Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Habari za watoto wa kike kuuawa kikatili huko Mbeya zinatisha. Kuna jamaa alinambia hiyo hadithi juzi lakini sikuamini. Alisema watoto 7 wa kike walikuwa tayari wameuawa baada ya kubakwa. Na Kwamba wauaji walikuwa wanachukua moyo wa kila mtoto baada ya kumuua, tena kupitia kwenye sehemu zake za siri. Sikuamini hadi jana niliposikia kwenye TBC1. Huko Mbeya nadhani kuna tatizo kubwa zaidi ya tunavyoelewa. Vinginevyo unaweza vipi kuamini hadithi kama hiyo?