Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,702
. . . . Ilikua ni leo wakati nimerudi mapema baada ya kwenda kijiweni na kukuta leo hakuna kibarua cha kuponda kokoto,tajiri alikua hajapata tenda.Nikaja mpaka home na kujilaza kwa machungu nikijua siku ya leo itakua ngumu sana,si hakuna hela ya kula!Wakati nipo ndani wapangaji wenzangu walijua sipo,pembeni ya chumba ninachoishi nimepakana na jamaa mmoja ambae ameoa,muda ule jamaa hakuwepo,alikuwepo mkewe.Ndipo nikiwa ndani nilisikia yule mke wa jamaa aliepanga chumba kinachopakana na changu akipata mgeni.Mgeni yule alikua ni dada ambae baada ya kumsikia sauti nikamfahamu,nyumba tuliyopanga haina siling bodi hivyo nilisikia yote waliyoongea. . . . . . . . .Yule dada mgeni baada ya salam na story kidogo akamwambia mwenyeji wake,"Mwenzangu ndoa yangu inanishinda" mwenyeji akamwuliza,"kulikoni?"dada mgeni akajibu "Si unajua ndoa yangu na mume wangu mlokole inatimiza miezi sita kesho,mh,yaani mimi na mume wangu kila tukifanya mapenzi,akipiga bao moja tu hataki kurudia,nikimwambia sijatosheka ananiambia,mke wangu maandiko yanasema tuwe na kiasi,tukizidisha ni ulafi.Na imekua ndo kauli yake kila siku,mi nimechoka"!Yule mwenyeji alitoa mguno wa mshangao kisha akampa pole,walizungumza mengi ila mwisho yule mke wa mlokole alisema "nampa miezi 6 asipojirekebisha ataisoma namba"kisha nikasikia mlango unafunguliwa kukawa kimya. . . . , .Nikajiuliza;hivi na ushamba wangu kumbe box manyoya nayo inaliwa kwa kiasieeeee au nyie mnasemaje waungwana?