zote huwa unaanzia kwenye foundation.

Respect.

FMEs!
 
"Dola lazima isimamie sheria ili kulinda haki na kuhifadhi amani. Wajibu huu usipozingatiwa, wataibuka manabii wenye kuihubiri haki kwa kuwahukumu wengine. Hamtabaki salama mkifikia hapo"

J.K. Nyerere

Mkuu, huu ni ujumbe wa mtu aliekuwa makini na alieona mbali mno! Achana na watu wanaofikiri kwa kutumia makwapa!

Dola imeshindwa kabisa kusimamia sheria ili kulinda haki za wananchi wa Tanzania ndiyo maana wanatokea watu ambao wanadai wanatetea haki za waTanzania kutofisadiwa, sa hapa ndiyo penye tatizo...

Ni vigumu mno kujua niyupi anania ya kweli au ana ajenda yake chafu kuliko!
Sasa, Mwalimu hapa anatupa lawama kwa dola kwa uzembe (labda na ujinga pia) kwa kuliachia hili hadi kufikia hapa tulipo pa kutojua nani mkweli na nani mnafiki!
 
- Ni nguvu ya hoja ya Mwalimu, ndiyo iliyounda vyama vingi, ikampa urais Mwinyi, ikampa urais Mkapa, na ikampa kiburi Salmin na kuiba uchaguzi, sasa unaona nguvu ya hoja inakuwa juu ya sheria? Matokeo yake ndio haya tuliyonayo, Waziri Mbilinyi alituhumiwa na Mrema kwamba ni mla rushwa, kamati ya bunge ya Masilingi na Idd simba ikakubali kua ni kweli, badala ya kumfikisha kwenye sheria akapelekwa CC ambako iti took mstaafu Kawawa kumuondoa uwaziri, ghafla Idd simba na Masilingi wakawa mawaziri!
Mkuu FMES, labda mimi sijui maana ya sheria. Lakini nafahamu kuwa kushawishi si kuvunja sheria. Kuvunja sheria ni kukiuka taratibu, kanuni, miiko iliyowekwa katika kutekeleza jambo. Mimi sijaona mahali ambapo Nyerere amevunja sheria katika kupendekeza watu anaoona wanafaa kuongoza nchi kuchaguliwa, kuteuliwa au kupewa nafasi hizo hasa muda muafaka unapofika tena kwa kufuata taratibu, kanuni na sheria za nchi. Mkuu, Mwinyi alichaguliwa na wananchi (tena kwa asilimia zaidi ya 99 kila mara), Mkapa pia alichaguliwa na wananchi, Salmini pia alichaguliwa hivyo hivyo. Kosa la uvunjaji wa sheria liko wapi hapo?

Nakumbuka wakati Nyerere alipokuwa akishauri CCM kukubali vyama vingi, alitoa hoja ambayo ilikubalika na wengi. Na baada ya hoja ile, si kwamba nchi iliamua mara moja kukubali vyama vingi, bali mchakato wa kujua ukweli ulifuata na uamuzi ulichukuliwa kuwa, kutokana na hoja za Mwalimu ambazo kwa kweli hazikuwa za kulazimisha zaidi ya kutoa dira. Kumbuka wakati ule ndio ambao kauli kama serikali iko likizo zilianza kusikika. Viongozi wengi walikosa uadilifu na dira.
 
Wakati mwingine inakuwa VIGUMU sana kwa BAADHI yetu kumwelewa MWALIMU. Sababu ziko nyingi zikiwemo:
1. Kuna ndugu zetu waliumizwa enzi za utawala wake;
2.Tulitaka kutajirika haraka na kwa njia yoyote ile akatuzuia;
3.Alisimamia kikamilifu sheria zilizokuwepo ikiwemo ya RUSHWA;
4.Hatukumpenda tu hivyo alivyokuwa.
Tukubali jambo moja ambalo liko wazi mno kwa sasa, KATIBA na SHERIA havisimamiwi vizuri na utawala wa sasa.Nitatoa mifano miwili ya hivi karibuni.
1.Mjadala wa Zanzibar ni NCHI au sio NCHI na majibu ya RAIS wetu ambayo hakupaswa kuyatafuta nje ya Katiba kama alivyofanya WM Pinda.
2. Mengi na RA walipaswa kuwa ndani siku nyingi kwa malumbano yao yale ya kijinga.
 
