James Bond sinema 23 kwa miaka 50 dhidi ya Bongo movies sinema 1 kwa mwezi

Sinema za bongo zina mapungufu mengi, leo nitajadili matano tu. (1) UTAALAMU: Hatuna professional screen writers, Directors, Actors/Actresses, wapiga picha za sinema. (2) FEDHA: Bajeti za sinema za bongo ni ndogo sana, na hivyo huwezi kupanda mchicha ukavuna iliki au karafuu. (3) TAMAA/UBINAFSI/UPENDELEO: Mtu yule yule na ujinga wake ule ule na mapungufu yake yale yale ataigiza sinema A leo, kesho B halafu C. Matokeo anakuwa amedharaulika na amechujkas na sinema haiuziki. Na katika kipengele hiki yamo masuala ya rushwa za kila aina ili angalau upate nafasi ya kuigiza / kuonekana kwenye sinema za bongo ikiwemo ya ngono. (4) TAMTHILIA DUNI: Sinema za bongo hazina msingi mzuri wa tamthlia na hivyo zinapwaya, na hivyo mtazamaji anashindwa kujihusisha na matukio yalioyoko kwenye maigizo; inashangaza kuwaona wanangangania kuigiza mambo ya mapenzi, kutumia magari makubwa, kuwa katika majumba makubwa, kuongea wanachanganya broken english na kiswahili cha mjini. (5) UNYONYAJI: Producers wa hapa bongo wanawalalia sana waigizaji, ni wizi kwa kwenda mbele. Kwa ujumla, sinema za bongo zina safari ndefu kufikia kiwango ya kile kilichofikiwa na wenzetu wa Afrika Magharibi. Tuwaombee viongozi wa Idara ya Utamaduni wapate kufumbua macho na kuwasaidia hawa wanaojiita watayarishaji na waigizaji wa 'BongoWood'.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Asante mama mdogo kwa tathmini yako. Labda tujiulize je kuna bodi inayosimamia au inayo ratibu utoaji na uruswaji wa hizi movie Kama vile TBS inavyosimamia bidhaa za viwanda?
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
James Bond kwa takriban miaka 50 (1962 - 2011) ametoa sinema 23 ambazo ni wastani wa sinema 2 kwa mwaka kwa kuanza na Dr No ya 1962 hadi Quantum of Solace ya 2009. Katika kipindi hicho kuna madirector tofauti na Ma star tofauti ambao wamehusika katika hizo films.

Hawa watu ni matajiri wa dunia kwa hizo films chache walizocheza na familia zao zinaishi vizuri tu kwa movie hizo chache. Hapa Tanzania kila ukisoma kurasa za burudani za magazeti utaona matangazo ya wasanii wetu wakitangaza film mpya kila mwezi. Kwa harakaharaka wasanii kama akina JB, Kanumba, Ray au Richie wanapaswa kuwa ni mabilionaire kupita hata kiwango cha akina Sean Connery au akina Leonardo Di Caprio. Kinyume chake watu hawa wanaonekana bado wachovu ingawa wana kiasi cha kubadili mboga na kununua jeans na cream. Je wadau tatizo liko wapi?

Mkuu sahihisho........ni wastani wa sinema moja kila miaka miwili na ya mwisho siyo quantum of solace

Official James Bond films
  1. Dr. No (1962-Sean Connery)
  2. From Russia With Love (1963-Sean Connery)
  3. Goldfinger (1964-Sean Connery)
  4. Thunderball (1965-Sean Connery)
  5. You Only Live Twice (1967-Sean Connery)
  6. On Her Majesty's Secret Service (1969-George Lazenby)
  7. Diamonds Are Forever (1971-Sean Connery)
  8. Live and Let Die (1973-Roger Moore)
  9. The Man with the Golden Gun (1974-Roger Moore)
  10. The Spy Who Loved Me (1977-Roger Moore)
  11. Moonraker (1979-Roger Moore)
  12. For Your Eyes Only (1981-Roger Moore)
  13. Octopussy (1983-Roger Moore)
  14. A View to a Kill (1985-Roger Moore)
  15. The Living Daylights (1987-Timothy Dalton)
  16. Licence to Kill (1989-Timothy Dalton)
  17. GoldenEye (1995-Pierce Brosnan)
  18. Tomorrow Never Dies (1997-Pierce Brosnan)
  19. The World is Not Enough (1999-Pierce Brosnan)
  20. Die Another Day (2002-Pierce Brosnan)
  21. Casino Royale (2006-Daniel Craig)
  22. Quantum of Solace (2008-Daniel Craig)
  23. "Bond 23" (November 2012-Daniel Craig)
 
Mkuu Camaraderie, nikushukuru kwa kufanya maboresho na hiyo ndiyo faida ya jamvi kwa kuwa inapanua upeo, na nikuwa sina habari na hiyo movie mpya ambayo inaonekana itatoka 2012 ya "Bond 23".
 
Kwa Tanzania kinachohitajika ni uamuzi wa Serikali kuona hii tasnia kama chanzo cha mapato. Tuchukulie watu wazima wanaopenda filamu zetu ni 1,000,000 kati ya watu wazima 21,000,000(kwa mujibu wa NEC), sasa kati ya hawa 1,000,000, tuchukulie 100,000 wanao uwezo wa kutoa 10,000 kununua nakala halali, halisi yenye ubora ya filamu kila mwezi, hapa nazungumzia mzunguko wa 1,000,000,000 kwa wazalishaji wa filamu na kodi kwa serikali (VAT) ya 200,000,000. Lakini sidhani kama wizara ishawahi kufikiria hilo. Sidhani kama ni rahisi kutoa filamu ya ubora mzuri kama kuna piracy ya kutisha kama ilivyo hapa Tanzania, waigizaji ,waandaji hawataweza kujiendeleza, kujiwezesha kutoa filamu za ubora kwa kutegemea hali ya saa hivi ambapo sidhani kama wakina Kanumba, Ray et al wanaingiza zaidi ya 5,000,000 kwa mwezi kwa hizi muvi zao. Kama kungekuwa na utaratibu mzuri kama nilivyoainisha hapo juu nadhani waandaji wangeweza kuandaa filamu moja tu kwa mwaka yenye ubora na mapato mazuri.
 
napingana na wewe vitabu ndio vilikuwa a big hit ila sio lazima iapply to movies movie ikihit ujue kuna a big effort from the director production company producer pamoja na the cast james bond movies simefanya vizuri saana for the past years tokana na production company directors plus the cast ila ever since the new bond come in Daniel Craig kwenye Casino Royale imefanya vibaya mnoo if u ask why utakuta hapo vigezo nliotoa ingawa still kitabu kilifanya vizuri muv hiyo pamoja na Quantum Of Solace haikufanya poa soo hiyo point yako hapanaaa
Tofauti kubwa ya kwanza ni kuwa hizo series za James Bond zime base kwenye vitabu vya Ian Fleming na vilikuwa mashuhuri kama vitabu kabla ya kuwa movie.

Pili hivyo vitabu umashuhuri wake sio Uingereza tu, bali duniani kote na kusababisha movie zake pia kupendwa duniani kote.

Siwatetei kina Kanumba lakini kufananisha hivyo viwili ni sawa na kichunguu na mlima.
 
Back
Top Bottom