jamani msaidieni happy

hivi kuna wapenzi hapa duniani ambao wanatumia condom...kila siku nasikia watu wanapigana kavu kavu dah!! tutakufa wengi aisee...

wamepata habari za hiyo tiba ya mwanza ya herbal works, dawa inaitwa TANVIR CEX-R. Ndio maana wanaenda peku tu! LORD HAVE MERCY!
 
subiri kwanza ukapime tena baada ya miezi mitatu. Upo uwezekano mkubwa kuwa nawe ni muathirika, ila titre haijafika ya kusomeka...

mbona cku hizi wanasema kuna kipimo, kinaconfirm only after 3 weekes after being infected??? Hebu nijuzeni hapa inakuaje?
 
Story nzuri sana.....lakini bado unahitaji kusoma sana fasihi andishi ili uweze kutengeneza inayovutia zaidi.Usisahau pia kujifunza kwamba si kila mahali kwenye sentesi unatakiwa kuweka "comma" au "dot" na pia kumbuka herufi kubwa wakati unaanza sentensi nyingine. Usisahau wewe ni msomi wa chuo kikuu.

Asante kwa kupokea ushauri!
 
yesu wangu na maria.....
wewe mtoto wewe .... iyo ni alert tu mungu amekupa kwamba hayo mapenzi uliyoyaparamia kwa pupa ipo siku yatakutokea puani .... tena inabidi ukapime tena maana si ulishangonoka na alex bila condomu?
mimi nakushauri umrudie mungu .....
achana na zinaa na tamaa za dunia hii....
tulia kama mimi ...
soma kwa sasa ,mapenzi yapo nenda taratibu dunia hii....

Wasichana kama hawa ndio wanaofanya wanaume tusieleweke na daily wadada wawe wanaumizwa, how can you lv alex back? Nahisi ban itanikuta nikiendelea kuchangia hii thread acha nirudi kwenyr outlook niingize siku
 
Umechezea shilingi chooni....tamaa ndugu. Kaa kimya mpaka akili iwe sawa, halafu mtafute Alex ujue kama anamtu au siyo, kama nafasi ipo mwambie alikuwa college mate, hakuna kitu serious nikimaanisha ulikuwa unamzuga tu na wewe ulisikia kama ana demu mwingine ndio ukataka usitishe mahusiano bali kwasasa uko ready kuzungumza and rekindle the relationship.

best of luck.
 
usirudi kwa alex.huna mapenzi ya kweli kwake.dont play with his feelings.
 
pole sana dada Happy. katika maisha yako jitahidi kua mwaminifu katika mapenzi la sivyo you will end up with pains only,,,,,,,,,,,,,,,. usimrudie dogo tayari ulisha muumiza so, remain single............na hayo ndo yatakua mlipizi yako
 
Maskini Happy!

Achana na habari ya kumtafuta Alex now
Chamsing kaa uangalie afya yako kwanza, umesema mapenzi ya victa yalikuwa matamu, inamaana mlikuwa mna-DO!
Kitendo cha kupima na kukutwa wewe huna VVU kinaweza kukupa moyo but baada ya kupima hiyo jana, subiri miezi mitatu ukapime tena hapo ndo unaweza kuanza kushangilia, miezi mitatu mingine ikipita kapime tena hapo sasa ukikutwa u-HIV negative ndo ushangilie. Na kwa kipindi hiki chote cha matazamio please usi-DO kabisa au uki-DO tumia kodomu
 
Duh!Hongera kwa uzima wa afya,jikague ujue ni kitu gani kilikufanya uachane na na mpenzi wa kwanza!Usiniambie ni upendo!

hatakiwi kumkimbia victa ghafla namna hiyo. Anatakiwa amcontain kisaikologia kwa kumpa kampani mpaka pale atakapohisi amezoea kidogo hii stress aliyonayo. Kumuacha ghafla utamchanganya na kumfanya arudi kwenye tufe wengi. Haya mambo siyo rahisi,inahitaji moyo lakini we ulishafanya naye mapenzi hatakuwa mpya kwako. Please usimkimbie lakini usifanye naye mapenzi. Inatakiwa ukae ujadili naye maana kurudi ghafla kwa jamaa yako itamfanya ahisi utasambaza taarifa zake kwa watu wengine. Anaweza kukuua kabisa. Kuwa makini na uamuzi unaotaka kuuchukua.
 