Kwa mtazamo wangu, Nyerere alikuwa na mapungufu makubwa katika uwezo wa kuleta maendeleo. Hatua nyingi za kiuchumi alizokuwa akizichukua hazikuwa na tija kwa ustawi wa Taifa (hasa kwa kuwa kulikuwa na vita baridi duniani). Ila sioni mahali ambapo naweza kusema Nyerere alikuwa akivunja sheria. Sheria zote za nchi zilimruhusu kufanya mambo mengi ambayo alikuwa akiyafanya (bila kujali kuwa sheria hizo zilikuwa nzuri au mbaya). Sheria ni sheria tu.

Mambo mengi yanayotokea sasa yanasababishwa na nchi kukosa dira. Hakuna imani yoyote ya mwelekeo wa Taifa hili hasa baada ya kuvunjika kwa Azimio la Arusha, na maazimio mengine yote (ambayo aliefanya hivyo si Nyerere). Tangu wakati huo, nchi hii inayumba na itaendelea kuyumba hadi hapo tutakapoacha ulevi na kushika usukani kuongoza nchi kuelekea tunapotaka kwa kupajua.

Hoja ya thread hii ni sahihi na maneno ya Nyerere ndio yanaanza kukamilika. Hatujachelewa, tunaweza kubadilisha mwelekeo. Ila tusipobadilika, tutachelewa na maneno ya Mwalimu Nyerere yatakamilika.

Hakuna lolote ambalo serikali hizi (tangu muhula wa 2 wa Mwinyi hadi leo ambayo yanamuhusu Nyerere tena). Hakuna hata moja ambalo tunaweza kusema lilibuniwa na Nyerere na linaendelea kutumika. Miiko yote imevunjwa, direction ya uchumi imebadilishwa, maazimio yote yameuawa, siasa ya nchi imebadilishwa (japokuwa wanasiasa wanaona aibu kutangaza rasmi). Tatizo kubwa ni kwamba, mabadiliko yaliyofanywa hayajitoshelezi na hayatekelezeki. Hivyo kila anaeongoza nchi atakuwa na dira yake mwenyewe ambayo nayo haidumu, na mara nyingi atavunja sheria.

Nyerere sio designer wa maisha yetu ya sasa. Maisha haya tumeyaharibu wenyewe, na bahati mbaya aliona kidogo jinsi tulivyoharibu. Alilalamika hakuna aliemsikiliza. Sasa tuendelee kuvuna tulichopanda bila kumfufua Nyerere kwa makosa yetu.
 
Wacha na utimie huo 'unabii' wa mwalimu. Hongera zao manabii wa kuhubiri haki hata kama kuwataja wanaokalia haki za wengine kutaonekana kana kwamba ni 'hukumu'.

Pia tukumbuke Nyerere alishatoa angalizo; SERIKALI DHALIMU HAIKUSANYI KODI KWA MATAJIRI. Kuliparafrezi hilo, SERIKALI ISIYOJALI, INAWAKANDAMIZA WANAOPIGIA KELELE WANAOKEMEA UFISADI.

Na badala yake serikali isiyo jali, INAWALINDA WEZI, MAFISADI PAPA NA NYANGUMI--- KUDADADEKI!
 
Inawezekana uko sahihi lakini tulitaraji walioomba uongozi (isomeke utawala) kurekebisha hayo. Ni uhawayani uliopindukia kuendelea kumlaumu mfu. Tuwaache wafu wawazike wafu wenzao.
Pamoja na matatizo mengi ya Nyerere, alikuwa ni mtu anayejari watu wake.Angeliweza kumuiga Mobutu, Idd Amini, Hasting Banda etc. Hawa na wengine wengi waliiba mamilioni wakala wao na familia zao, walikosa uzalendo na kuendeleza ukabila na kurithishana watu wa aina ile ambayo waliona watayalinda madudu waliyoyafanya.
Nyerere, I dont think is one of them. Kwa hilo namheshimu sana, na kweli wafu wawazike wafu wenzao. Matatizo ya leo tuyapatie ufumbuzi basing on what is prevailing today? Tunaionaje hii hali ya siasa na the so called wafadhili wa wanasiasa? Mi nachoka kabisa! Na katika hayo, Is there anything to do with Nyerere?
 
Back
Top Bottom