kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Wadau nimepata hii habari kutoka kwa blog ya Michuzi. Hivi huyu Lyatonga ameugua ugonjwa gani au ni kweli kuwa alipandikiza ili aue upinzani?
Mwenyekiti wa TLP Mh. Augustine Lyatonga Mrema akishangiliwa na wana CCM kwenye mkutano mkuu wa Chama hicho Kizota, Dodoma
Mwenyekiti wa TLP Mh. Augustine Lyatonga Mrema akishangiliwa na wana CCM kwenye mkutano mkuu wa Chama hicho Kizota, Dodoma
Uzuri wa ndege manyoyaaaaa
Uzuri wa CCM seraaaaa
Huu ni ujumbe wa Khadija Kopa akimfagilia Mheshimiwa Lyatonga Mrema, mwenyekiti wa Chama Cha TLP alipofungua moyo wake akimmwagia sifa kede kede Mwenyekiti wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete.
Hapa sasa hivi Lyatonga Mrema anatoa salamu rasmi kutoka chama cha TLP na kuwasema wale wanaosingizia katumwa na wana CCM wakome.
Anashangiliwa na wana CCM kwa nyimbo na vigelegele, anasema kwamba CCM haikamatiki. CCM Chama Kubwa, amesalimu amri. Kwani mwaka 1995 alishindwa, mwaka 2000 aligaragazwa na Mh. Mkapa, na mwaka 2005 ndio kabisaa Kikwete akammaliza. Hivyo CCM ni chama imara, hakishikiki. "Kweli CCM inagaragaza upinzani".
Mheshimiwa Mrema aliongeza, "Kila mwaka wa uchaguzi inakula kwangu, sasa nimechoka" anasema Mrema kwa hamasa huku akiendelea kusifia CCM na uongozi wake.
Kwa maneno yake amesema, hana sababu ya kuacha kumsifia Rais Kikwete kwani ndiye Rais pekee anayemjua. Amefanya kazi kubwa sana katika kipindi cha miaka mitano hususan katika harakati za kupambana na ufisadi na mafisadi nchini.
Amekiri ya kuwa katika marais wengi waliopita , Kikwete ni mthubutu na mtekelezaji. Anaumia roho sana kusikia kuna watu wanaombeza ati hajafanya lolote hivyo wamtose.
Mrema amewasuta wote wanaobeza maendeleo ya serikali ya Rais Kikwete na amewaomba wana CCM waendelee kumsaidia ili afanye vizuri zaidi. Hapo Mrema alishangiliwa sana kwa nyimbo za CCM na kusindikizwa na bendi ya TOT.
Mrema amemaliza kwa kusema ya kwamba anafuata wosia wa baba wa Taifa na hivyo atagombea ubunge Vunjo kupitia chama chake cha TLP.
Mwenyekiti wa CCM amemshukuru kwa kuwa mkweli lakini amemuhakikishia ya kwamba hata wana CCM watakwenda huko VUNJO na watakutana tena.
Mambo moto moto hapa Kizota, salamu zinaendelea. Picha zinakuja
Uzuri wa CCM seraaaaa
Huu ni ujumbe wa Khadija Kopa akimfagilia Mheshimiwa Lyatonga Mrema, mwenyekiti wa Chama Cha TLP alipofungua moyo wake akimmwagia sifa kede kede Mwenyekiti wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete.
Hapa sasa hivi Lyatonga Mrema anatoa salamu rasmi kutoka chama cha TLP na kuwasema wale wanaosingizia katumwa na wana CCM wakome.
Anashangiliwa na wana CCM kwa nyimbo na vigelegele, anasema kwamba CCM haikamatiki. CCM Chama Kubwa, amesalimu amri. Kwani mwaka 1995 alishindwa, mwaka 2000 aligaragazwa na Mh. Mkapa, na mwaka 2005 ndio kabisaa Kikwete akammaliza. Hivyo CCM ni chama imara, hakishikiki. "Kweli CCM inagaragaza upinzani".
Mheshimiwa Mrema aliongeza, "Kila mwaka wa uchaguzi inakula kwangu, sasa nimechoka" anasema Mrema kwa hamasa huku akiendelea kusifia CCM na uongozi wake.
Kwa maneno yake amesema, hana sababu ya kuacha kumsifia Rais Kikwete kwani ndiye Rais pekee anayemjua. Amefanya kazi kubwa sana katika kipindi cha miaka mitano hususan katika harakati za kupambana na ufisadi na mafisadi nchini.
Amekiri ya kuwa katika marais wengi waliopita , Kikwete ni mthubutu na mtekelezaji. Anaumia roho sana kusikia kuna watu wanaombeza ati hajafanya lolote hivyo wamtose.
Mrema amewasuta wote wanaobeza maendeleo ya serikali ya Rais Kikwete na amewaomba wana CCM waendelee kumsaidia ili afanye vizuri zaidi. Hapo Mrema alishangiliwa sana kwa nyimbo za CCM na kusindikizwa na bendi ya TOT.
Mrema amemaliza kwa kusema ya kwamba anafuata wosia wa baba wa Taifa na hivyo atagombea ubunge Vunjo kupitia chama chake cha TLP.
Mwenyekiti wa CCM amemshukuru kwa kuwa mkweli lakini amemuhakikishia ya kwamba hata wana CCM watakwenda huko VUNJO na watakutana tena.
Mambo moto moto hapa Kizota, salamu zinaendelea. Picha zinakuja