Nimekaa kwenye Luninga kwa takribani saa nzima nikiangalia kipindi cha nyimbo bora 2010 kinachorushwa na Star TV, cha ajabu nyimbo zote ninazoziona zinazungumzia mapenzi tu mwanzo mwisho, ina maana wabongo hatuna uwezo wa kuimba nje ya mapenzi ?
Ukiimba umasikini sio wote wana guswa na umasikini, ukimba ujamaa sio wote wana guswa na ujamaa, ukiimba ucha Mungu sio wote wana guswa na ucha Mungu, ukiimba maadaili sio wote wana giswa na maadili ,ukiimba kufunza nakujenga jamaii sio wote ana guswa na hayo, lakini ukiimba mapenzi karibu kila mtu ana guswa na mapenzi ndio mana siku zote mapenzi yatakubalika ,karibu kila mtu anakutana nayo! na nadhani ni watu wachache wasio guswa namapenzi labda unaweza kua ni wewe peke yako, sasa kwanini msanii ambaye anataka kuuza kazi yake akuhangaikiwe wewe peke yako kukuridhisha wakati ana hitaji kujikumu na maisha kwa kuuza kazi yake kwawengi wanao isikiliza? , maana ina wezekana labda wewe hata kazi hununui au ni mara moja moja , je ni kuulize mara ya mwisho umenunua kazi za wasanii yeyote iwe mapenzi au Ujamaa lini ilikua?
Mtoto wa Kishua umejitahidi kujitetea lakini unataka kuniambia wasanii kama Rose Mhando, Mr, Ebo, ebo,wakina camirion,na wengine wengi ambao hajikiti sana kwenye nyimbo za mapenzi hawatoki? Mi naona ni kukosa ubunifu tu, na hii ni kwa wanaojiita wanamziki wa bongo ambao mziki wao hadumu hata miezi miwili unapotea kabisa.
Nimekaa kwenye Luninga kwa takribani saa nzima nikiangalia kipindi cha nyimbo bora 2010 kinachorushwa na Star TV, cha ajabu nyimbo zote ninazoziona zinazungumzia mapenzi tu mwanzo mwisho, ina maana wabongo hatuna uwezo wa kuimba nje ya mapenzi ?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.