Jasusi la kitanzania lilivyowatoka wanajeshi Uganda

Prince Mhando

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
9,645
12,208
"Tuliamuriwa kutoka nje ya jengo kupitia mlango wa bustanini na majasusi wa shirika la ujasusi la Idi Amin.
Nje ya jengo kulikuwa na bustani nzuri iliyojaa miti midogo midogo na barabara zenye kokoto. Mbele yetu hatua kama 200 hivi iliegeshwa Land Rover.
Koplo Sudi akawa na kiherehere, akatangulia kuifata Landrover hiyo akifuatiwa na Sajini Binda.
Mimi nilikuwa nyuma yao lakini mawazo yangu yalihisi kuna hatari mbele yetu, haiwezekani watuachie kirahisi namna ile.
SAJINI BINDA NA KOPLO SUDI WAUAWA BAADA YA KUISOGELEA LANDROVER
"Wakati akili yangu ikiwaza bila kupata majibu, ghafla nikamwona Koplo Sudi ambaye alikuwa anajitayarisha kuingia ndani ya Landrover hiyo akianguka chini.
Kabla sijamuangalia vizuri, nikasikia Sajini Binda akitoa sauti ya kung'aka na kuanguka chini.
Bila kuzubaa nikaruka na kujiviringisha kama gogo linalobiringika kutoka mlimani.
Niliingia uvunguni mwa Landrover na kusikilizia wakati huo Koplo Sudi na Sajini Binda walikuwa wamelala kando huku damu zikiwavuja kwa wingi.
Utulivu waliouonesha na damu zilivyokuwa zikiwatoka nilijua kuwa wameshakufa.

JASUSI LA KITANZANIA LAWATOROKA WANAJESHI WA UGANDA KININJA

"Sasa milio ya bunduki na risasi kutoboa gari hilo zilisikika vizuri masikioni mwangu lakini gari halikulipuka.
Hii ilidhihirisha kuwa Landrover hiyo iliwekwa hapo kama chambo tu, haikuwa na petroli na labda hata haikuwa na injini.
Kilichonishangaza ni jinsi risasi hizo zilivyonikosa, sijui wapigaji hawakuwa na shabaha au ni Mungu tu.
"Huu ndio mlango wa bustanini, mlango wa mauaji unaotumiwa na wauaji wasioonekana wakiwa na bunduki zisizotoa mlio," nilijisemea kama mwehu kisha kama umeme nilitoka hapo uvunguni na kukimbia kwa kasi kwa mtindo wa zigizaga.
Risasi zilivuma karibu yangu na moja ikanipata begani lakini sikusimama.
Niliacha barabara inayoelekea kwenye mlango ambako kulikuwa na kibanda cha walinzi, nikapinda upande wa kushoto bila kujua ninapoelekea.
Walinzi hao waliponiona nao walianza kunifyatulia risasi ambazo zilitoa sauti ya kutisha lakini Mungu alikwishasema hapana.
Maofisa Usalama wa Taifa wa Idi Amin nao hawakukubali kunikosa, walikuja nyuma yangu kwa kasi sana lakini kwa vile nilishawaacha mbali hawakufanikiwa kunipata.

ARUKA SENG'ENGE ZENYE MIIBA NA KUDANDIA LORI HUKU RISASI ZA WANAJESHI WA ZIKIMKOSA KOSA

"Nilipofika kwenye seng'enge zenye miiba na urefu wa kama mita mbili hivi kwenda juu nikashtukia naruka kama karatasi kwenye upepo na kujikuta naangukia upande wa nje wa eneo hilo la wauaji.
Bila ya kufanya ajizi nikainuka na kutimua mbio huku risasi zikiendelea lakini hazikunipata.
Nilikimbia mbele zaidi nikatokea kwenye barabara kubwa ya lami ambako nililiona lori moja lililobeba mifuko ya saruji likijikongoja.
Niliongeza kasi ya mbio na kulirukia nyuma ambako nilijibwaga juu ya mifuko hiyo ya sementi huku nikitweta.
Nilipotazama nyuma sikuwaona maadui zangu hivyo nikajua wameenda kufuata magari ili wanifate.
Tulipita eneo lililoandikwa Nakulabye na baadae tukaelekea barabara inayoelekea eneo liitwalo Bombo lakini tulipofika eneo la Namirembe, lori likaanza kupunguza mwendo, nikahisi linakaribia kusimama.
Niliruka haraka na kuanza kutembea kufuata barabara ya Balintuma hadi kwenye mzunguko wa barabara iliyooneshwa kwa kibao inaelekea Chuo Kikuu cha Makerere.
Baadhi ya watu walinishangaa kutokana na damu ilivyokuwa ikinitoka lakini mimi nilisonga mbele huku nikiwakwepa polisi na askari wengine waliovaa sare.

