zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Baada ya kufunguwa nyuzi humu JF tarehe 27-09-2012 "Mengine ya Upinzani yana Ukweli... Polisi wanatumiwa", siku ya pili yake (28-09-2012) niliweka hii update:
Katika hiyo update niliahidi kurudi na kufunguwa nyuzi kuelezea kwa kirefu jinsi "nyuzi" ile ilivyosaidia. Ukweli ni kwamba nyuzi ile isingekuwepo "Jamii Forums" isingepelekea kuwa na "impact" iliyodhamiriwa.
Siku ya pili (28-09-2012) ilibidi watuhumiwa wapelekwe mbio mbio mahakamani asubuhi na mapema, licha ya kuwa jalada lao lilishafikishwa kwa Polisi wapelelezi (mmoja wao anaitwa David) kutoka kwa (DPP) siku mbili kabla likielekeza kuwa watuhumiwa hawana mashtaka ya kujibu na wawachiwe. Cha kusikitisha ni kuwa huyu David amma alikuwa anafanya makusudi kabisa kuendelea kuwazuia watuhumiwa dhidi ya hitimisho la DPP, huyu David ana kila sababu ya kufanya makusudi kwani baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho cha mafuta wanasema toka hii kesi ilipoanza (inawezekana na kabla pia kwani wafanyakazi waliobaki hapo ni wapya) huyu David alikuwa akienda kumiminiwa petroli ya bure mara kwa mara pale pale kituo cha GBP kinachomilikiwa na Bwana Badr, amma huyu David alikuwa na shinikizo kutoka kwa OCD wa Wazo Hill (kahamishwa kituo juzi) ambae nae alikuwa na shinikizo kwa wakubwa zake kuwa asiwawachie, ukweli ni upi? sijui. Lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Walipofikishwa asubuhi hapo mahakamani, mwendesha mashtaka hakuwa na kesi ya kuwasomea wala kuwafungulia kwani ilishaelekezwa waachiwe. Mpelelezi David, badala ya kuwawachia, akawachukuwa tena na kuwarudisha rumande kituo cha Polisi Wazo Hill ili mradi tu, kwanini waachiwe. Hapo ndipo kikundi cha watu waliokwenda mahakamani kuwawekea dhamana hawa watuhumiwa walipopaza sauti zao na kusema leo "mpaka kieleweke" na hatukubali warudishwe Polisi. Mpelelezi David wakati huo anaambiwa maneno hayo alikuwa anatabasamu na kucheka kidharau, kuonesha kuwa ndio wanakwenda na hamna mtachoweza kufanya.
Naomba ieleweke kuwa siku hiyo mahakamani walikuwepo watu wengi waliojitolea kwenda kuwawekea dhamana hawa vijana kiasi cha kustaajabisha, vipi wezi wa Millioni 80 wawe na wadhamini wengi namna hiyo, wake kwa waume? Waliojitolea na kupeleka hati za nyumba zilizothaminiwa walikuwa hawapungui 6, watumishi wa idara za Serikali ambao ndiyo mara nyingi huwa wanatakiwa wa wadhamini watuhumiwa wenye kesi kubwa walikuwa hawapungui 20 kila mmoja na barua ya dhamana, licha ya wafanya biashara na wengineo wengi waliojitokeza kuwadhamini hawa vijana. Wengi wao, habari zilizopelekea wajitokeze kwa wingi ni hizi zilizorushwa Jamii Forums.
Baada ya watuhumiwa kurudishwa tena Polisi pasi na haki, akajitokeza Wakili na kujitolea kufatilia hili sakata kwa RCO hapo Oyster Bay Police, baada ya wakili kukutana na RCO na RPC, mpelelezi David akaitwa na baada ya kujadiliana humo ndani na "Mtandao wa Kijamii" ukitajwa mara kadhaa ikaamuriwa warudishwe tena Mahakamani, DPP akapigiwa simu atayarishe mashtaka ya wizi wa lita 40 za mafuta yenye thamani ya Shillingi 80,000 (elfu themanini) na kituo cha Polisi cha Wazo Hill wakaamuriwa wawarudishe tena watuhumiwa mahakamani wasomewe mashtaka.
Watuhumiwa waliporudishwa mahakamani, mmoja akaachiwa kabla ya kufikishwa kwa hakimu, (Huyu ni dereva Mzee wa Zaidi ya miaka 65) na alipoachiwa alibubujikwa na machozi huku akisema "hii dhulma italipwa na Mwenyeezi Mungu hapa hapa duniani, iwe Badr au yeyote yule, Mwenyeezi Mungu atanihukumia". Wengiine watatu wakafikishwa kwa hakimu na kushtakiwa kwa shtaka la wizi wa mafuta Lita 40. Wakaambiwa dhamana iko wazi na wakadhaminiwa kwa dhamana ya mdhamini mmoja mmoja kila mmoja na kwa thamani ya elfu 30 (za maandiko) kila mmoja.
Jamani, Mheshimiwa Rais Kikwete alipoona Polisi inaadhibu na kutesa watu kwa kuwabambikia kesi za ajabu ajabu na kupunguza msongamano magerezani, akaanzisha mfumo wa waendesha mashtaka (DPP) ambao hawahusiani na Polisi, cha kushangaza ni kwenye tukio kama hili na nna uhakika yapo mengine mengi tu, pale DPP anapoona watuhumiwa hawana mashtaka ya kujibu lakini Polisi wanapokuwa na kiburi na ushupavu wa kuwarudisha tena polisi watuhumiwa na kuwafungulia kesi za kuwabambikia na wakubwa wa Polisi kushinikiza yafunguliwe mashtaka haraka haraka mradi tu wajilinde wao na waoneshe kuwa hawakuwashikilia bure bure kwa siku 9.
Sitaki kuyasema mengi kwa kuwa hii kesi ipo mahakamani kwa sasa, nimejaribu kuelezea yaliyojiri kabla ya hii kesi kufikishwa mahakamani na yaliojiri kupelekea kurudishwa tena mahakamani na kuwachiwa amma kupewa dhamanana jinsi Jamii Forums ilivyosaidia.
Ni dhahiri kuna uonevu wa hali ya juu katika hili sakata na kuna shinikizo la kifedha, cha kushangaza zaidi ni pale ambapo hakuonekana mahakamani bwana Badr mmiliki wa GBP ambae ndio walalamikaji, wala mawakala wa GBP Nassoro (Nasa) na Musa ambao walikuwa wakionekana mara kwa mara huko kituo cha Polisi cha Wazo Hill wakiingia ofisini kwa OCD (licha ya huyu OCD kukataa katakata kuonana na ndugu, jamaa na marafiki wa watuhumiwa, lakini alivyofika Nassoro na Musa walikuwa wanaingia ofisini kwake kama wako nyumbani kwao!). Jee Mwakilishi wao mahakamani alikuwa Mpelelezi David? inashangaza sana!
Halima Mdee upo? haya yanatendeka jimboni kwako. Nna uhakika umeisoma hii habari lakini labda kwako kufunguwa matawi huko Boko ni bora zaidi kuliko kusimamia dhulma ya wana jimbo lako.
Wote waliochangia ile nyuzi (Mengine ya Upinzani yana Ukweli... Polisi wanatumiwa), walioniponda na walioniunga mkono napenda kuwajulisha kuwa mmechangia kwa njia moja amma nyingine kupaza sauti za wanyonge walioshikiliwa bila dhamana kinyume cha sheria. Naomba muendelee kutoa maoni yenu kistaarabu zaidi ili wanaoyasoma haya wasichoke kuyasoma, yana impact kubwa sana, tukubaliane kutokukubalina.
Kwa mara nyingine ahsante JF.
Latest Update:
Watuhumiwa 3 wamewachiwa leo kwa dhamana, mtuhumiwa mmoja hana mashtaka ya kujibu, kawachiwa huru.
Kesi imebadilishwa badala ya Millioni 80 imekuwa Elfu 80!.
OCD wa Wazo Hill kahamishwa kituo.
RPC Kinondoni na RCO wabishana kuhusu hili sakata!
Nimeongea kwa simu na mmoja kati ya ndugu wa watuhumiwa, anakuja kunielezea kwa kirefu jinsi hii nyuzi ilivyosaidia. Nikipata habari kamili ntakuja ifungulia nyuzi.
Katika hiyo update niliahidi kurudi na kufunguwa nyuzi kuelezea kwa kirefu jinsi "nyuzi" ile ilivyosaidia. Ukweli ni kwamba nyuzi ile isingekuwepo "Jamii Forums" isingepelekea kuwa na "impact" iliyodhamiriwa.
Siku ya pili (28-09-2012) ilibidi watuhumiwa wapelekwe mbio mbio mahakamani asubuhi na mapema, licha ya kuwa jalada lao lilishafikishwa kwa Polisi wapelelezi (mmoja wao anaitwa David) kutoka kwa (DPP) siku mbili kabla likielekeza kuwa watuhumiwa hawana mashtaka ya kujibu na wawachiwe. Cha kusikitisha ni kuwa huyu David amma alikuwa anafanya makusudi kabisa kuendelea kuwazuia watuhumiwa dhidi ya hitimisho la DPP, huyu David ana kila sababu ya kufanya makusudi kwani baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho cha mafuta wanasema toka hii kesi ilipoanza (inawezekana na kabla pia kwani wafanyakazi waliobaki hapo ni wapya) huyu David alikuwa akienda kumiminiwa petroli ya bure mara kwa mara pale pale kituo cha GBP kinachomilikiwa na Bwana Badr, amma huyu David alikuwa na shinikizo kutoka kwa OCD wa Wazo Hill (kahamishwa kituo juzi) ambae nae alikuwa na shinikizo kwa wakubwa zake kuwa asiwawachie, ukweli ni upi? sijui. Lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Walipofikishwa asubuhi hapo mahakamani, mwendesha mashtaka hakuwa na kesi ya kuwasomea wala kuwafungulia kwani ilishaelekezwa waachiwe. Mpelelezi David, badala ya kuwawachia, akawachukuwa tena na kuwarudisha rumande kituo cha Polisi Wazo Hill ili mradi tu, kwanini waachiwe. Hapo ndipo kikundi cha watu waliokwenda mahakamani kuwawekea dhamana hawa watuhumiwa walipopaza sauti zao na kusema leo "mpaka kieleweke" na hatukubali warudishwe Polisi. Mpelelezi David wakati huo anaambiwa maneno hayo alikuwa anatabasamu na kucheka kidharau, kuonesha kuwa ndio wanakwenda na hamna mtachoweza kufanya.
Naomba ieleweke kuwa siku hiyo mahakamani walikuwepo watu wengi waliojitolea kwenda kuwawekea dhamana hawa vijana kiasi cha kustaajabisha, vipi wezi wa Millioni 80 wawe na wadhamini wengi namna hiyo, wake kwa waume? Waliojitolea na kupeleka hati za nyumba zilizothaminiwa walikuwa hawapungui 6, watumishi wa idara za Serikali ambao ndiyo mara nyingi huwa wanatakiwa wa wadhamini watuhumiwa wenye kesi kubwa walikuwa hawapungui 20 kila mmoja na barua ya dhamana, licha ya wafanya biashara na wengineo wengi waliojitokeza kuwadhamini hawa vijana. Wengi wao, habari zilizopelekea wajitokeze kwa wingi ni hizi zilizorushwa Jamii Forums.
Baada ya watuhumiwa kurudishwa tena Polisi pasi na haki, akajitokeza Wakili na kujitolea kufatilia hili sakata kwa RCO hapo Oyster Bay Police, baada ya wakili kukutana na RCO na RPC, mpelelezi David akaitwa na baada ya kujadiliana humo ndani na "Mtandao wa Kijamii" ukitajwa mara kadhaa ikaamuriwa warudishwe tena Mahakamani, DPP akapigiwa simu atayarishe mashtaka ya wizi wa lita 40 za mafuta yenye thamani ya Shillingi 80,000 (elfu themanini) na kituo cha Polisi cha Wazo Hill wakaamuriwa wawarudishe tena watuhumiwa mahakamani wasomewe mashtaka.
Watuhumiwa waliporudishwa mahakamani, mmoja akaachiwa kabla ya kufikishwa kwa hakimu, (Huyu ni dereva Mzee wa Zaidi ya miaka 65) na alipoachiwa alibubujikwa na machozi huku akisema "hii dhulma italipwa na Mwenyeezi Mungu hapa hapa duniani, iwe Badr au yeyote yule, Mwenyeezi Mungu atanihukumia". Wengiine watatu wakafikishwa kwa hakimu na kushtakiwa kwa shtaka la wizi wa mafuta Lita 40. Wakaambiwa dhamana iko wazi na wakadhaminiwa kwa dhamana ya mdhamini mmoja mmoja kila mmoja na kwa thamani ya elfu 30 (za maandiko) kila mmoja.
Jamani, Mheshimiwa Rais Kikwete alipoona Polisi inaadhibu na kutesa watu kwa kuwabambikia kesi za ajabu ajabu na kupunguza msongamano magerezani, akaanzisha mfumo wa waendesha mashtaka (DPP) ambao hawahusiani na Polisi, cha kushangaza ni kwenye tukio kama hili na nna uhakika yapo mengine mengi tu, pale DPP anapoona watuhumiwa hawana mashtaka ya kujibu lakini Polisi wanapokuwa na kiburi na ushupavu wa kuwarudisha tena polisi watuhumiwa na kuwafungulia kesi za kuwabambikia na wakubwa wa Polisi kushinikiza yafunguliwe mashtaka haraka haraka mradi tu wajilinde wao na waoneshe kuwa hawakuwashikilia bure bure kwa siku 9.
Sitaki kuyasema mengi kwa kuwa hii kesi ipo mahakamani kwa sasa, nimejaribu kuelezea yaliyojiri kabla ya hii kesi kufikishwa mahakamani na yaliojiri kupelekea kurudishwa tena mahakamani na kuwachiwa amma kupewa dhamanana jinsi Jamii Forums ilivyosaidia.
Ni dhahiri kuna uonevu wa hali ya juu katika hili sakata na kuna shinikizo la kifedha, cha kushangaza zaidi ni pale ambapo hakuonekana mahakamani bwana Badr mmiliki wa GBP ambae ndio walalamikaji, wala mawakala wa GBP Nassoro (Nasa) na Musa ambao walikuwa wakionekana mara kwa mara huko kituo cha Polisi cha Wazo Hill wakiingia ofisini kwa OCD (licha ya huyu OCD kukataa katakata kuonana na ndugu, jamaa na marafiki wa watuhumiwa, lakini alivyofika Nassoro na Musa walikuwa wanaingia ofisini kwake kama wako nyumbani kwao!). Jee Mwakilishi wao mahakamani alikuwa Mpelelezi David? inashangaza sana!
Halima Mdee upo? haya yanatendeka jimboni kwako. Nna uhakika umeisoma hii habari lakini labda kwako kufunguwa matawi huko Boko ni bora zaidi kuliko kusimamia dhulma ya wana jimbo lako.
Wote waliochangia ile nyuzi (Mengine ya Upinzani yana Ukweli... Polisi wanatumiwa), walioniponda na walioniunga mkono napenda kuwajulisha kuwa mmechangia kwa njia moja amma nyingine kupaza sauti za wanyonge walioshikiliwa bila dhamana kinyume cha sheria. Naomba muendelee kutoa maoni yenu kistaarabu zaidi ili wanaoyasoma haya wasichoke kuyasoma, yana impact kubwa sana, tukubaliane kutokukubalina.
Kwa mara nyingine ahsante JF.