Jane Mponzi wa Vodacom is no more!

du nafasi ya kazi hiyo. job seekers kazi kwenu


Jamani! Ni lazima useme jambo? Si ukae kimya tu? Ila umenikumbusha jambo.

Siku moja niliingia ofisi moja mahali nikakuta kuna staff amefariki. Waliweka picha ya huyo dada na maua na kadi kibao meza aliyokuwa anakaa. Akaingia staff mmoja alikuwa safari, akaonyesha masikitiko yake kuwa - ooh, its so sad, she was so gooood. Mwenziye akamwambia yeah, that's true, ila tumeshatangaza nafasi yake ya kazi. Hapo hata mwezi haujapita tangu afariki dada wa watu.

Nilijifunza jambo katika hilo. Afya yako ni yako mwenyewe, maisha yako ni yako mwenyewe. Tunza afya na maisha yako, ukiondoka wanakusahau siku hiyo hiyo...siyo unakaa ofisini masaa 20 na deadlines zinakuua, ukifa wanakuwekea maua wanatangaza nafasi yako.
 
Rest in peace Jane. Maskini, siamini umetutoka. ni siku nyingi nilikuwa sijakuona zaidi ya miaka 10, ila tabasam lako bado nalikumbuka. Mungu awape faraja familia ya Mponzi na wote mlioguswa na msiba huu.
 
Gama na mwenzake john komba watakufa mapema kama hawatabadilia style ya maisha yao......wana ongezeko na mlindikano mkubwa wa mafuta mwilini mwao..ambao ndio inachangia kwa kasi kikubwa heart attack.....na kwa komba ni mbaya zaidi maana mbali na kuwa na mwili ule pia ni mzinzi wa kutupwa......kitendo kile kina consume msukumo mkubwa damu na mtu kama yule vains zake hazipitishi damu balabala....soon he'll die kwa heart attack

Bongo vya kukuua vingi tu. Unaweza kukwepa unene ukaishia kufa kwa kemikali za mwenyue mbogambaga za msimbazi, ukakwepa taifodi, ukaishia kufa kwa ngoma uliyoipata wakati ukutafuta mchumba au kuuguza nduguyo; ukakwepa sulua, ukafa kwa kupoteza pumzi ukiwa kwenye ukumbi wa disko, ukakwepa malaria, ukaishia kufa kwa mafuriko au ajali ya daladala..., ukakwepa kukifua kikuu, ukafa kwa mtindio wa mawazo (stress) zitokanazo na majukumu ya kifamilia au kiofisi au kukwazwa na mume/mke/mchumba/boy/girl friend..ukajitahidi kuwahi hospitali kila ukiumwa kuogopa kufa, lakini ukafia wodini ukisubirio daktari ambae yupo kwenye mgomo au kwa kukosa dawa (tiba)..

......vyanzo vya kifo Bongo hauhitaji kuhoji na usione watu wanapenda kuishi maisha wanayoishi...
 
Poleni wafiwa, hasa watoto. Its so sad watoto kukosa wazazi.
BTW, Iringa ndiyo nyumbani kwao au kwa marehemu mumewe? Naona kama jina la marehemu mumewe halikukaa ki Iringa vile.

Huyu Dada ni Iringa na ninadhani kutoka Mufindi. Mponzi maana yake "Mhunzi" kwa kimombo tunaita "Iron Smith"
 
Dada yetu Mpendwa Jane Mponzi aliyewahi kufanya kazi VODACOM amefariki dunia ghafla jana asubuhi,Ndugu wa karibu wamesema alipatwa na "Heart attack" Jane aliolewa na Herry Makange (Marehemu) aliyekuwa Channel 10 na alifariki kwa ajali ya Boda boda Tegeta. Msiba upo Oysterbay Barabara ya Msasani Baada ya Jackies Bar unaingia mtaa wa kulia kabla ya kile kilima maarufu. MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMEN!

Natumaini naye aliwahi kuwa MwanaJF kwani alikuwa mtu wa Mtandao
Jaman hata kuamini inakuwa ngumu! R.I.P Jane, jirani yangu tuliecheza wote long time kitambo pale Msasani Road, ninyi mkiwa #45 karibu na Jaji Kiongozi wakati ule, Barnabas Samatta, #47! Pole pia Grace, mdogo wa Jane, ww ndo mama mdogo wa Melanie, take a good care of her. Lol, mama yake Jane alifariki kwa ugonjwa huo huo miaka michache iliyopita!
 
Yaaah! Heart Attack kwa umri gani? Yo Yo hujakosea, ukweli hua unauma bt bora useme tu atakae nuna anune, jamani tuangalie afya zetu, tusile kwa time bali kwa njaa, tufanye mazoezi na tuchague vyakula na kuskip meal kama huna ulazima wa kula. Hakika tutakufa mapema kwa unene wa aina hii vile ni ugonjwa tayari hata kama unatembea. Tusimlaumu Mungu kwa kila kitu. RIP JANE
 
Mimi nilitegemea mniunge mkono kwa kuweka angalizo kwa sisi tuiobakia......hivi vifo vya ghafla vinaweza kuepukika....haya ndio nyie marehemu kafa na ukimwi mnasema kafa kwa kisukari....na makaburini kafa mwizi/mla rushwa,mzinzi,mshirikina mnasema Mungu amlaze mahala pepa peponi....mna utani na Mwenyezi Mungu nyie.....dada Jane kweli katutangulia lakini nasisitiza na sisi tuwe waangalifu na milo yetu.....ili tuepukane.....
siwezi kusema apumzike kwa amani maana imani yangu inaniambia mtu akisha kufa roho yake itahukumiwa kutokana na matendo yake......Mungu mwenyewe ndio anajua wapi atamuweka.....

maandishi yako yanaonesha dhahiri umezaliwa mwaka gani,kweli wewe yo yo a.k.a Rapa,ndo shida ya kuwa na under 18 humu.
 
Gone too soon.JPG
Wakati wa uhai wao mke na mume.
 
Duh dada alikuwa amenona ee mola tusaidie na haya ma castle light bila tbs
rip jane popote ulipo
 
dada yetu mpendwa jane mponzi aliyewahi kufanya kazi vodacom amefariki dunia ghafla jana asubuhi,ndugu wa karibu wamesema alipatwa na "heart attack" jane aliolewa na herry makange (marehemu) aliyekuwa channel 10 na alifariki kwa ajali ya boda boda tegeta. Msiba upo oysterbay barabara ya msasani baada ya jackies bar unaingia mtaa wa kulia kabla ya kile kilima maarufu. Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi amen!

Natumaini naye aliwahi kuwa mwanajf kwani alikuwa mtu wa mtandao.

ndugu zangu
polen wafiwa a msiba huu mkubwa..nimesoma baadhi ya mada vifo vya mumewe na mama yake ..
Naomba watanzania tuwe macho tuwe makini ....iwapo unajua babako ama mamko amekufa na kisukari ama ugonjwa wa moyo jitahdi sana kujihadhari na vishawishi husika na hili litasaidia kuondoa vile vifo vya hata mamake alikufa hivyo hivyo.....
Ukiangalia kilichomuua jane ni spirit of death ya heart attack..ambayo akiwa hai alipoona mama ke aliondoka hivyo alitakiwa kusimama na mungu nakuachana na maisha ama vyakula vinavyokaribisha ugonjwa moyo.....mungu awalaze wote mahali pema peponi
 
Would you please shut up and respect the dead!

Umeanza kutaka kujua yeye ni nani and why the special treatment, then amejitakia kifo do you know her background and the surrounding circumstances that lead to her death?

RIP Jane

its true, watu hawajui background ya m2 wanaropoka 2. RIP dia sis..
 
ni wakati sasa wa wabongo kuacha kula vyakula vya barabarani chips,kuku na mafuta mengine....pia kuanza mazoezi sio kushinda bar na kunywa pombe.....imagine dada kama huyu kafa kifo cha kujitakia naweza kusema.......kama angefuata kanuani za mlo ulio bora na kushiriki mazoezi inawezekana kabisa leo hii engekuwa bado yu hai.....heart attack nyingine sisi wanadamu tunazitafuta......

Watz mpunguze altitude yenu ya kuwa mwenye kitambi ndio mwenye afya....ati ukiwa mnene ndio una afya....rip dada jane....

Kwa hakika heshima yako kwa wengine ni kiduchu!
 
Gama na mwenzake john komba watakufa mapema kama hawatabadilia style ya maisha yao......wana ongezeko na mlindikano mkubwa wa mafuta mwilini mwao..ambao ndio inachangia kwa kasi kikubwa heart attack.....na kwa komba ni mbaya zaidi maana mbali na kuwa na mwili ule pia ni mzinzi wa kutupwa......kitendo kile kina consume msukumo mkubwa damu na mtu kama yule vains zake hazipitishi damu balabala....soon he'll die kwa heart attack

Duuuh imekuwa kweli wore wamefariki.
 
Cardiac arrest, myocardial infarction, stroke, hypertension, diabetes ni magonjwa baba mmoja, mama mbalimbali.
 
Back
Top Bottom