Jamani huyu binti yangu ataniua kwa presha....

lol! umenifurahisha mpendwa. wanawake smart namna hii, akina nyamayao wa kesho huwa hata ku-date mfumo dume hawawezi.inaishia date ya kwanza,lol! amkazanie tu kusoma ili akutane na civilised mwenzie!
Na kweli mwali ila tu nafikiri waangalie namna ya kumkuza kwenye maadili mmema. Kwa jinsi nilivyomsoma naona kama kuna kipunje cha kiburi!! Kama anaambiwa aandae meza, yeye anatandua meza kwa madai ya kuwa mamake kakosea hakumwambia aandae chakula kwa nini atandue na kukaa kuwaangalia kusubiri wamuulize kwa nini ametandua?? Kwa nini akiambiwa aandae meza; asimkosoe tu mama yake kuwa......sio kuandaa meza mama, ni kuandaa chakula .............huku akifanya kile alichokuwa anajua mama yake anakimaanisha?!

Na wasiporeduce hii speed (hasa kwenye kubishana na wazazi wake kwenye vitu vya kmsingi, iko siku atawaumbua mbele ya wageni). Hakawii kuropoka wewe baba umezoea kuja umelewa hadi unakokotwa .....imtoke mbele ya wageni. Ndio anahoji na kukemea tabia mbaya juu ya mzazi wake mlevi lakini sehemu na namna atakavyokemea lawama zote zitakujamrudia mamake kuwa kamdekeza, kamlea vibaya.

Hapana wampunguze speed kwa mambo yasiyo na maana la sivyo wanalea maradhi. Mambo ya msingi ambayo ni haki yake kuhoji na kudadisi wamuongoze ahoji na kudadisi kwa adabu.
 
Mtambuzi hii story mbona kama ya kutunga ili ifikishe ujumbe wa watoto wetu wa leo hii? Is it real my bro?
 
kaka binti yako ni mtambuzi sana,...
usimkaripie ila mfundishe yote lakini umwambia na madhara yake.

Yawezekana akijua mengi,kama alivo onesha kutaka kujua mengi yata
msaidia kujilinda katika umri mbaya unaokuja.

Nakumbuka mdogo wangu (mvulana),.......alibarehe
akiwa 11,lakini alikua anajua mambo mengi kuliko hata mimi,hata kutongoza.

Ila kujua kwake mengi kumemsaidia kujua nini afanye,na lini afanye ingawa ni
mtukutu balaa.,....ni udadisi tu anao,usiue kipaji hicho.
 
...mtambuzi, mwanao anaku challenge kidogo tu presha inakupanda?
hapana bana...jirudishe kwenye 8yrs old....fikiria ungekuwa wewe ungefikiria nini...
kiukweli nimefurahishwa na maendeleo ya bintiyo...

ni juu yako na mama'ke kumuendeleza hiko kipaji cha kutaka kujua.
ingekuwa uswahilini au wazee waliokosa busara ungekuta huyo mtoto keshakula
bakora na onyo asirudie tena kuuliza maswali ya 'kipuuzi'...kumbe mzazi kapitwa na
kiwango cha elimu na busara...
 
Kama anakupinga hadi wewe baba yake, tandika huyo. Ipo siku atakuaibisha.
Mjengee mazingira atambue kuwa wewe ni baba, hawezi kukupinga hovyo.
Tanzania bado hatujafikia hatua ya kukaa na kudiscuss mambo sensitive kama hayo na watoto wa umri wake.
Lazma uwe mkali.
 
maadili tu yameporomoka siku hz,mleen mtoto wenu awe na hofu na MUNGU, pia ajue nini cha kuongea na baba na nin cha kuongea na mama kwa heshma na adabu,coz kwa hayo majibu anayompa mama yake akikua kidogo ipo siku atakuja kupigana na mama yake,pia inaelekea tatizo lipo kwenu pia wazazi either mnamdekeza sana or mnamuacha sana free kuongea chochote anachotaka mbele yenu...mpen darasa
 
Kama anakupinga hadi wewe (NYIE) baba (WAZAZI) yake, tandika (MREKEBISHENI) huyo. Ipo siku atakuaibisha.
Mjengee mazingira atambue kuwa wewe (NINYI) ni baba (WAZAZI), hawezi kuku(WA)pinga hovyo.
Tanzania bado hatujafikia hatua ya kukaa na kudiscuss mambo sensitive kama hayo na watoto wa umri wake.
Lazma uwe mkali.

Mzee wazazi wote wanastahili heshima so wamlee katika hali ya kuheshimu wazazi wote wawili na yeyote anayemzidi umri awe mzazi au jirani. Heshima ya mtoto kwa wakubwa na wadogo ndiyo inayowaweka uchi wazazi wake. Kama ana waheshimu watu basi wazazi wamemlea vema la sivyo akimisbehave hawatasema Mtoto huyu vipi? watasema mtoto huyu kalelewaje? ambalo ni tuc kwa wazazi/walezi.

2. Kupinga hatukatai kwani ni sawa tu kwa mtoto kujengewa kujiamini na kuamini mawazo yake. Mwache akupinge ili uwezejua anachofikiria/jua. Issue ni anakupingaje? Kwa hoja au kwa nguvu? kwa adabu na heshima au kwa dharau? Mtoto mwingine anawezakukupinga kama anavyopingwa shuleni na wenzake au mwalimu wake. Mwalimu akimpingwa kwa dharau na jeuri ile ya hebu nawe unajifanya mjuaji, hakawii kukutolea the same, baba nawe unajifanya mjuaaaaaaaji - mbele za watu. So kukupinga akupinge lakini akupinge kwa ustaarabu, maadili na heshima.

Unawezamfunza kutumia maneno kama lakini baba/mama mbona tumefundishwa a,b,c wakati wewe unasema ni c,b,a? unaanzia hapo kumwelewesha. Halafu kumtandika si kumrekebisha Mzee, sana sana utamtia usugu na kisha kuua kabisa hata kipaji chake cha kudadisi.
 
Mtambuzi..Binti yako kichwani kumetulia ..na anakimbia kwenda mbele..inabidi nawe ukimbie kwenda mbele, kikubwa hakikisha Ki-saikolojia unakuwa unafikiri mbele yake muda wote. Kuna aina ya kumpinga ambayo inaweza kumvunja moyo na kupunguza kasi yake ya udadisi mzuri.

Kingine tukumbuke watoto wanatumia muda mwingi shuleni kuliko nyumbani. Tunaamini walimu wanapanda mbegu bora, lakini hatuna uhakika huo. Binti ambaye ana-challenge mzazi ni dalili nzuri ya kujua kile wanachopandikizwa shuleni kuliko yule ambaye yuko kimya.

Ushauri wangu ni kuwa uendelee ku-challenge binti yako ili ujue anafikiri nini.. Ni vizuri kama utachukua njia yake ambayo yeye anapenda kama vile inaonekana anapenda kutoa ushahidi "facts" kwa kile anachojua, basi nawe toa ushahidi kile unachompinga hata kama itabidi utengeneze kipeperushi wewe mwenyewe ili kuthibitisha kuwa watoto hawatakiwi kujua zaidi mambo ya uzazi wa mpango.

Otherwise, inabidi ushukuru Mungu kupata mtoto ambaye zinachemka na mdadisi..
 
Binti yangu ndio kwanza ametimiza miaka 7 mwaka huu, lakini amekuwa na mabadiliko makubwa sana kitabia. Ni mwaka huu ndio ameingia darasa la pili na amekuwa ni mdadisi na mbishi kupindukia.

Kuna wakati kama tunaangalia kipindi kwenye TV, naweza kutoa maoni yangu juu ya kipindi hicho, kama maelezo yangu hayatakuwa sahihi kulingana na uelewa wake, basi atabishana na mimi na mara nyingi anatoa reference za mwalimu wake (yaani jinsi walivyofundishwa) au kama aliwasikia wanafunzi wenzake wakilizungumzia jambo hilo, hata kama atakauwa amepotoshwa.


Nikiwa kama mzazi, najaribu kumuelewesha kulingana na umri wake lakini unaweza kuzuka ubishi mpaka nakereka. Mh! Watoto wa siku hizi wamekosa kweli adabu. Mfano, kulikuwa na tangazo la Kondom kwenye TV. Wakati tangazo likiendelea akaanza kusema, ‘hizi kondom ndio zinazotumika kuzuia maambukizi ya Ukimwi’

Mimi kwa hekima nikamuuliza kwamba, ni nani amemfundisha, akanijibu kuwa ni mwalimu wao. Nikamwambia ni kweli lakini sio ukimwi tu bali pia hutumika kwa uzazi wa mpango………..
Basi alinikata kalma na kuniambia kuwa uzazi wa mpango wanatumia vidonge vya majira na sindano za kuzuia mimba……………… He! Nilishikwa na butwaa. Mke wangu alinitupia jicho kali kama ananionya, ikabidi nikae kimya……….. nikajua nimechemsha.

Haikuishi hapo, siku iliyofuata alinijia na vipeperushi viwili, kimoja kinachoelezea njia mbalimbali za uzazi wa mpango na kingine kilikuwa kikielezea juu ya maambukizi ya Ukimwi, pamoja na kinga zake, na alikuwa anataka kuthibitisha kile alichokuwa akikisema siku iliyopita.

Nilijaribu kumuelewesha kwamba, mambo hayo sio wakati wake kujifunza kulingana na umri wake, nilimshauri asubiri akiwa mkubwa atajifunza mambo hayo kwa undani. Lakini alizidi kusisitiza kwamba anataka kunithibitishia kwamba jana alikuwa sahihi. Ilibidi nikubali kuwa alikuwa sahihi ili kuepuka malumbano.

Amekuwa na tabia ya kunikosoa bila hata ya aibu na si mimi tu hata mama yake pia hutofautiana naye kwa mambo madogo madogo. Anaweza kutumwa aandae meza kwa ajili ya chakula, yeye anachofanya ni kuondoa vitu vilivyopo mezani tu na kukaa kimya akiulizwa kwa nini hajaandaa meza, anadai ameshaandaa na ndio maana iko safi na haina kitu. Mama yake akimuuliza kwa nini hajaweka sahani na maji na vitu vingine. Anamwambia hakuwa specific, ‘ulitakiwa uniambie nitenge chakula’ atasema, akimkosoa mama yake.

Hebu nisaidieni nimfanyeje binti huyu…………………………?
Ha ha ha! Hapo huna binti,una mcharuko fulani hivi. Tafakari chukua hatua
 
uko sawa mamaa. japo nilipata feeling huyu binti anakuwa anafanya hivi coz anaona mbona kila kitu hawajui? ofcoz wakati mwingine anahitaji kuadhibiwa kwa fimbo ama kwa kunyimwa preveledge zingine za kitoto kama tv na mtoko. ili atambue kuna authority. anaweza pia kufundishwa jinsi ya kubishana ama ku-challenge watu as such bila kuwaudhi.
Na kweli mwali ila tu nafikiri waangalie namna ya kumkuza kwenye maadili mmema. Kwa jinsi nilivyomsoma naona kama kuna kipunje cha kiburi!! Kama anaambiwa aandae meza, yeye anatandua meza kwa madai ya kuwa mamake kakosea hakumwambia aandae chakula kwa nini atandue na kukaa kuwaangalia kusubiri wamuulize kwa nini ametandua?? Kwa nini akiambiwa aandae meza; asimkosoe tu mama yake kuwa......sio kuandaa meza mama, ni kuandaa chakula .............huku akifanya kile alichokuwa anajua mama yake anakimaanisha?!

Na wasiporeduce hii speed (hasa kwenye kubishana na wazazi wake kwenye vitu vya kmsingi, iko siku atawaumbua mbele ya wageni). Hakawii kuropoka wewe baba umezoea kuja umelewa hadi unakokotwa .....imtoke mbele ya wageni. Ndio anahoji na kukemea tabia mbaya juu ya mzazi wake mlevi lakini sehemu na namna atakavyokemea lawama zote zitakujamrudia mamake kuwa kamdekeza, kamlea vibaya.

Hapana wampunguze speed kwa mambo yasiyo na maana la sivyo wanalea maradhi. Mambo ya msingi ambayo ni haki yake kuhoji na kudadisi wamuongoze ahoji na kudadisi kwa adabu.
 
kabla ya haya mabadiliko mlikuwa mna tabia ya kukaa nae na kuongea au kumweleza mambo ya maisha au maadili??

Kwanza alikuwa ni binti mtaratibu sana na hakupenda kuongea ongea, mara nyingi alikuwa akipenda kuangalia TV na video za katuni tu, haya mabadiliko na kibri vimeanza muda si mrefu, tuseme tangu aingie darasa la pili mwaka huu
 
Wasiwasi wangu akiendelea hivyo halafu akaolewa na mfuasi wa mfumo dume sijui kama wataelewana. Sema naye taratibu ataelewa
Nimekuwa nikijitahidi kumpa elimu ya utambuzi kwa lugha nyepesi kulingana na umri wake lakini tatizo anakuwa na maswali mengi kuliko kawaida na yenye kukera, hasa akiwa na nadharia yake ambayo yeye anaiamini.
Mfano: aliniuliza kuhusu chanzo chetu sisi wanadamu, nikaanza kumweleza kuhusu evolution..............yeye kakimbilia kwenye Dini. akaingia kwenye Biblia akizungumzia Adam na Eva na kisa cha kula tunda bustanini..................... He, nisimamie wapi sasa..................!
 
Mtambuzi hii story mbona kama ya kutunga ili ifikishe ujumbe wa watoto wetu wa leo hii? Is it real my bro?

sasa nidanganye ili iweje? kama unataka nikuletee ukae nae siku moja tu kama hujamrudisha kwangu..............
 
