Jamani mbona wahamihaji haramu ni wengi Sana Tz??

Milango iko wazi nzige kenge,vyura,mende wote wataingia,baada ya muda mfupi tutalia kilio cha kusaga meno hamna mfuumo kabisa,wakuzuia tatizo hilo watu walioshika nafasi za kutekeleza taratibu za uhamiaji ndio wa kwanza kuzivunja,halafu watu wa wizara ya kazi hawakagui kabisa majedwali ya wafanyakazi katika makampuni mbalimbali ni nani
 
Wewe Wilfred Rwakatare nani kauuliza PR ya uliko? Njaa yako itakumaliza mwaka huu.
Usilolijua kwako ni kama usiku wa giza. Utajaribu kutaka kunifahamu usiweze na utabaki ukibashiri lakini hutoweza kunijua mimi ni nani. Baki ulivyo na mimi sina haja ya kukujua nungunungu yawezekana una id kibao hapa na hasa yaweekana wewe ni yule yule kanda 2. Pole sana.
 
Wewe inakuhusu nini kujua mambo yangu? Sikujui hunijui hata nikikwambia ninayo na labda nimeshachukua na uraia inakusaidia nini wewe!? Duh! watu wengine jamani! :confused:
Mbona unajibu kwa jaziba mkuu? Hii sio kawaida yako. Au kuna mtu kaiba password yako nini?
Mimi nimeuliza kwa nia nzuri kufuatana na jinsi ulivyojibu post yangu. Nilitaka twende kwa kuelewana ili uitetee vizuri post yako. Basi bwana yaishe!
 
...babu nilitegemea kwa sababu unaishi nchi za watu na kuelewa misekeseke ya wahamiaji wanayo go through labda ungekuwa more lenient na wahamiaji no matter where bro,ni rahisi kuongea tuu lakini nina uhakika path to legal resident ni ngumu sana na haiko clear kwa wahamiaji kwa nchi kama TZ na ukiongeza na rushwa basi ni next to imposible,kweli nawahurumia sana wahamiaji hawa,jamani hebu tuwe more compassionate na hawa watu maana wengi wanakuwa wamekimbia matatizo huko kwao au kutafuta unafuu wa maisha tuu,wengi wao sio criminal .

Mkuu Koba, pamoja na hayo ni lazima wafuate sheria na taratibu za nchi kuhusu uhamiaji na kama hawakufanikiwa katika kufuata taratibu hizo basi warudi kwao vinginevyo katika miaka 10 au 15 ijayo hili la wahamiaji litakuwa ni tatizo kubwa sana. Wachina wako more than 1 billion, Wahindi wako more than 1 billion wakiachiwa waingie kienyeji bila kufuata sheria basi miaka michache ijayo tunaweza kujikuta hawa watu population yao nchini ni kubwa sana kuliko ya Wazawa na hapo nchi yetu itakuwa imetekwa nyara na wahamiaji, ni lazima tuwe makini na wakali sana katika hili.
 
Mbona unajibu kwa jaziba mkuu? Hii sio kawaida yako. Au kuna mtu kaiba password yako nini?
Mimi nimeuliza kwa nia nzuri kufuatana na jinsi ulivyojibu post yangu. Nilitaka twende kwa kuelewana ili uitetee vizuri post yako. Basi bwana yaishe!

Mkuu katika watu ambao nawaheshimu sana hapa jamvini wewe ni mmojawapo, hivyo swali lako la "nguoni" kama naweza kuliita hivyo lilinishangaza. Basi yaishe mkuu.

Bado nakumbuka ile thread yako ya picha za Kigoma ambayo iliibua mjadala mzito na mrefu sana, kama nafasi ikikuruhusu basi uwe unachukua picha za sehemu mbali mbali na kuziweka hapa labda zinaweza pia kuibua mjadala mwingine mzito kama ule wa Kigoma mkoa ambao pamoja na kuwa na rutuba kubwa sana lakini bado uko nyuma sana kimaendeleo.
 
Did somebody say that from July 1 EAC subjects will be allowed to roam. acquire land and work freely within EAC ?

Is this the deal or am I just hallucinating?

Mkuu wewe subiri tu alafu anza kule tende na pop corn mambo Tanzania tambarare. Gonga hapa
 
Back
Top Bottom