Jamani huyu waziri wa mambo ya ndani si ajiuzuru?

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Majambazi yafanya kufuru Dar
Na Moshi Lusonzo
24th January 2010

Wimbi la majambazi linazidi kutikisa nchini, ambapo jijini Dar es Salaam watu wawili wameuawa kwa risasi na wengine wamejeruhiwa vibaya baada ya kundi la majambazi kuvamia mitaa miwili na kuiteka kwa muda wa saa 1.30.
Tukio hilo limetokea juzi eneo la Kimara Temboni, ambapo majambazi hayo yalianza operesheni hiyo ya kupora mali kuanzia majira ya saa 1:30 hadi saa 3:50 usiku.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Esaya Kalinga, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini hakuwa tayari kuzungumzia zaidi kwa kueleza yupo eneo la tukio.
Katika matukio hayo, majambazi hayo yaliyokuwa yamesheheni kila aina ya silaha ikiwa pamoja na bunduki za kivita, bastola, mapanga na mashoka, yalisababisha vifo vya watu wawili baada ya kuwapiga risasi pamoja na kuwajeruhi watu wengi kwa kuwakata mapanga na shoka.
Hata hivyo, kati ya watu waliokufa mmoja ameweza kutambuliwa kwa jina la Godfrey Chandeu mkazi wa Kimara B.
Waliojeruhiwa wametajwa kuwa ni Editha Peter (36) mumewe Peter Temarilwa (41) na mfanyakazi wao Sospeter Peter (2, Renatha Malya (33), mkazi wa Kimara Temboni pamoja na Mhasibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Gelvas Macha (41) mkazi wa Kimara Temboni.
Majeruhi wote wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa ya Muhimbili (MOI).
Wakisimulia tukio hilo, mmoja wa watu walioshuhudia tukio hilo, Salum Bakari, alisema kundi la majambazi idadi yake haijafahamika, walivamia eneo la Kimara Temboni majira ya saa 1:15 usiku, ambapo watu wawili wenye silaha walisimama mwanzo na mwisho wa mtaa huo na kuanza kuwaamuru watu wote wanaofika mtaa huo kulala chini na kisha kutoa vitu vyote walivyokuwa navyo.
Mmoja wa watu hao, Salum Bakari alisema katika tukio hilo watu wengi walijikuta wakiwa wametekwa na kukusanywa pamoja na kuanza kupigwa kwa kutumia mapanga na mashoka huku wakiwashurutisha kuonyesha kila kitu walichokuwa nacho.
"Ilikuwa ni hali ya kutisha, watu wengi walijeruhiwa kwa kipigo na mmoja alikufa baada ya kupigwa risasi kutokana na kutokea mabishano wakati walipomuamuru kulala chini," alisema Bakari.
Hata hivyo, Renatha Malya ambaye ni mmoja wa waliojeruhiwa alisema mara alipofika eneo hilo, alishtukia mtu akimfuata kwa nyuma na kumwambia kulala chini na alipohoji kwa nini alale chini, alishtukia akipigwa kitu kichwani na papo hapo alipoteza fahamu.
Baada ya kuhakikisha wamewateka watu wengi walianza kuwapekua kila mmoja na kuchukua kila kitu ikiwemo pochi, mikoba, simu na pesa walizokuwa nazo na kuondoka eneo hilo.
Operesheni hiyo haikushia hapo, watu hao walikwenda katika mtaa wa jirani wa Kimara B, huko waliwapiga risasi watu pamoja na kufanya uporaji wa mali kwa watu mbalimbali.
Majeruhi mwingine anayeishi mtaa huo, Edither Peter, alisema watu hao walimvamia wakati akiingia ndani ya nyumba yake, ambapo katika tukio hilo walijeruhiwa kwa kupigwa shoka kichwani yeye,mume wake na mfanyakazi wake. Pia majambazi hayo yalimfungia ****** mama mkwe wake ambaye alikuwa amelala sebuleni.
Alisema watu hao walichukua pesa taslimu shilingi milioni 1.8, simu nne, mkoba mmoja na kompyuta yake ya mkononi.
Aidha, wakati wakiondoka eneo hilo walimpiga risasi jirani yake aliyekuwa akipita eneo hilo na alifariki papo hapo.
Afisa Uhusiano wa MOI, Almas Jumaa alisema majeruhi wote waliolazwa hapo wanaendelea kupatiwa matibabu, lakini hali zao bado mbaya kutokana na majeraha waliyokuwa nayo.
CHANZO:NIPASHE JUMAPILI


My take:
Ufike wakati sasa viongozi wajifunze kuwajibika kutokana na uzembe wao. Katika hali ya kawaida, baada tu ya lile la Ukerewe, ilikuwa IGP na waziri wa mambo ya ndani waachie ngazi.
Halafu kingine, hivi idara ya usalama wa taifa nchini ilifutwa? Kama ipo inafanya kazi gani? Si isaidie kulinda usalama wa raia? Au usalama wa taifa manake nini kama watu wanauawa kila kukicha?
Shida na hawa majambazi wanatuonea sisi raia masikini, wanatuua kwa ajili ya visimu tu, si wavamie huko majumbani kwa mawaziri?
However, gazeti la juzi lilisema polisi ni member wa ujambazi, sasa wa kutulinda nani? Wadau mnasemaje kuhusu mwelekeo wa nchi?
Kuna tetesi kwamba chama xx kinakusanya hela ya uchaguzi, kuna ukweli kuhusu hilo?
 
