Hi wanaJF
Kuna uvumi ambao unaenea kwenye jamii kuwa "CCM ni wezi wa kura na hata watu wapigie kura vyama vingine lakini mara nyingi CCM hufanya kila namna anatangazwa mgombea wao kuwa mshindi"
Pamoja na ukweli ilioko katika jambo hilo lakini tumegundua mpango wa CCM (katika jimbo letu) kutumia jambo hilo kama mtaji kwao. Wameamua kueneza taarifa kuwa hata iweje CCM wataiba kura na watashinda. Lengo ni kuwakatisha tamaa watu wasiotarajia kuwapigia kura ili wakate tamaa ya kupiga kura. Hii ni falsafa ambayo hutumiwa hata katika ajira ambapo baadhi ya watu hupenda kueneza uvumi kuwa kazi fulani tayari imeshaandaliwa mtu ili kudiscourage watu wasiapply inapotangazwa au wasiattend interview na matokeo yake wanapunguza ushindani kwa watakaojitokeza! Kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa kwani kwa sasa vijana wengi wakiulizwa kama watapiga kura wanasema haina haja ya kwenda kupoteza mda wakati mshindi hatokani na kura. Hii ina maana kuwa CCM watashinda kirahisi kwani wengi wa wapinzani wao hawatapiga kura.
Ushauri: Hata kama una hakika kuwa utakayempigia kura hatashinda, we piga kura kwani idadi ya kura itampa moyo na hamasa ya kujaribu tena.
Hata kama wataiba, kazi ya kuiba itakuwa ngumu kadiri margin ya kushindwa kwao itakavyokuwa ngumu.
TUJITOKEZE KUPIGA KURA
Kuna uvumi ambao unaenea kwenye jamii kuwa "CCM ni wezi wa kura na hata watu wapigie kura vyama vingine lakini mara nyingi CCM hufanya kila namna anatangazwa mgombea wao kuwa mshindi"
Pamoja na ukweli ilioko katika jambo hilo lakini tumegundua mpango wa CCM (katika jimbo letu) kutumia jambo hilo kama mtaji kwao. Wameamua kueneza taarifa kuwa hata iweje CCM wataiba kura na watashinda. Lengo ni kuwakatisha tamaa watu wasiotarajia kuwapigia kura ili wakate tamaa ya kupiga kura. Hii ni falsafa ambayo hutumiwa hata katika ajira ambapo baadhi ya watu hupenda kueneza uvumi kuwa kazi fulani tayari imeshaandaliwa mtu ili kudiscourage watu wasiapply inapotangazwa au wasiattend interview na matokeo yake wanapunguza ushindani kwa watakaojitokeza! Kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa kwani kwa sasa vijana wengi wakiulizwa kama watapiga kura wanasema haina haja ya kwenda kupoteza mda wakati mshindi hatokani na kura. Hii ina maana kuwa CCM watashinda kirahisi kwani wengi wa wapinzani wao hawatapiga kura.
Ushauri: Hata kama una hakika kuwa utakayempigia kura hatashinda, we piga kura kwani idadi ya kura itampa moyo na hamasa ya kujaribu tena.
Hata kama wataiba, kazi ya kuiba itakuwa ngumu kadiri margin ya kushindwa kwao itakavyokuwa ngumu.
TUJITOKEZE KUPIGA KURA