JamiiForums Issues an Official Responce to CCM allegations: (Press Release)

Status
Not open for further replies.
h.sep7.gif
Jamii Forum yaijibu CCM


na Hellen Ngoromera


amka2.gif
MTANDAO wa Jamii Forums umesema madai ya Chama cha Mapinduzi (CCM) yaliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Tanzania Bara), Pius Msekwa, kuuhusisha mtandao huo na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni ya kubuni na yana lengo la kuwatisha Watanzania kutoa maoni yao kwa uhuru kupitia mitandao mbalimbali.
Mtandao huo ulianzishwa mwaka 2006 na madai hayo kwamba mtandao huo unafanya kazi hatarishi dhidi ya CCM na serikali yana lengo la kuuchafua na kuuvunjia hadhi ambayo imejijengea kwa gharama kubwa na kwa muda mrefu.
"…Ni jaribio dhaifu la Chama cha Mapinduzi kubebesha lawama mitandao ya intaneti kwa mapungufu na migongano iliyojitokeza ndani ya chama chao katika miaka michache iliyopita na siku za karibuni," ilisema taarifa hiyo.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, mtandao huo unaotembelewa na wastani wa watu 20,000 kwa siku umekanusha madai hayo kwa maelezo kuwa hayana msingi wala ukweli.
"Tunapinga vikali madai yasiyo na msingi ya Chama cha Mapinduzi kuhusu umiliki, malengo na nafasi ya JF (Jamii Forums) katika medani ya vyombo vya habari nchini na mchango wake katika mijadala ya kisiasa nchini," ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Ilisema kwa mara ya kwanza waliyasoma madai hayo yakiwa yameripotiwa kwenye magazeti mawili ya kila siku.
Kwa mujibu wa mtandao huo hawajawahi kufadhiliwa na CHADEMA lakini wanaamini kuwa wamelengwa na CCM kwa sababu katika miaka mitano iliyopita mtandao wao umekuwa ukishiriki vilivyo kufichua kashfa mbalimbali ambazo zimelindima nchini hatimaye kusababisha chama tawala kuamua kujivua gamba.
Mtandao huo umesema madai hayo yamesomwa na kusikiwa na watu wengi nchini hivyo kuwasababishia usumbufu mkubwa. Yamesababisha wasiwasi usio wa lazima kwa wanachama 40,000 ambao wametawanyika pote nchini na katika kila kona ya dunia.
Madai hayo ya CCM yalitolewa hivi karibuni mkoani Dodoma na Msekwa wakati wa kutambulisha uongozi mpya wa chama hicho.
 
Mwanakijiji, inasikitisha kuona hata vijana wa leo fikra zao zimekuwa za uoga kupindukia. Usishangae hayo ya kuogopa CCM, mfano mdogo wa jinsi CCM ilivyoharibu psych ya watanzania ni pale unapoenda benki na kuona tellers na services mbaya kupindukia na hakuna hata mmoja anayethubutu kumconfront manager au kufunga account kuwalazimisha watambue uzito wao. Watanzania utawasikia wakilalamika huku wakiwa wamekaa kwenye foleni ndefu na ATMs hazifanyi kazi. Mpaka hapo tutakapotambua umuhimu wa kupigania hazi zetu ndio tutabadilika. Press release kama hii ni mojawapo ya njia za kusafisha damage done over many years.
 
Kama nilivyosema awali ni vyema kupitia vielelezo vilivyopo na kufanya maamuzi sahihi. Kwenda mahakamani ni haki ya kila ambaye anaona haki yake imekanyagwa na mwingine bila kujali unyonge wake wala ubabe wa aliyeikanyaga. Katika hili muda unahitajika angalau kujiridhisha kama JF watakuwa na kesi dhidi ya CCM au la. Ni jambo la kisheria ambalo halipaswi kusukumwa na hisia.

Katika hili kuna walalamikaji zaidi ya mmoja, YouTube, Twitter, Facebook na CHADEMA. Wote waliotajwa ni tishio wanaweza kulalamika. Chadema wanaonekana wamesingiziwa kumiliki mtandao ambao sio wao. Huo unasemekana ni uongo. JF wanasemekana kumilikiwa na Chadema wakati si kweli. Je kumiliki au kumilikiwa katika hali hii kuna athari kisheria? Kwa maneno hayo JF/Chadema wamepoteza sifa mbele ya jamii? Huu ni mfano tu nimeutoa. Yote yanawezekana ila ni lazima kuangalia hili suala kwa mapana yake na si hisia.

Wakati hayo yanaendelea hakuna kinachotuzuia kuendelea kuwa JF. Mijadala ndiyo inayotufanya tuwe JF hivyo tuendelee kujadili.
 
JF inajibizana na CCM

kazi kweli kweli

you could have put the other way around.. CCM inailalamikia JF? think abou it.. Chama chenye umri wa zaidi ya miaka 50, wanachama milioni 5, mabilioni ya fedha na hazina kibao ya watu wenye dalili za usomi - inalalamikia JF? Unless you are implying JF is way bigger than the ruling party.
 
you could have put the other way around.. CCM inailalamikia JF? think abou it.. Chama chenye umri wa zaidi ya miaka 50, wanachama milioni 5, mabilioni ya fedha na hazina kibao ya watu wenye dalili za usomi - inalalamikia JF? Unless you are implying JF is way bigger than the ruling party.

Hehehe 'eti wenye dalili za usomi'.
Kweli tumechoka!
 
you could have put the other way around.. CCM inailalamikia JF? think abou it.. Chama chenye umri wa zaidi ya miaka 50, wanachama milioni 5, mabilioni ya fedha na hazina kibao ya watu wenye dalili za usomi - inalalamikia JF? Unless you are implying JF is way bigger than the ruling party.

Hii inaonyesha kwamba hawana cha kuwaeleza wananchi,, ili waweze kuwasikiliza.
 
nimeipenda hii PDF. nimewatumia rafiki zangu kama ishirini ambao kwao mtandao ni shinda. Alishawambie Mdee bungeni kuwa hiki ni kizazi cha Digital Analogue haipo tena...Naona bado magamba yapo...it is still morning:drum:
 
kwa style hii.. watu wasiojiua jf watajiuliza ni kitu gani hicho...? hatimaye watajuwa kumbe kunasehemu we can dare to talk freely , anonymously na kuja kumwaga uchafu wote unaotekelezwa na wala rushwa bila kujali itikadi za chama.. kwa hili nawashukuru ccm wameruka majivu na kukanyaga moto....
 
Melo na mwenzake Mushi walishawai kamatwa na kuhojiwa na police. Tundu lisu chadema ndio mwanasheria wao. Utakataaje kama si mtandao wa chama. Mijadala iwe ya busara si matusi wala uchochezi ulivyo sasa. Hakuna uhuru bila mipaka.
 
Hongereni sana wana JF wenzangu...........majibu murua kabisa hayo..........
 
Wakuu!

Members wa JF wengi wameenda Kidogo Shule. Sio wale wa Kuuza kura kwa T-shirts.
Lazima Tuipinge CCM kwa sababu sera ya CCM ni kulinda zaidi maslahi ya Chama kuliko wananchi.

Mimi siamini kila ainayeipinga CCM ni Chadema! mimi Binafsi siikubali kabasi CCM, Lakini mimi sio Chadema.

Hata leo akaja Koffi Annan Kama mwenyekiti wa CCM, Lazima ataonekana hana maana kwasababu ya Sera hii ya kulinda Maslahi ya Chama.

CCM inatakiwa kusoma alama za nyakati. Hiki kizazi Cha wasomi kinaendelea kukua kila kukicha, Hata kule vijijini wanakopata kura kwa kugawa T-shirts, kile kizazi kinapotea sasa.

Ningewashauri CCM wachukue hii kama changamoto wabadilike.
 
Melo na mwenzake Mushi walishawai kamatwa na kuhojiwa na police. Tundu lisu chadema ndio mwanasheria wao. Utakataaje kama si mtandao wa chama. Mijadala iwe ya busara si matusi wala uchochezi ulivyo sasa. Hakuna uhuru bila mipaka.

Ulijiunga humu siku nne kabla ya Uchaguzi kuokoa jahazi la Chama
 
Melo na mwenzake Mushi walishawai kamatwa na kuhojiwa na police. Tundu lisu chadema ndio mwanasheria wao. Utakataaje kama si mtandao wa chama. Mijadala iwe ya busara si matusi wala uchochezi ulivyo sasa. Hakuna uhuru bila mipaka.

Huku ndio uwezo wa kufikiri na mantiki wa baadhi ya watu na Marando na CCM ni ya Chadema kwa sababu Marando anamtetea Jeetu Patel! ..
 
Melo na mwenzake Mushi walishawai kamatwa na kuhojiwa na police. Tundu lisu chadema ndio mwanasheria wao. Utakataaje kama si mtandao wa chama. Mijadala iwe ya busara si matusi wala uchochezi ulivyo sasa. Hakuna uhuru bila mipaka.

Mipaka ni muhimu, lakini hii mipaka inapangwa na nani - vyama vyote ama CCM pekee?
 
Nawashauri CCM waende kwa Tendwa, wapeleke ombi la kubadilisha jina kuwa Chama Cha Magamba, japo kifupi kitabakia CCM, mbona CCK walifanya hivyo. kidumu chama cha Magamba. lidumu gamba!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom