MESTOD
JF-Expert Member
- Nov 12, 2010
- 4,798
- 2,004
Imemkuta jamaa yangu juzi. Alimuona dada mmoja jana maeneo ya fire anasubiri usafiri wakati anamuacha mshokaji wa ofisini pale. Yule dada alimfata na kumuomba msaada kwa madai kuwa anashuka Manzese.
Kutokana na shida ya usafiri iliyokuwepo juzi na foleni jamaa kaingiwa na moyo wa huruma, akakubali. Walipofika Manzese yule dada akamwambia simama nashuka. Jamaa aliposimama dada kaanza kupiga kelele, 'nilipe hela yangu, nasema nilipe hela yangu sasa hivi! Haiwezekani unilale muda wote ule halafu usinipe hela yangu, nipe sasa hivi'.
Jamaa alishikwa nabutwaa akawa haamini anachosikia na kukiona. Na kama kawaida ya Dar, watu wakaanza kujaa kuangalia kulikoni na kulizingira gari. Mshikaji ikabdi atoe sh. 10,000 na 'kumlipa', na kuondoka kwa fedheha sana.
Jamani tuwe makini sana barabarani. Unaweza ona unatoa msaada kumbe unajiumiza.
Kutokana na shida ya usafiri iliyokuwepo juzi na foleni jamaa kaingiwa na moyo wa huruma, akakubali. Walipofika Manzese yule dada akamwambia simama nashuka. Jamaa aliposimama dada kaanza kupiga kelele, 'nilipe hela yangu, nasema nilipe hela yangu sasa hivi! Haiwezekani unilale muda wote ule halafu usinipe hela yangu, nipe sasa hivi'.
Jamaa alishikwa nabutwaa akawa haamini anachosikia na kukiona. Na kama kawaida ya Dar, watu wakaanza kujaa kuangalia kulikoni na kulizingira gari. Mshikaji ikabdi atoe sh. 10,000 na 'kumlipa', na kuondoka kwa fedheha sana.
Jamani tuwe makini sana barabarani. Unaweza ona unatoa msaada kumbe unajiumiza.