Inatisha sana hii!

Hata kama hawa jamaa wakijiuzulu, usipobuniwa utaratibu wa kisasa wa kulinda mitaa yetu bado shida itakuwa palepale!

Hakuna hatua serious zinazochukuliwa maana Kimara ni uswahilini, na hao waliofanyiziwa ni watu wadogo.

Sijui kama uko sahihi sana, pale juu unasema kuanzia saa1.30 hadi saa3.50(ambapo tofauti ni masaa 2.20), hv inawezekana tukio lidumu kwa muda wote huo bila kuwa intercepted na polisi, bila kujali umbali?

Kama ni kweli, basi "Bwana asipoulinda mji, waulindao wanakesha bure"!..huh!
 
Kujiuzulu kwa maana ya kuonyesha uwajibikaji, sio mila wala desturi ya viongozi wa kitanzania. Labda tujaribu kuhoji kwa kujiuliza, watumia silaha hizi kali kali tena za kivita wamepata wapi uzoefu? Kulikuwa na fununu hapa nyuma kwamba vijana wanaofundishwa mafunzo ya kijeshi JKT wanatuhumiwa kwa wingi kujihusisha na ujambazi. Ni kweli kama mtu unampa elimu fulani ni lazima apata mahali pa kui-apply. Sasa hawa wahitimu wa kijeshi ambao hawaajiriwi wanajitafutia ajira katika njia zisizofaa. Nyuma watu walikuwa wanajiunga na kambi hizi za kijeshi wakitokea shuleni na wanapotoka pale wanaendelea na masomo vuoni na baadae wanaishia kwenye ajira. Jambo hilo lilikuwa halitoi nafasi ya kuwawezesha kuyatumia mafunzo ya kijeshi kijinai, tofauti na siku hizi vijana wengi wanajiunga na JKT kutokea vijiweni na wanapohitimu hurudi katika vijiweni vile vile walivyotokea. Kwa hali hiyo tutegemee nini zaidi ya kuwaona vijana wakiuonyesha uzoefu wao wa kijeshi mitaani?. Halafu inaingia akilini kweli majambazi yanauteka mtaa kwa zaidi ya saa moja na nusu mjini police bado wawe hawajafika kwenye tukio? Hapa raia tujihesabu tu kwamba hatuna ulinzi wa raia na mali zao, ila tuna ulinzi wa viongozi na madaraka yao.
 
JK alingiia madarakani nchi ikiwa na matukio kama hayo na sasa anamaliza na matukio hayohayo, pana siri gani hapo?
 
Inatisha sana hii!

Hata kama hawa jamaa wakijiuzulu, usipobuniwa utaratibu wa kisasa wa kulinda mitaa yetu bado shida itakuwa palepale!

Hakuna hatua serious zinazochukuliwa maana Kimara ni uswahilini, na hao waliofanyiziwa ni watu wadogo.

Sijui kama uko sahihi sana, pale juu unasema kuanzia saa1.30 hadi saa3.50(ambapo tofauti ni masaa 2.20), hv inawezekana tukio lidumu kwa muda wote huo bila kuwa intercepted na polisi, bila kujali umbali?

Kama ni kweli, basi "Bwana asipoulinda mji, waulindao wanakesha bure"!..huh!

Hali ni mbaya hii ni siku ya pili haya yanatokea, Juzi same situation happened at Chanika, na nilisema jana kuwa maana ya uamiri jeshi wa nchi kwa Raisi wetu inapotea, kwa sababu wanaofanya hivyo ni majeshi. To me it is like , nchi imepinduliwa muheshimiwa bila kujua. Kwani saizi hamna amani Tanzania, itafikia wakati raia masikini nao wataanza kuwavamia familia za maaskari ambao wengine ni waaminifu, na uzuri tunakaa nao mitaani hapo ndo vita za wenyewe kwa wenyewe zitaanza. Upuuzi mtupu, yani kwa kweli saizi TZ ifutwe kwenye nchi zenye stable political. Kikwete wamekusaliti na hawakutaki, kua jasiri aidha ujiuzulu kwa dhuluma wanazokufanyia au deal nao , mbaya zaidi ni unaokula nao na kucheka nao ndo wanaokufanyia huu ubaradhuli. Mungu ibariki Tanzania
 
Chama gani hicho?

Wee Kibunango mbona harakaharaka kuuliza chama? Unajishuku? Just think, kinaweza kuwa ni kipi hicho, kinachoweza kuendesha ujambazi super namna hii? mimi nimesikia watu wanasema, hata mimi sikijui, pengine humu tunaweza kukigundua.
 
JK alingiia madarakani nchi ikiwa na matukio kama hayo na sasa anamaliza na matukio hayohayo, pana siri gani hapo?

Hapo ndipo panapozusha utata, kama kweli ni ujambazi wa kawaida au una agenda ya siri nyuma yake?
 
Hali ni mbaya hii ni siku ya pili haya yanatokea, Juzi same situation happened at Chanika, na nilisema jana kuwa maana ya uamiri jeshi wa nchi kwa Raisi wetu inapotea, kwa sababu wanaofanya hivyo ni majeshi. To me it is like , nchi imepinduliwa muheshimiwa bila kujua. Kwani saizi hamna amani Tanzania, itafikia wakati raia masikini nao wataanza kuwavamia familia za maaskari ambao wengine ni waaminifu, na uzuri tunakaa nao mitaani hapo ndo vita za wenyewe kwa wenyewe zitaanza. Upuuzi mtupu, yani kwa kweli saizi TZ ifutwe kwenye nchi zenye stable political. Kikwete wamekusaliti na hawakutaki, kua jasiri aidha ujiuzulu kwa dhuluma wanazokufanyia au deal nao , mbaya zaidi ni unaokula nao na kucheka nao ndo wanaokufanyia huu ubaradhuli. Mungu ibariki Tanzania

Na huu ndo wasiwasi wangu, kwamba tunakoelekea ni kubaya. Tunaweza kuingia vitani siku si nyingi. wenzetu wa Ukerewe wameshajaribisha vita sasa sijui huko kwingine itakuwaje?
Na taabu inayokuja ni kwamba ndugu zetu wengi wakishakufa, tutatafuta namna ya kulipa kisasi.
 
Na huu ndo wasiwasi wangu, kwamba tunakoelekea ni kubaya. Tunaweza kuingia vitani siku si nyingi. wenzetu wa Ukerewe wameshajaribisha vita sasa sijui huko kwingine itakuwaje?
Na taabu inayokuja ni kwamba ndugu zetu wengi wakishakufa, tutatafuta namna ya kulipa kisasi.

Hii ni mbaya sana. kwani machafuko yakitokea TZ yatakua mabaya kuliko nchi yeyote ya Afrika ambapo machafuko yalikwishawai tokea. Wasiwasi wangu na huu msuguano ndani ya chama tawala, ukijaribu connect matukio ya ujambazi ya sasa yanalenga raia masikini, indicating that si kwamba hao jamaa wanataka pesa, kwani kuwavamia wauza nyanya na kauzu kwa silaha kalikali haiwalipi hao majambazi, hizo ni cheche za machafuko Mh. Raisi Amka kabla hawaota pembe hao mafisadi.

Kwa sababu gani wasiende kuwavamia mawaziri au mafisadi wenzao wenye pesa wanakuja kutuvamia sie ambao hatuna pesa? issue naiona hapo ni kuvuruga amani ya nchi na kunakundi pengine limeshajipanga kufanya hivyo kwa matamanio ya nafsi zao, lakini wajue wataua raia na wao hawatastarehe kama wanavyo dhani kwani wakiua raia, raia nao wakiwagundua watawaua ndugu zao na kama wanatumiwa baada ya deal kwisha wamafia watawaua, kwani hukumu ya msaliti ni kuuwawa.
 
karibu 7% ya polisi ni majambazi sasa hapo usitegemee ujambazi kukoma

mi nadani ni asilimia 70% ya mapolisi ni majambazi.wengine hawaendi physically kwemnye ujambazi lakini wanashiriki sana ujambazi
 
Kwa mwendo huu hata ile dhana ya polisi jamii haiwezi kufanikiwa kamwe, ushiriki wa polisi katika matukio ya kihalifu unaleta picha mbaya sana kwa raia, sidhani kama katika hali ya msuguano kati ya polisi na raia ushirikiano wa kukabiliana na uhalifu unaweza kuwepo, nadhani raia tumeachwa kama yatima sasa, viongozi wetu wanajua uozo uliopo ndani ya jeshi la polisi lakini hakuna anayechukua hatua..ni jana tu nimesoma kwenye gazeti la mwananchi eti polisi wamekwenda kumuiba mmoja wa majeruhi wa tukio la ukerewe na kumpa kichapo kikali sana kisa eti ametoa siri kuwa polisi nao walihusika kwenye sakata lile..,sasa jamani tutafika kweli..Mungu ibariki Tanzania na watu wake wote wenye mapenzi mema.
 
Back
Top Bottom