Source radio 5 arusha!
Anaongea kwa hasira sana akisema CCM siyo baba wala mama yake! Anadai chama kinatumia fedha za walipa kodi kuzunguka nchi nzima kumchafua.
Millya ambaye ni mfuasi mkuu wa Edward Lowassa, anaelezwa kutaka kupata nafasi ya kuwania ubunge Arusha mjini, lakini Chadema wamemkatalia, kama walivyomkatalia Lowassa, kwa maelezo kwamba bado si wasafi kubeba bendera ya chama chenye nia ya kupambana na ufisadi. Chadema wanawakaribisha wote kwa sharti la kuwa wanachama wa kawaida, na watapewa muda wa kujisafisha na kuwaomba radhi Watanzania.
Anaongea kwa hasira sana akisema CCM siyo baba wala mama yake! Anadai chama kinatumia fedha za walipa kodi kuzunguka nchi nzima kumchafua.
Millya ambaye ni mfuasi mkuu wa Edward Lowassa, anaelezwa kutaka kupata nafasi ya kuwania ubunge Arusha mjini, lakini Chadema wamemkatalia, kama walivyomkatalia Lowassa, kwa maelezo kwamba bado si wasafi kubeba bendera ya chama chenye nia ya kupambana na ufisadi. Chadema wanawakaribisha wote kwa sharti la kuwa wanachama wa kawaida, na watapewa muda wa kujisafisha na kuwaomba radhi Watanzania.
Mkiti wa CDM Freeman Mbowe amesema CDM kinamkaribisha Millya kwa mikono miwili kwani ni mwanasiasa safi na CDM hawana historia chafu inayomhusu James Millya.
Mbowe amesema watashirikiana kikamilifu na Millya na kama mwanachama watampatia majukumu ya kuharakisha ukombozi wa Taifa hili.
Mbowe amesema ni uamuzi wa kishujaa ambao kila mwanademokrasia wa kweli anapaswa kuufurahia.Amesema anamfahamu vizuri Millya ni mpambanaji na mpiganaji hasa.
Mbowe pia amesema anawakaribisha wale wanachama wote wa CCM wanaojijua ni wasafi waje CDM kushiriki ukombozi wa Taifa lao.
Source:TBC Habari