AINGIA KANISANI NA KUANGUA KILIO KILICHOMSHITUA PADRE

"Ghafla bila kutarajia nikaona bango kubwa mbele yangu limeandikwa 'Namirembe Cathedral'.
Nilihisi hapo ndipo mahali pekee napoweza kuonewa huruma. Nikaangazo macho huku na huku kuthibitisha hakuna anayenifuata au kuniangalia kisha haraka nikaingia kwenye mlango wa uwa wa ukuta wa kanisa hilo ambako ndani nilikuta ibada ikiendele kukiwa na waumini wapatao hamsini huku padre wa kizungu akiongoza ibada.
Nikatafuta sehemu nzuri ya peke yangu nyuma kabisa na kusikiliza ibada hiyo iliyokuwa ikiendeshwa kwa lugha ya Kiingereza.
Mwisho wa ibada watu wote walitoka nje lakini mimi nikabaki ndani na kupiga magoti nikainamisha kichwa chini na kuanza kububujika machozi kama bomba la maji lililopasuka.
Nililia sana na hatimaye nikalia kwa sauti kubwa.
Kilio changu hakikuwa cha kumuomba Mungu bali maumivu, njaa na uchovu ambao binadamu mwenye afya ya kawaida lazima angezimia.

PADRE AMSAFISHA JERAHA NA KUMTOA RISASI MWILINI

"Baada ya kama nusu saa nikasikia mtu akinisemesha na kunigusa kwa mkono begani kisha akaniinua kichwa.
"Pole sana kijana, umepatwa na nini?" aliniuliza mtu huyo kwa kiingereza.
"Umetoka wapi na umeumia na nini?" aliniuliza.
Nilimuomba kwanza anisaidie chakula na matibabu ya jeraha nililokuwa nalo kisha nitamueleza kilichonisibu.
Alinitoa nje ya kanisa na kunipeleka kwenye jengo moja la ghorofa ambapo alinipa chakula na kunisafisha jeraha ambapo alinitoa risasi moja mwilini".
Nukuu ya jasusi wa Tanzania aliyetekwa nyara na wanajeshi wa Uganda.
 
