white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,314
- 13,278
jana nimekwenda bank ya nmb-temeke,kwenda kuchukua pesa kwenye atm,nilitoa tsh.laki moja cha ajabu wakati nazihesabu nikagundua kuna sh.elfu thelathini(wekundu 3) ni bandia!nikatoka nikaingia ndani kumuona customer manager,nikamuonyesha hizo fedha,cha ajabu anasema haiwezekani kabisa!eti nimekuja nazo!ikabidi niachane nao,na nilipoulizia wa2 wanasema mbona,kwenye atm za nmb ni ki2 cha kawaida sana,hivyo nachelea kusema kwamba mjiadhari kwani huwezi kukwepa na kurudishiwa haiwezekani,ila mimi kuanzia sasa kama nachukua pesa nyingi nitalazimika kwenda kwa teller,japo huwa hawataki nitapambana,kwani cku unaweza kuta laki 2 zote fake c inakuwa balaa!na huu mchezo watakuwa wanaufanya wale wanaoongeza pesa kwenye hizi atm.na zile hela fake nilimrushia meneja.