Jambazi sugu wa majeneza ashindwa kuhudhuria kwenye mazishi ya watu nchini Kenya

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Jambazi sugu wa majeneza.jpg


Aliyekuwa jambazi sugu na mwizi wa majeneza jijini Nairobi John Kibera ameshindwa kuhudhuria mazishi ya mtu yoyote .

Licha ya kutumikia kifungo chake baada ya kupatikana na hatia ya uhalifu wa kufukua na kuiba majeneza kabla ya kuyaauza,Kibera amesema sasa hata familia yake inaogopa kumuona kwenye mazishi.

John amesema kwa sasa yeye ameokoka na hafanyi tena uhalifu huo .

Amepeana kwa mayatima nyumba ya shilingi milioni 7 aliyonunua kwa pesa za kuuza majeneza .

Zama zake alikuwa mmoja kati ya majambazi sugu waliosakwa na polisi kote nchini.


Chanzo: CRI Kiswahili
 
Back
Top Bottom