"...Mlango ulifunguliwa na askari sita waliovalia kivita wakiwa na bunduki aina ya AK 47 kila mmoja wakatuzunguka. Moyo ulinilipuka, mate yakanikauka. "Simama juu". Alituamuru askari mmoja aliyekuwa na cheo cha Sajini. Tulitolewa nje ambako tulikuta askari wengine wanane waliovalia kivita wakiwa na bunduki mikononi. Raia wa kijiji hiko walisimama kwa mbali sana wakishuhudia tunavyokuwa mateka mpakani. Tuliingizwa katika lori moja la kijeshi na safari ya kupelekwa kusikojulikana ikaanza. Baada ya mwendo wa kama kilomita nne hivi, tukaingia katika kambi ndogo ya jeshi inayoitwa Kabiyanda. Tuliteremshwa kwenye gari na kuingizwa katika kijumba cha mabati matupu ambapo ndani kulikuwa na joto kali pamoja na hewa nzito kutokana na kutokuwa na dirisha bali vitundu vidogo vipatavyo sita.
Luteni awakabidhi kwa Koplo awafunze adabu.
"Saa tisa tulitolewa humo kwenye kijumba na kukalishwa chini kwenye uwanja niliohisi ni wa kufanyia kwata. "Nani mkubwa kati yenu?" alituuliza Luteni mmoja mweusi mwenye sura mbaya. Hakuna aliyemjibu hivyo akatuona tumemdharau, akaamua kumwita Koplo mmoja aliyekuwa amesimama kwa mbali. "Funsa adabu hawa" alimwamuru koplo huyo kwa Kiswahili kibaya kisha akaondoka zake kwa hasira. "Ah! Mnataka 'kufunswa' heshima, hebu simameni". Tuliinuka kwa hofu huku tukimwangalia anachotaka kutufanya. "Nyinyi ni askari?", "Hakuna askari kati yetu" nilimjibu kwa hasira. "Eh! Wewe ndiyo mkubwa eenh!" ,"Mkubwa wa nini?" nilimjibu na kumfanya acheke.
"O.K nyinyi mnajua Kiswahili kingi sana, hebu chuchumaeni chini huku mkishika masikio yenu". "Tuoneshe mfano", nilimwambia bila hofu.
"Eh! Nyinyi jeuri sana, hebu laleni chini niwachape fimbo" alituambia huku akitabasamu. Wakati tunalala ghafla alikuja askari asiyekuwa na cheo na kumwambia mwenzake tunatakiwa tupakiwe ndani ya gari na kupelekwa kambi ya Mbarara".
Waswekwa mahabusu na kuhojiwa na maofisa wa jeshi la Uganda.
"Tulifikishwa kambi ya Mbarara giza likiwa limeshaingia, dereva akasimamisha gari nje ya lango la kambi kubwa ya jeshi ambayo baadae niliitambua inaitwa Simba Battalion. Taa kubwa ya usalama ikawashwa na kuzimwa kama ilivyo katika kambi nyingi za jeshi kisha sauti kali ilitaka utambulisho.
"Tumeleta mateka kutoka Kabale" alijibu askari mmoja aliyekaa mbele. Gari iliingia na kuegeshwa nje ya jengo dogo ambalo hata asiyekuwa askari angegundua ni mahabusu.
Tulitelemshwa kwenye gari na kuingizwa mahabusu. Asubuhi ilipofika tulitolewa nje na kupelekwa katika ukumbi mmoja mdogo na kukalishwa chini. Dakika chache baadae waliingia wanajeshi wanne, watatu wakiwa na cheo cha meja huku mmoja alikuwa kanali.
"O.K Watanzania, tunaanza na wewe, inuka ujibu maswali yetu". Alitamka kanali huyo huku akimuonesha kidole koplo Sudi.
Koplo Sudi aangua kilio baada ya kuzidiwa na maswali ya Kanali wa kiganda.
"'Una kitambulisho chochote hapo ulipo?" aliuliza meja mmoja ambaye ni mrefu zaidi ya wenzake. "Sina kitambulisho". "Sawa, vua shati na suruali yako," aliamuru Kanali huyo. Koplo Sudi akavua suruali na shati na kuviweka mbele yake. "Wewe unafanya kazi gani pale Murongo?" aliuliza meja mwingine aliyekuwa akinukuu maelezo yetu. "Nafanya biashara ya kuuza vitabu sokoni", alijibu Koplo Sudi huku akigwaya. "Unajua sisi tunawafahamu nyinyi vizuri sana, nakuonya usiseme tena uwongo" alifoka kanali. "Jina lako nani?" aliuliza Kanali. "Abdallah Salum" alidanganya Koplo Sudi.
"Hatuna jina la Abdallah katika orodha tuliyopewa, nyinyi wote ni wanajeshi lakini wewe unajifanya mfanyabiashara. Hatupo hapa kufanya mchezo," alifoka Kanali.
"Umeelewa, sasa yajibu maswali yetu kwa ukweli. Jina lako nani na unafanya kazi gani pale Murongo?" aliuliza meja huyo.
Swali hilo lilimfanya Koplo Sudi aanze kutoa machozi.
"Unalia kabla hujateswa, sasa ukiteswa si utakufa kabisa" alitamba meja. Maneno haya hayakupunguza kasi ya machozi ya Koplo Sudi, kwahiyo Kanali akamwambia arudi akae chini".
Nukuu ya jasusi wa Tanzania aliyetekwa nyara na wanajeshi wa Uganda mara baada ya kuvuka mpaka na kuingia Uganda akiwa sambamba na askari polisi wawili; Sajini Binda na Koplo Sudi.
 
"...Mlango ulifunguliwa na askari sita waliovalia kivita wakiwa na bunduki aina ya AK 47 kila mmoja wakatuzunguka. Moyo ulinilipuka, mate yakanikauka. "Simama juu". Alituamuru askari mmoja aliyekuwa na cheo cha Sajini. Tulitolewa nje ambako tulikuta askari wengine wanane waliovalia kivita wakiwa na bunduki mikononi. Raia wa kijiji hiko walisimama kwa mbali sana wakishuhudia tunavyokuwa mateka mpakani. Tuliingizwa katika lori moja la kijeshi na safari ya kupelekwa kusikojulikana ikaanza. Baada ya mwendo wa kama kilomita nne hivi, tukaingia katika kambi ndogo ya jeshi inayoitwa Kabiyanda. Tuliteremshwa kwenye gari na kuingizwa katika kijumba cha mabati matupu ambapo ndani kulikuwa na joto kali pamoja na hewa nzito kutokana na kutokuwa na dirisha bali vitundu vidogo vipatavyo sita.
Luteni awakabidhi kwa Koplo awafunze adabu.
"Saa tisa tulitolewa humo kwenye kijumba na kukalishwa chini kwenye uwanja niliohisi ni wa kufanyia kwata. "Nani mkubwa kati yenu?" alituuliza Luteni mmoja mweusi mwenye sura mbaya. Hakuna aliyemjibu hivyo akatuona tumemdharau, akaamua kumwita Koplo mmoja aliyekuwa amesimama kwa mbali. "Funsa adabu hawa" alimwamuru koplo huyo kwa Kiswahili kibaya kisha akaondoka zake kwa hasira. "Ah! Mnataka 'kufunswa' heshima, hebu simameni". Tuliinuka kwa hofu huku tukimwangalia anachotaka kutufanya. "Nyinyi ni askari?", "Hakuna askari kati yetu" nilimjibu kwa hasira. "Eh! Wewe ndiyo mkubwa eenh!" ,"Mkubwa wa nini?" nilimjibu na kumfanya acheke.
"O.K nyinyi mnajua Kiswahili kingi sana, hebu chuchumaeni chini huku mkishika masikio yenu". "Tuoneshe mfano", nilimwambia bila hofu.
"Eh! Nyinyi jeuri sana, hebu laleni chini niwachape fimbo" alituambia huku akitabasamu. Wakati tunalala ghafla alikuja askari asiyekuwa na cheo na kumwambia mwenzake tunatakiwa tupakiwe ndani ya gari na kupelekwa kambi ya Mbarara".
Waswekwa mahabusu na kuhojiwa na maofisa wa jeshi la Uganda.
"Tulifikishwa kambi ya Mbarara giza likiwa limeshaingia, dereva akasimamisha gari nje ya lango la kambi kubwa ya jeshi ambayo baadae niliitambua inaitwa Simba Battalion. Taa kubwa ya usalama ikawashwa na kuzimwa kama ilivyo katika kambi nyingi za jeshi kisha sauti kali ilitaka utambulisho.
"Tumeleta mateka kutoka Kabale" alijibu askari mmoja aliyekaa mbele. Gari iliingia na kuegeshwa nje ya jengo dogo ambalo hata asiyekuwa askari angegundua ni mahabusu.
Tulitelemshwa kwenye gari na kuingizwa mahabusu. Asubuhi ilipofika tulitolewa nje na kupelekwa katika ukumbi mmoja mdogo na kukalishwa chini. Dakika chache baadae waliingia wanajeshi wanne, watatu wakiwa na cheo cha meja huku mmoja alikuwa kanali.
"O.K Watanzania, tunaanza na wewe, inuka ujibu maswali yetu". Alitamka kanali huyo huku akimuonesha kidole koplo Sudi.
Koplo Sudi aangua kilio baada ya kuzidiwa na maswali ya Kanali wa kiganda.
"'Una kitambulisho chochote hapo ulipo?" aliuliza meja mmoja ambaye ni mrefu zaidi ya wenzake. "Sina kitambulisho". "Sawa, vua shati na suruali yako," aliamuru Kanali huyo. Koplo Sudi akavua suruali na shati na kuviweka mbele yake. "Wewe unafanya kazi gani pale Murongo?" aliuliza meja mwingine aliyekuwa akinukuu maelezo yetu. "Nafanya biashara ya kuuza vitabu sokoni", alijibu Koplo Sudi huku akigwaya. "Unajua sisi tunawafahamu nyinyi vizuri sana, nakuonya usiseme tena uwongo" alifoka kanali. "Jina lako nani?" aliuliza Kanali. "Abdallah Salum" alidanganya Koplo Sudi.
"Hatuna jina la Abdallah katika orodha tuliyopewa, nyinyi wote ni wanajeshi lakini wewe unajifanya mfanyabiashara. Hatupo hapa kufanya mchezo," alifoka Kanali.
"Umeelewa, sasa yajibu maswali yetu kwa ukweli. Jina lako nani na unafanya kazi gani pale Murongo?" aliuliza meja huyo.
Swali hilo lilimfanya Koplo Sudi aanze kutoa machozi.
"Unalia kabla hujateswa, sasa ukiteswa si utakufa kabisa" alitamba meja. Maneno haya hayakupunguza kasi ya machozi ya Koplo Sudi, kwahiyo Kanali akamwambia arudi akae chini".
Nukuu ya jasusi wa Tanzania aliyetekwa nyara na wanajeshi wa Uganda mara baada ya kuvuka mpaka na kuingia Uganda akiwa sambamba na askari polisi wawili; Sajini Binda na Koplo Sudi.

Hivi wewe una akili kweli? Hivi ulishawahi kusikia popote pale duniani polisi anafanya kazi za kishushushu?
 
Back
Top Bottom