Nicky82
JF-Expert Member
- Mar 14, 2009
- 941
- 64
Wakiongea katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo asubuhi, J.Makamba kama m/kiti wa kamati ya bunge ya nishati na madini na Mnyika kama waziri kivuli wa nishati, wamependekeza ni lazima maamuzi magumu yafanyike ili kuwezesha mitambo ya Dowans kuwashwa ili kupunguza makali ya mgao.
Kwa mujibu wa Makamba, mitambo ya dowans inazalisha MW 120 na itasaidia kupunguza makali ya mgao kwa 60-70%.Wote wametambua uwepo wa swala la dowans mahakamani.
Mnyika: Mnyika amependekeza sheria ya uhujumu uchumi itumike katka swala la dowans. Huku akisema kuwa hawezi kwenda deep zaidi, Mniyka alimaanisha kuwa mitambo ya Dowans inapaswa kutaifishwa sbb ya ukweli kuwa mkataba wa dowans/richmond ni wa kitapeli na huwezi kuwa na mgao wakati mitambo iko pale imezimwa.
Makamba: Makamba emependekeza kuwa usainiwe mkataba wa muda mfupi (hata wa miezi 3) na hao wenye mitambo ili kuwezeshwa mitambo kuwashwa maana kama hakutakuwa na mvua, basi Mtera itazimwa by March. Amependekeza uangaliwe utaratibu ambao hauta athiri kesi iliyopo
Wote wawili Mnyika na Makamba wameonyesha kuwa utakuwa ni uzembe na kichekesho kwa nchi kuingia gizani au kuathiriwa na mgao wakati iko mitambo ambayo imezimwa huku viongozi wa juu wakikaa kimya na kushindwa kuchukua maamuzi magumu.
Wadau hizi hoja mnazionaje?
Kwa mujibu wa Makamba, mitambo ya dowans inazalisha MW 120 na itasaidia kupunguza makali ya mgao kwa 60-70%.Wote wametambua uwepo wa swala la dowans mahakamani.
Mnyika: Mnyika amependekeza sheria ya uhujumu uchumi itumike katka swala la dowans. Huku akisema kuwa hawezi kwenda deep zaidi, Mniyka alimaanisha kuwa mitambo ya Dowans inapaswa kutaifishwa sbb ya ukweli kuwa mkataba wa dowans/richmond ni wa kitapeli na huwezi kuwa na mgao wakati mitambo iko pale imezimwa.
Makamba: Makamba emependekeza kuwa usainiwe mkataba wa muda mfupi (hata wa miezi 3) na hao wenye mitambo ili kuwezeshwa mitambo kuwashwa maana kama hakutakuwa na mvua, basi Mtera itazimwa by March. Amependekeza uangaliwe utaratibu ambao hauta athiri kesi iliyopo
Wote wawili Mnyika na Makamba wameonyesha kuwa utakuwa ni uzembe na kichekesho kwa nchi kuingia gizani au kuathiriwa na mgao wakati iko mitambo ambayo imezimwa huku viongozi wa juu wakikaa kimya na kushindwa kuchukua maamuzi magumu.
Wadau hizi hoja mnazionaje?