Unaonja MOTO kwa ulimi? Acha ukuunguze.....!

if this is true inatakiwa tuachana na kuwalaumu wote wawili. Kinachotakiwa ni namna ya kukata hii chain isiendelee haraka. Mfano hapy akirudi kwa alex hatuko sure kama yuko salama kwani kuna vile vifaa vya mtasiwa hivyo utaendelea kusambaa. Pia akimuaacha vikta kuna vitu vingi,anaweza kuuawa na victa na ye kujiua,vikta ataanza kusambaza kwa hasira,hana uhakika kama alex yuko salama. Kinachotakiwa ni wao kuendelea kupeana psychological support ili victor asipatwe na severe post traumatic stress disorder. Kwani kitendo cha kujua tu unao unapatwa na stress,ukiongeza na kuachwa sababu hiyo na ule wasiwasi wa leaking of information ikifuatiwa na unyanyapaa hali inakuwa ngumu zaidi. Take responsibility ya kumfanya jamaa azoee situation(ni ngumu lakini kuna vitu vitapungua) huku mkiendelea kujadili mustakabali wenu. Vile unavyofikiri ungejisikia wewe ingekupata hali hiyo hata mwenzio atakuwa hivyo. Kuwa mvumilivu,achana na tamaa kwa muda huu,muombe Mungu akupe nguvu.
 
I salute Alex, ni mstaarabu. Mwache jamaa usije mliza mara ya pili.
Wewe hujui kupenda, Happy wewe ni opportunist.
Please mpe nafasi ampende mwingine.
 
shigongo at work!.. Story za kutunga bana..hivi ni mwanaume gani ataenda kupima pamoja na mwanamke wakati hawako hata ktk hatua za uchumba?...thidanganyiki
 
Wasichana wengi wanapovuka tabaka moja kwenda jingine mara nyingi hudharau wale waliowaacha nyuma au chini. Mathalani, akipata kazi na mpenzi wake akawa bado ni mtu wa mtaani, ni rahisi huyo wa mtaani kutoswa.
Hapa tumeona mfano hai wa Happy kumwacha Alex vile tu kafanikiwa kufika chuo kikuu na huko kakutana na Victor,so far kijana ambaye kielimu kamzidi Alex.
Dada Happy, inampasa asubiri baada ya muda fulani upite halafu apime tena mara mbili au zaidi ili kwa uhakika kabisa athibitishe kuwa yu mzima.
Pili, kwa heshima ya wanaume wote tafadhali Happy muache Alex aendelee na maisha yake maana awali si kwamba ulitupa tu jongoo, bali ulitupa pia na mti wake.
Mwenyewe kwa matamshi yako hapo juu umekiri kuwa "mwaka mmoja uliopita ulipofika chuoni ulitokea kumpenda kijana mmoja kwa jina Victor"...hivyo sidhani kama kweli Alex ni aina ya mwanume ambaye kwako unaona ndiye akufahaye pamoja na mambo yote mlofanya mkiwa A-Level.

"Majuto ni mjukuu"

hapo penye red....." inaelekea binadamu si walipaji wa fadhila kabisa, huyu happy kwanza kafika chuo kwa msuli wa Alex lakini kasahau kabisa na kuona hamfai" wakaka nawapeni pole sana. but na ninyi muwe macho msiwakaribishe tu hawa siyo wazuri kwenu watawaumiza tu.
 
if this is true inatakiwa tuachana na kuwalaumu wote wawili. Kinachotakiwa ni namna ya kukata hii chain isiendelee haraka. Mfano hapy akirudi kwa alex hatuko sure kama yuko salama kwani kuna vile vifaa vya mtasiwa hivyo utaendelea kusambaa. Pia akimuaacha vikta kuna vitu vingi,anaweza kuuawa na victa na ye kujiua,vikta ataanza kusambaza kwa hasira,hana uhakika kama alex yuko salama. Kinachotakiwa ni wao kuendelea kupeana psychological support ili victor asipatwe na severe post traumatic stress disorder. Kwani kitendo cha kujua tu unao unapatwa na stress,ukiongeza na kuachwa sababu hiyo na ule wasiwasi wa leaking of information ikifuatiwa na unyanyapaa hali inakuwa ngumu zaidi. Take responsibility ya kumfanya jamaa azoee situation(ni ngumu lakini kuna vitu vitapungua) huku mkiendelea kujadili mustakabali wenu. Vile unavyofikiri ungejisikia wewe ingekupata hali hiyo hata mwenzio atakuwa hivyo. Kuwa mvumilivu,achana na tamaa kwa muda huu,muombe mungu akupe nguvu.

asante kwa ushauri mzuri
 
Alex anaweza kukubali ila mapenzi na uaminifu kwako tena utakuwa umepungua na atakaa na wewe akiamini iko siku tena unaweza kumkimbia.....

So na yeye anaweza pata Back up ikimvutia utasikia anakwambia Happy mie na wewe it is over nimepata mwingine wa kufanana na mie
Pole....
Endelea kupima kabla hujaenda kumwambukiza Alex
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom