JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala

Status
Not open for further replies.

JamiiForums

Official JF Response
Nov 9, 2006
6,200
4,982
Hapana shaka kuwa kutakuwa na maoni na mawazo anuai juu ya masuala mbalimbali yanayojadiliwa katika Jukwaa hili. Washiriki hawatarajiwi kukubaliana na kila jambo linalojadiliwa! Kwa msingi huo, ili kudumisha mijadala yenye heshima, ubunifu na ushiriki kamilifu, taratibu zifuatazo zimewekwa ili kuwaongoza washiriki wote:

1) Washiriki wanapaswa kutumia lugha ya kiungwana na kistaarabu ili kuhakikisha kuwa heshima na uvumilivu vinatawala katika mijadala.

2) Mpangilio sahihi wa viakifishi (uandishi) na uzingatiaji wa sarufi unatarajiwa kuonekana katika andiko lako, katika hili unapaswa kuwakumbuka wasomaji wako. Ikiwa unaweza kuhoji/kukosoa uandishi wa watu wengine, basi tarajia kuwa uandishi wako unaweza kuhojiwa au kukosolewa pia. Zingatia kuwa unapokuwa mtandaoni (si JamiiForums pekee) wapo watu ambao watahoji ubora wa uandishi wako. Hivyo, unapaswa kusoma tena andiko lako kisha lihariri ili ueleweke!

3) Kuwa mwenye mwenye adabu, mwenye heshima na muadilifu: Unapoamua kuwa mkosoaji au mtoaji wa maoni unapaswa kutambua kuwa wapo watu ambao masuala hayo yanawahusu au kuwagusa kwa namna moja au nyingine. Hivyo, unapawa kuwa mkarimu na kutumia busara ili usiumize hisia za watu wanaosoma andiko lako.

Kubali kuwa na mawazo au majibu yenye kujenga na wala yasiwe makali yenye kumshambulia mtu mwingine au kushambulia mawazo yao. Aidha, epuka kutumia herufi kubwa (CAPS), hati mkolezo au hati mlalo katika andiko lote. Kimsingi, andiko au uzi wako unapaswa kuwa wenye mawazo yenye mantiki yaliyosemwa vizuri. Hivyo, matusi yanayoelekezwa kwa mchangiaji hayakubaliki. Hata kama hukubaliani na mawazo yaliyotolewa na mshiriki mwingine haimaanishi kuwa mtu huyo hayupo sahihi (amekosea). Badala yake unapaswa toa maelezo au mtazamo tofauti ili kuchochea mjadala zaidi.

4) Epuka kutumia utani unaokera (usiofaa), uwapo jukwaani hapa, unakuwa katika mazingira ambayo hauonani ana kwa ana na washiriki wengine. Kwa hiyo, unapofanya utani ni rahisi kwa mshiriki mwingine kuuchukulia kwa mtazamo tofauti.

5) Unapotumia chanzo fulani hakikisha unakirejelea kwa usahihi: Tambua mchango wa mwingine katika andiko lako ikiwa kuna umuhimu. Weka kiungo (link) pale kinapohitajika. Hatuna jukumu la kuthibitisha maudhui yoyote, wala hatutakubali kuwajibika kwayo na wala hatuhakiki usahihi au ukamilifu wa ujumbe wowote au vigezo vya mdau yeyote.

6) Fupisha habari yako: Usipoteze muda wa washiriki wengine kwa kutoa taarifa ndefu inayojirudia rudia. Iweke hoja yako kwa uwazi, kwa ufupi na inayoeleweka.

7) Wapuuze wanachama wasumbufu: Ikitokea mshiriki yeyote jukwaani amekusumbua, tafadhali mpuuze (ignore) kisha toa taarifa kwa wasimamizi wa maudhui (moderators) huku ukiambatanisha na uthibitisho wenye kiungio kinachoonesha ulichofanyiwa ili hatua stahiki zichukuliwe. Aidha, unaweza kubonyeza kitufe cha kutoa taarifa (Report button) ili taarifa ifanyiwe kazi haraka.

8) Epuka kutukana, kushambulia au kukwaza wengine: Maandiko ya chuki na yenye mrengo wa kuwashambulia watu hayatovumiliwa na JamiiForums. Wachukulie (waheshimu) wengine kama ambavyo wewe unataka uchukuliwe (uheshimiwe). Hivyo, kuleta andiko ambalo litachochea muitikio hasi kwa watu wengine inashauriwa kuepukwa.

Jiepushe kutuma kitu chochote ambacho ni kichafu, chukizo au cha kudhalilisha ambacho kinaweza kuvunja haki miliki ya mtu au haki yake ya faragha (privacy). Ikiwa unajiuliza mwenyewe kama jambo fulani linafaa, yawezekana halifai.

9) Uradidi (Urudiaji): Uradidi wa makusudi wa ujumbe usio na maana, ujumbe mfupi sana uanolenga kuongeza idadi ya maandiko yako (posts) au kuwakera wengine hauruhusiwi kabisa. Sambamba na hilo, uradidi wa matangazo ya biashara nao hauruhusiwi kabisa. Hata hivyo, kutangaza ukurasa wako wa biashara inaruhusiwa endapo tu utaomba na kupewa kibali kutoka kwa waendeshaji wa jukwaa hili. Kutumia viungio vya nyuzi za zamani wakati wa mjadala inaruhusiwa, lakini ikionekana viungio unavyovitumia ni vile ambavyo havihitajiki au haviendani jambo husika, basi hili pia litachukuliwa kama uradidi. Vilevile, kutuma uzi wako zaidi ya mara moja huchukuliwa kama uradidi.

ZINGATIA: Ikiwa washiriki watatumia sehemu ya ujumbe binafsi kupaka/kuponda wengine kwa mambo yasiyo ya msingi jumbe zao zitafungwa. Usitume ujumbe wowote binafsi (Private Conversations) hadharani bila kuomba idhini kwa mtu aliyekutumia ujumbe huo.

10) Kuvaa uhusika wa mtu mwingine au kuingilia akaunti ya mtu: Usithubutu kuvaa au kujifanya wewe ni muhusika fulani ikiwa wewe siye. Usivae uhusika wa viongozi wa umma au mwanachama fulani au kutengeneza akaunti maalumu kwa dhumuni la kuwadhalilisha au kuwachafua wanachama wengine na wananchi wengine kwa ujumla. Kitendo cha kufanya jaribio la kuingilia akaunti ya mdau mwingine hakitavumiliwa. Kufanya matendo haya kunaweza kusababisha akaunti yako kufungiwa au kufutwa kabisa.

11) Kuitana Majina kwa mlinganisho: Hairuhusiwi Wanachama kumfananisha mdau aliyeamua kutumia jina fulani na jina jingine au majina yao halisi (aidha ni yao kweli au si yao). Kufanya hivyo kunaweza pelekea ukafungiwa akaunti yako.

12) Mijadala au andiko linaloenda nje ya mada: Hakuna adhabu yoyote kubwa inayotolewa kwa watu wanaotoka nje ya mjadala. Lakini, tuwe wawazi tu kuwa jambo hili halipendezi na linakera. Kama una jambo la kusema lakini haliendani na mada ilyowasilishwa unashauriwa kuanzisha mjadala mpya vinginevyo wazo lako litaondolewa.

13) Kujaribu kukwepa kufungiwa: Unapoingia katika akaunti yako ukakutana na ujumbe kuwa umefungiwa, tafadhali wasilisha ombi la kufunguliwa akaunti yako kwa waendeshaji wa mtandao huu ili kuwa na makuabliano juu ya sababu zilizopelekea ukafungiwa. Mkifikia makubaliano, utaruhusiwa kutumia akaunti yako bila shida. Usijisajili tena kwa jina lingine hata kama mfumo wetu ukikuruhusu. Ukijaribu kujisajili tena na tukakubaini, itasababisha kufungiwa moja kwa moja.

14) Masuala yanayohusu ponografia na utupu: Unakumbushwa kuwa jukwaa hili ni la umma, kuna watoto wenye umri mdogo na watu wazima wenye zaidi ya miaka 60 na kuendelea. Hivyo, masuala yote yanayohusu ponografia na utupu hayaruhusiwi kabisa.

15) Saini na Avata: Hatuna sheria na kanuni za uandishi wa saini wala uwekaji wa ‘avata’. Katika hili unaombwa usitumie Saini au Avata ambazo zitawakwaza watu wengine. Mathalan, saini na avata hizo zisiwe zenye maudhui yasiyofaa, kibaguzi au zinazohamasisha kutenda makosa ya jinai n.k.

16) Maudhui tata: Kwakuwa hatuwezi gusia kila kitu lakini sheria hii inagusia kila jambo... Tambua kuwa hili ni jukwaa la Umma kwahiyo unapaswa kutenda kama mtu ambaye yuko mbele ya macho au umati wa watu. Masuala mengine yote yameachwa chini ya wasimamizi wa maudhui ambayo yanajumuisha mambo yote ya uongo, upotoshaji, matusi, machukizo, udhalilishaji wa kijinsia, kutishia, uvamizi wa faragha za watu au kufanya mambo mengine yanavyovunja sheria na kuchochea uhalifu.

Kumbuka, tunayo haki ya kumfungia mwanachama yeyote kwa kipindi kifupi au moja kwa moja, kukataa andiko lolote lililotumwa, jina ambalo linachukiza au andiko baya.

Tunayo haki ya kuhariri au kufuta andiko lolote au kuweka ukomo wa mjadala wowote na kuufunga kwa sababu yoyote au hata bila sababu, pengine bila ufafanuzi wala onyo.

MSISITIZO: Kama ukikuta kuna mjadala wowote ambao unakiuka misingi iliyowekwa katika andiko hili tafadhali wasiliana nasi ili mjadala huo ufanyiwe mapitio haraka iwezekanavyo.


===============
ENGLISH VERSION
===============


COMMUNITY ENGAGEMENT GUIDELINES ON JAMIIFORUMS DISCUSSIONS

There will no doubt be different views on issues being discussed on this forum. Participants are not expected to agree on all matters. In order to stimulate respectful dialogue, creative thinking and a fully participatory approach, the following rules are set out for all participants:

1) Participants will keep a polite tone and ensure that a sense of respect and tolerance permeates the discussion.

2) Correct spelling, grammar, and style are expected in your writing. However, remember your audience. If you would judge another person’s writing, you can expect that someone is judging yours. Be mindful of how you look online; others will likely judge the tone and quality of your writing. Reread your posts and edit for clarity.

3) Be courteous, respectful and appropriate
Be critical of ideas, but remember there are other people involved. Be tactful and kind. You can hurt the feelings of a person reading your post.

You agree that your comments/ideas and feedback will be constructive and will not sharply criticize or attack another participant or their ideas, avoiding the use of all capital, all bold or italic letters. Criticism must be constructive, well-meaning, and well-articulated. Rants directed at any contributor are highly unacceptable. Just because you do not agree with another participant’s post/opinion does not mean that he/she is terribly wrong. Instead, offer a different perspective to encourage further discussion.

4) Avoid provocative jokes
Because you are not in a face-to-face environment, it’s easier for someone to take something you say the wrong way.

5) If you use a source, cite it properly
Give credit where credit is due. Include links where appropriate. You are solely responsible for the content of your messages. We cannot verify content and thus accept no responsibility for it, nor do we vouch for the accuracy, completeness, or utility, of any message or the qualifications of any user.

6) Be concise
Do not waste people’s time by posting basic, repetitive information. Make your point clearly and quickly.

7) Ignore bothersome members
If there is someone on this forum that bothers you, ignore him/her. Instead, report it to us (Link to a thread elaborating on how to ignore a person on JF or Report a post)

8) Flaming, Bashing, and Trolling
Hate posts and personal attacks will not be tolerated on JamiiForums. Treat others on these forums as you would expect them to treat you. Posting topics specifically designed to provoke a negative response from someone (aka trolling) is also asked to be avoided.

You agree to refrain from posting or uploading anything obscene, hateful, blasphemous, derogatory or uploading anything that is defamatory or libelous or invades another person’s privacy or proprietary rights. If you need to ask yourself whether something is appropriate, it’s probably not.

9) Spam
Purposely spamming a message board with senseless, vacuous, or very short messages to gain a higher post count, or just to annoy others is HIGHLY frowned upon! Commercial spamming and advertising are just as unwelcome. Promoting your site is only allowed with permission of the site owners. Bumping old threads is allowed, but needless bumps will be classed as spam. Double posting any entry is also considered as spamming!

If the members are using the Private Message (Conversations) facility to spam the others with pointless, unsolicited messages they will be banned. If anyone receives one of these messages, please contact moderators immediately. Do not post Private Messages at JamiiForums or elsewhere without the express permission of the sender of the Message.

10) Impersonating Other Users / Accessing another User’s account
You may not impersonate another known public figure or forum member or even create an account specifically for the purpose of provoking other users. Also, attempting to access or using someone else's account is strictly prohibited. You will be banned and your account may be terminated.

11) Name calling
There should be no ‘name calling’ (linking two/more display names or a display name with a real name), doing so will result into a serious ban.

12) Off-Topic Posts
There is no major punishment for off-topic posters. But let’s be honest, it drives us all mad!If you have something to say but it really has nothing to do with the current thread you are in, please open a new thread for it. Otherwise it will just be trashed.

13) Circumventing a Ban
If you log onto the forums and receive a message that you have been banned, please submit an unban request and wait for a staff member to get in touch with you. You may NOT re register under a new name if our software lets you. But, if you try to sign up again and we caught you, then it will result into a permanent ban.

14) Nudity / Porn
Please, remember that this board is a PUBLIC forum. There are 12 year olds here just as there are 60+ year olds. Nudity and porn are prohibited for obvious reasons.

15) Signatures & Avatars
We do not have any specific set of rules regarding signatures. However, we do ask you that it will not be offensive to others. No adult, drug related or racist content please.

16) Questionable Content
Since we can't have a rule to cover everything, this is the rule to, well, cover everything. These are public boards, so act like you would if you were in a public place. These issues are left to the discretion of the individual moderators, but may include any material that is knowingly false and or defamatory, misleading, inaccurate, abusive, vulgar, hateful, harassing, obscene, profane, sexually oriented, threatening, invasive of a person's privacy, that otherwise violates any law, or that encourages conduct constituting a criminal offense.

We reserve the right to ban any user temporarily or permanently, refuse posting from screen names we find offensive, edit or delete any post, limit postings on any topic, and shut down any topic altogether, for any reason, or no reason, without explanation or warning.


IF you find any content that contravenes the above, please CONTACT US so that it gets reviewed ASAP
 
Status
Not open for further replies.
294 Reactions
Reply
Back
Top Bottom