Kwanza alikuwa ni binti mtaratibu sana na hakupenda kuongea ongea, mara nyingi alikuwa akipenda kuangalia TV na video za katuni tu, haya mabadiliko na kibri vimeanza muda si mrefu, tuseme tangu aingie darasa la pili mwaka huu

mkuu hayo mabadiliko yanatakiwa uende nayo sambamba inaonekana kuna mengi anajua hivyo kuna muda unatakiwa usiweke kujua zaidi bali kaa chini umsikilize na ujaribu kutengeneza challenge fulani kwani binti yako anaonekana anapenda sana vitu vya uhakika
... usimkaripie na itabidi ubadili staili ya maisha kuwa nae karibu zaidi ili umwelewe zaidi kuliko kukaa na kuangalia njia ya kumzuia
... kwa hali aliyofikia inatakiwa muwe basi moja ndo mtaelewana
... pili jaribuni kumbadilisha kwa kuongelea zaidi vitu ambavyo mnavitaka nyie na kumfanya muda mwingi atumie kwenye kazi za nyumbani au homework na muda mwingine muwe nae mkijaribu kuongea nae vitu mnavyovitaka nyie
... na mwisho mjitahidi kumpangia muda wa kutumia kuielewa dini zaidi
 
wa hivi hawabanduliki prof, trust me! ukiangalia mentality ya vijana wa siku hizi, hata mwenye umri wa miaka 20 hana ujasiri wa kumshawishi huyu mtoto. Namuonea wivu mtambuzi aisee, na ukimshawishi huyu bintiye atakupiga maswali hadi ukimbie!
Huyo mtoto atabanduliwa mapema sana!
 
mtambuzi, mimi nisamehe lakini naona tatizo linakuja upande wenu wazazi zaidi. approach nyingine, fanya vitu kwa kumuuliza maswali yeye, uchote ufahamu wake ndo kishaye umpe yaliyosalia. na wakati mwingine its ok kumuambia mtoto 'sina hakika na ulisemalo,nitaangalia na kukupa jibu sahihi', nilimheshimu sana baba yangu kwa sababu alikua mwepesi kusema ' nisamehe mwanangu. nadhani idea yako ilikua bora zaidi,tuifanyie kazi' . mwanao hakukosea kuhusu evolution na dini. hizi ni theories mbili zinazopingana na hata mwalimu alietufundisha evolution alikua mlokole na alituambia hivyo! so ni busara kumuambia yuko sahihi na ww uko sahihi. kuna sayansi na kuna mungu, ndo maana tunapika chakula kuua vijidudu na kuondoa sumu lakini pia tunasali kabla ya kula mungu akibariki na kukiponya chakula
Mfano: aliniuliza kuhusu chanzo chetu sisi wanadamu, nikaanza kumweleza kuhusu evolution..............yeye kakimbilia kwenye Dini. akaingia kwenye Biblia akizungumzia Adam na Eva na kisa cha kula tunda bustanini..................... He, nisimamie wapi sasa..................!
 
wa hivi hawabanduliki prof, trust me! ukiangalia mentality ya vijana wa siku hizi, hata mwenye umri wa miaka 20 hana ujasiri wa kumshawishi huyu mtoto. Namuonea wivu mtambuzi aisee, na ukimshawishi huyu bintiye atakupiga maswali hadi ukimbie!

ushawishi wa vitendo na si maneno ....
 
mtambuzi, mimi nisamehe lakini naona tatizo linakuja upande wenu wazazi zaidi. approach nyingine, fanya vitu kwa kumuuliza maswali yeye, uchote ufahamu wake ndo kishaye umpe yaliyosalia. na wakati mwingine its ok kumuambia mtoto 'sina hakika na ulisemalo,nitaangalia na kukupa jibu sahihi', nilimheshimu sana baba yangu kwa sababu alikua mwepesi kusema ' nisamehe mwanangu. nadhani idea yako ilikua bora zaidi,tuifanyie kazi' . mwanao hakukosea kuhusu evolution na dini. hizi ni theories mbili zinazopingana na hata mwalimu alietufundisha evolution alikua mlokole na alituambia hivyo! so ni busara kumuambia yuko sahihi na ww uko sahihi. kuna sayansi na kuna mungu, ndo maana tunapika chakula kuua vijidudu na kuondoa sumu lakini pia tunasali kabla ya kula mungu akibariki na kukiponya chakula

Nakushukuru sana kwa maoni yako, nitajitahidi sana kutumia mbinu hiyo, naamini itanisaidia........................ Kuna jamaa yangu kaniambia kuwa inawezekana akavunja ungo mapema, hiyo nayo imenishtua sana, MIAKA 7! inawezekana kweli? na kama ni kweli nadhani akili yake itakuwa anaendana na maumbile yake...................... anyway maoni yenu kwa ujumla nitayafanyia kazi.
 
Back
Top Bottom