The Finest
JF-Expert Member
- Jul 14, 2010
- 21,605
- 6,071
kila mtu ameumbwa na silka yake,mwangalie yeye kama yeye na si kabila lake[/QUOTE]
Siyo kuangalia tu, hata kufikiria kabila lake tayari kwangu ni dhambi kubwa. Labda kama katumiwa hiyo parcel na wazazi wake toka huko uheheni.
Mtu mmekutana mjini, tayari wote ni synthetic product halafu unaanza kuuliza kabila? Siwezi kuelewa hata kidogo!
Shikamoo Babu,
Baada ya salamu napenda kujua kama mzima wa afya mimi sijambo huku mjini wote wazima kabisa natumaini bibi yangu hajambo yule mbuzi bibi aliyenipa ameishaanza kutoa maziwa? Nikija kijijini nitakuja nimchukue nimlete huku mjini nipate kumfuga vizuri babu huku mjini kuna magari mengi sana sio kama kijijini halafu kuna umeme na video na kuna taa barabarani mji ni mzuri kweli babu nitakutumia nauli uje huku unitembelee.
Babu ile baiskeli yangu ilikuwa na matatizo ya spoko nakumbuka niliiacha kule kwenye migomba huku baiskeli ziko nyingi nitakutumia na wewe ya kwako yule mchumba wangu mtoto wa jirani yetu Shemdoe yupo? Msalimie sana babu.Babu naomba ukimaliza kusoma hii barua umpe na bibi naye asome nimeweka humo noti ya elfu kumi kwa ajili ya ugoro wako nahisi utakuwa umeisha.
Nikipata nauli nitakuja.
Mjukuu wako mpendwa
The Finest.