Hizi kauli zinanikumbusha anguko la Sadam Hussein, yule Waziri wake wa habari Bwana Aziz (kama sijakosea jina).
Huwezi kusema CUF kina nguvu Zenji kwani tunavyoelewa 1995 kilishinda kulingana na habari kutoka vyombo vya kimataifa wakadhurumiwa wakaandamana wakabutuliwa na polisi wakafyata CCM ikatawala, 2010 walishinda wakadanganywa wakakubali ndoa na ndo ukawa mwisho wao, usitegemee kama CUF itaimalika labda Maalim Seif na Lipumba wapigwe chini wapatikane viongozi wengine wenye mtazamo tofauti na hao.Nimevutwa kusema haya kwani CDM kushika dola 2015 ni sawa na ndoto za mchana,huu ni ujanja wa kuwatia moyo wanachama ili wasikate tamaa,nayasema haya kwa kulinganisha nguvu yakisiasa kwa wapinzani kati ya zanzibar na bara,nguvu ya wapinzani zanzibar ni kubwa huwezi kulinganisha na hawa ndugu zangu CDM wanao jipa moyo japo kupeana matumaini lakini ndio hao kila siku wanafurukuta na wanachemka,CDM jaribuni kulinganisha pumzi yenu na CUF kule zanzibar kisha mjipange upya muache ndoto zenu za kushika dola 2015
Baba yake alimwachia yeye atawaachia wanae sasa sisi ambao hatuna majina ya Makamba kwisha habari yetu!!!! Vijana wengi wanakimbia usultani na wizi uliokidhiri ndani ya ccm