Jay Mo ameniskitisha sana

inaniuma saana. siku ya shindano la mfalme wa rhymes sugu ndo aliyekuwa anampa saport hadi kumbeba mabegani. angalia video ya DARUBINI KALI utamuona SUGU akimbeba AFANDE SELE. Lakini leo anamgeuka. Kweli sanaa ya bongo yataka moyo. Mwenye access atubandikie hapa video ya DARUBINI KALI watu waone. SUGU alikuwa anamtetea hadi anataka kulia.mia

Ukiacha kagari kamoja alikokapata Afande kama zawadi kwenye Ushindi wake wa kumchakachua Msafiri (Solo Thang) , maisha yake ndio yaleyale tu ya kubangaiza waliyonayo wanamuziki wengine baada ya kudhulumiwa sana na hawa Clouds.
Tuongee tu ukweli, kwa uwepo wa hawa mapromoter wa Couds, mwanamuziki gani anaeweza kujivunia kua uzuri wa maisha yake umechangiwa na hawa matapeli?
Sio Prof. Jay wala Juma Nature.
Kwa mbaali anaweza kua Lady Jay Dee sababu ya kutembea na Ruge + Vipromo vya hapa na pale from Gadner.
 
Mnakumbuka hii mistari ya Afande sele?

"naota ndoto za pesa mpaka naweweseka/mara natupa shuka nastuka/naota Sugu ananiita uku analalamika/mziki bongo haulipi mwanangu mi nang'atuka/duh miguu inakosa nguvu nahisi kama naanguka/kwa vile bila Sugu hapa nilipo nisingefika...

Uyo ndio baba Tunda kwa ambao walikuwa hawamfahamu.... tenda wema uende zako Sugu.
 
Muziki wa Hip-Hop ya hapa kwetu na Bongo Flava kwa pamoja vina historia kidogo.
Inawezekana kabisa kuna baadhi ya waimbaji wa sasa ambao wamezaliwa wakaikuta Bongo Flava ishaanza.
Wapo wasanii wengi tu, wenye historia kubwa tu na huu Muziki ambao kwa namna moja au ingine wamechangia kutufikishia hapa tulipo.
Binafsi hua namkubali sana Juma Mohammed Mchopanga (Jay Mo) kama mojawapo ya waimbaji wazuri wa huu muziki.
Ila ki ukweli huyu Msanii pamoja na kujitahidi kutunga amekua ni kielelezo tosha cha wale wasanii ambao walifanikiwa kimuziki lakini sio kimaisha. Sababu kubwa ya kutofanikiwa kimuziki kupitia uimbaji kwa Msanii huyu ni kutokana na maslahi duni kutoka kwa ma-distrubutors na waandaaji wa matamasha mbalimbali. Distribuors wengi ni wadosi hivyo sihitaji kujua wanawajali vipi watanzania wa asili, but promoters tunawajua ni watanzania wenzetu hivyo inatia uchungu kutuona wakiwanyinya hawa wasanii akiwemo Jay Mo.
Mojawapo ya promoters hao ni Clouds enterainment ambayo binafsi siipendi.
Cha ajabu Jay Mo huyohuyo akijua kua kuna wanaharakati (za kimuziki) wanapinga unyonyaji huo, leo anakuja anajiunga na wanyonyaji hao against wanaharakati.
Jay Mo hakutakiwa kabisa kua hapo alipo kimaisha, lakini sijui kadanganywa na nini kukubali kujiunga na wanyonyaji hao (snitch).
Jay Mo kama kielelezo na kiwakilishi cha wasanii waliofanikiwa kimuziki lakini sio kimaisha umeniangusha sana mimi kama mshabiki wako, na ki ukweli haukutakiwa kabisa uwepo LEADERS siku ya Jumamosi, bali KIJITONYAMA kwa wanaharakati (Vinega).

Shida ni kwamba game ya bongo imejaa vilaza wasio na muelekeo wa maisha. Wengi wanafanya muziki wapate mademu na si kufanya musiki kama kazi na wawe na maisha bora pitia huo muziki. Wasanii wengi wanaendekeza dhiki na hawawezi acha kubali hivo visent toka clouds ndo mana nenda rudi maendeleo yao yatabaki kusuasua. Kujua jinsi gani wasanii wanafanya mziki kupata mademu Jay Moe katika wimbo wake mpya wa FAMOUS ana line inasema "Nimegonga madem wengi kuzidi nakala za Mamu" asa hii ni sifa au ujingaaaa na upunguani wa akili kwa mkongwe kama Jay Moe.
 
hao watt awajielew hiv kwel ktk normal situation linah amemshinda j mo katika mafanikio yA kimusic wakat jmo kaanza music linah ajazaliwa kweli her mungu akunyime vitu vyote akupe hekima na akil leo jmo ana suport watu wAliomnyonya takriban miaka kumi kwel hv vituko
 
hao watt awajielew hiv kwel ktk normal situation linah amemshinda j mo katika mafanikio yA kimusic wakat jmo kaanza music linah ajazaliwa kweli her mungu akunyime vitu vyote akupe hekima na akil leo jmo ana suport watu wAliomnyonya takriban miaka kumi kwel hv vituko

Hii point muhimu sana mkubwa!!
Ukisikiliza falsafa za mashairi ya wimbo kama MVUA na JUA ya Jay Mo utaamini hata Diamond akae chini miaka 100 hawezi kutunga kitu kama kile.
Lakini kwa akili zilezile za kushikiwa anaibuka na kuwashabikia wanyonyaji.
 
asilimia kubwa waliomtosa sugu wana nidhamu ya uoga..wanawaza kesho watakula nin incase nyimbo zao zisipopigwa kwenye ile redio ya mabishoo na tv yao..sio kosa lao
 
Kinachoniboa Jaymo anajisifia kwa nyumba ya urithi, hana elimu, hana gari hana nyumba, hana hata mke. hana responsibilities zozote, anasubiri hela ya pango kila mwezi basi. jina kubwa afu huna kitu. haujagundua tu kwamba unanyonywa na hao wafu fm?
 
Mnakumbuka hii mistari ya Afande sele?

"naota ndoto za pesa mpaka naweweseka/mara natupa shuka nastuka/naota Sugu ananiita uku analalamika/mziki bongo haulipi mwanangu mi nang'atuka/duh miguu inakosa nguvu nahisi kama naanguka/kwa vile bila Sugu hapa nilipo nisingefika...

Uyo ndio baba Tunda kwa ambao walikuwa hawamfahamu.... tenda wema uende zako Sugu.

Yaani afande amenisikitisha sana,na nimemchukia sana sana sana msaliti mkubwa hana hata aibu?Sugu moto chini na wataisoma namba kudadadeki.
 
Kwa hakika, tangu ile siku nimemchukia afande sele totaly! Nilikuwa na nyimbo zake nyingi sn na nilikuwa namkubali kimziki ile mbaya! Lakini ss nimefuta na kuchoma moto kila kitu kinachomhusu afande. Sugu kaza buti, masnitch watakutosa ila waelewa tutakuwa pamoja nawe mwanzo mwisho!
 
msiwalau sana wanamuziki wetu kwani mwanamuziki yeye kama yy ni ngumu kusimamama peke yake kupigania maslahi yake kwa mfano promoter anaweza kusain ideal na mwanamuzk akamlipa 2million lakini jamaa akaingiza 30million, kutokana na uelewa mdogo wa mwanamuzk na pengine hajawahi kupata kiasi cha pesa kama hicho akaona ni nyingi kumbe mwenzake ametengeza mara 15 yake. Dunia zima watu waoitwa mapromoter ni wanyonyaji sema wenzetu wa mamtoni wanakuwa na maneja na wanasheria wanaowasadia kuingia mikataba.

Mkomavu upo sahihi sana kwa hicho unachokisema Cha msingi kwa wanamuzi hao kujiunga pamoja chini ya mwamvuli mmoja kupigania maslahi yao. Nafikiri wengi wao wataelewa jitihada za Sugu baada ya muda mrefu sana. Kinachosikitisha ni kuwa bangi na elimu ndogo ndo vinavyowamaliza kina Jay Mo. Yupo tayari kupoteza milioni 30 kwa ajili ya milioni 5 ya haraka. Wanatakiwa wafikiri nje ya box la sivyo wataendelea kuwa kicheko mtaani. Ukiwa hapa Namibia utagundua kuwa haki miliki kwa wasanii inawasaidia sana. Mikataba ipo vizuri na wengi wao wanafanya vizuri sana kwa kuwa wanajua haki zao. Siyo tu kuwalaumu Clouds FM bali media houses zote - tv na radio. Kila wanapotumia nyimbo za wasanii wanatakiwa wawalipe na siyo presenters kutangaza sifa kibao za mwanamuzi lakini wanashindwa kutafsiri sifa hizo in monetary terms. Wauzaji wa kanda na wanaorekodi mitaani wanatakiwa wadhibitiwe kwa kiasi kikubwa ili kuongeza kipato cha kina Mchopanga. lakini kama watakubali kuendelea kutumiwa kama kondom hawawezi kufika kokote
 
tatizo la hawa wasanii wa bongo ni elimu, shule hakuna vichwani mwao, kwao wao hawafanyi muziki kama ajira(kazi), kwao wao wanafanya muziki ili wasukume maisha siku ziende mbele. Kwao wao akijitokeza mtu yeyote akawapa hela ya kula kwa siku basi watamthamini huyo kuliko hizo harakati unazoongelea. Na matajiri wa mjini kwa vile wanaujua udhaifu huo wa wasanii wa kibongo basi wanautumia kuwavuruga na kuwapotezea dira. Ukiwa na elimu, ukajitambua wewe ni nani, ukatambua upo hapa duniani kufanya nini, ukatambua haki zako ni zipi......hakuna ataethubutu kuharibu dira yako.
So, mwambie jay mo aende shule.

wanaridhika na ulevi wa sifa za kishabiki.
 
Kinachoniboa Jaymo anajisifia kwa nyumba ya urithi, hana elimu, hana gari hana nyumba, hana hata mke. hana responsibilities zozote, anasubiri hela ya pango kila mwezi basi. jina kubwa afu huna kitu. haujagundua tu kwamba unanyonywa na hao wafu fm?

Ngwea alimpa kagar awe anazugia kipindikile haja amia sinza
 
Shida ni kwamba game ya bongo imejaa vilaza wasio na muelekeo wa maisha. Wengi wanafanya muziki wapate mademu na si kufanya musiki kama kazi na wawe na maisha bora pitia huo muziki. Wasanii wengi wanaendekeza dhiki na hawawezi acha kubali hivo visent toka clouds ndo mana nenda rudi maendeleo yao yatabaki kusuasua. Kujua jinsi gani wasanii wanafanya mziki kupata mademu Jay Moe katika wimbo wake mpya wa FAMOUS ana line inasema "Nimegonga madem wengi kuzidi nakala za Mamu" asa hii ni sifa au ujingaaaa na upunguani wa akili kwa mkongwe kama Jay Moe.
Wlijua Leaders kutakuwa na mademu kibao na ndio kilichowapeleka,
 
its not late Tuwashauri warudi Kundini wale waliopotea
Ni njaa tu ndo imewaondoa
 
Ngwea alimpa kagar awe anazugia kipindikile haja amia sinza

hahahaaaa...!! kumbe mkuu ile gari unaifahamu..basi ile gali yao kama walibambikiziwa vile sababu ilipo halibika dar es salaam nzima walikosa spea. ilikuwa imepaki pale gereji kijito nyama sijui siku hizi ipo wapi. Lile gari lilikuwa ni kijiwe cha kuvutia ganja.
 
Wapumzike kwa amani popote walipo ma snitch wakubwa hawa.
Watakuja kujitambua mvi zikiota kichwani huku mafanikio yao wakiyasoma kupitia Ruge.
 
Mziki wa bongo, pumba tupu. Wao acha watoe ngoma kali, wa2 tu bang ila mifukoni wabaki chali!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom