Kunatabia imezuka katika hizo taasisi hapo juu tunapo tuma wake zetu kufuatilia masuala labda kulipia kodi au kuomba mkopo kutoka bank,inapotokea mke wako akapangiwa ofisa mikopo mwanaume au ofisa wa kodi mwanaume basi imekuwa ni kero ya ajabu kwa hawa watumishi kuwatongoza wake za watu!mfano mke wangu alikuwa anafuatilia TIN number yake mwenge TRA pamoja na kuwa ameshaipata TIN number jamaa bado anampigia simu za kumtaka pamoja na kumweleza kuwa ameolewa lkn jamaa hasikii,hivyo hivyo katika Bank moja hapo Makumbusho pamoja na kuwa mkopo ameshapata lakini yule ofisa mikopo bado anamsumbua kwa kumtaka kimapenzi, huyu yeye ananijua kwa sura na wakati wa kukagua vitu vya ndani alinikuta nyumbani na nikaweka saini katika zile form za uzamini kama mume,naongea haya kwa uchungu kwa sababu huyo wa bank jana kampigia simu anamuomba wakutane maana wkend hii free,Sasa nauliza wanaJf nifanye nini kukomesha hili? naomba kuwasilisha hoja