Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,398
- 319
1.Nawaomba amkeni,
Enyi mlio vitandani,
Amkeni wajameni,
Amkeni msione soni.
2.Msilale kama pono,
Tena bila ya maono,
Tushikamane mikono,
Ili kuonesha mfano.
3.Umefika muda tena,
Tulioungoja kwa sana,
Wa kuzikataa furana,
Kuwachagua firuna.
4.Wana sura za huruma,
Kwa ndani zinahujuma,
Kutufanya maamuma,
Na akili zimezama.
5.Tumia akili yako,
Wala usijipe mwiko,
Simama usikae kitako,
Kutumia haki yako.
6.Vijana jitokezeni,
Fisadi weka pembeni,
Taifa tuokoeni,
Toka mwao mikononi.
7.Vijana taifa la kesho,
Hivyo ni vichekesho,
Huwa haifiki kesho,
Tuachane na mipasho.
Enyi mlio vitandani,
Amkeni wajameni,
Amkeni msione soni.
2.Msilale kama pono,
Tena bila ya maono,
Tushikamane mikono,
Ili kuonesha mfano.
3.Umefika muda tena,
Tulioungoja kwa sana,
Wa kuzikataa furana,
Kuwachagua firuna.
4.Wana sura za huruma,
Kwa ndani zinahujuma,
Kutufanya maamuma,
Na akili zimezama.
5.Tumia akili yako,
Wala usijipe mwiko,
Simama usikae kitako,
Kutumia haki yako.
6.Vijana jitokezeni,
Fisadi weka pembeni,
Taifa tuokoeni,
Toka mwao mikononi.
7.Vijana taifa la kesho,
Hivyo ni vichekesho,
Huwa haifiki kesho,
Tuachane na mipasho.