Jamani hii ya Kamanda Kova imekaaje?

Kama ana heshima ampigie basi Dk. Slaa kama haujasikia another version of story, labda aseme to the late Kanumba was secret service na alikua na cheo kuliko yeye, otherwise babu kachemka mazima

Mkuu, kamanda kova ampigie saluti dr slaa wakati gani?
 
kova hajakosea.., polisi na jeshi, wote wanapaswa kum-salute marehemu YOYOTE..., awe na cheo asiwe na cheo.., ni heshima anayopewa marehemu..,

haku-salute kwa sbb ni kanumba, amesalute kwa sbb yule ni marehemu na anapewa heshima yake....,

kama hujui kanuni na nidhamu za kijeshi usibishe vitu usivovijua.., lakn ku-avoid kuchanganya watu wasiojua haya mambo ndio maana servicemen wengi wanaenda na civ clothes,

Ile ni nidhamu ya kijeshi kwa marehemu wetu si kwa sbb ni kanumba, nada!
 
Huyo mzee alikuwa anatafuta jinsi atakavyotoka kiaina. Kanumba alikuwa na title gani hadi kupigiwa saluti?

Kwa maoni yangu kamanda Kova hakuwa sahihi kuipigia salute maiti ya Kanumba.

Sababu salute ni salamu au heshima ya kijeshi kwa mtu aliyekuzidi cheo au mamlaka.

Kova anajua miko ya salute lakini nadhani alipitiwa tu.
Kama kitu haukifahamu kwa kina hakuna haja ya kubishana..... Waache wenye uelewa na jambo watoe ufafanuzi.

 
Mzee Luhala kaeleza vizuri lakini bado tusiokuwa wajeshi hatumwelewi.

Ndio maana wengine hata hawajui kwa nini tu maskini!
 
Huu ni ushenzi/ujinga wa kutojua mamlaka. Najiuliza, Kanumba alikuwa na mamlaka gani Tanzania? Hakuchangia chochote kwenye pato la taifa na hakuitangaza Tanzania kwenye sinema yeyote aliyetoa/kucheza halafu leo hii anapigiwa saluti kana kwamba yeye ni kiongozi wa nchi? Hapa sasa muone jinsi hii nchi ilivyo na viongozi feki. Haya ndiyo matokeo ya kuroga ili upate cheo wakati kazi huijui. Jamani, tutafika kweli?
 
Kwa uelewa wangu ambao si shaka nao heshima ya mwisho inayotolewa kwa mwili wa marehemu na skari jeshi,polisi,au magereza anapokuwa amaevaa unifomu na saluti ya kijeshi. Hii haitegemei kama marehemu wakati wa uhai wake alikuwa askari au kiongozi wa kiserikali, hii ndiyo protocali ya vyombo hivyo wakati wa msiba. so kamanda kova hakukosea na alifanya hivyo kama heshima yake kwa marehemu na sio kwa sababu ya uwepo wa viongozi.
 
Jaman watu hebu eleweni. Jeshini hakuna shikamoo, za asubuhi wala habari gan. Kule saluti tu. Kova hajakosea hata kdogo.
 
Jaman watu hebu eleweni. Jeshini hakuna shikamoo, za asubuhi wala habari gan. Kule saluti tu. Kova hajakosea hata kdogo.
 
quote_icon.png
By luhala
Nimesoma gazeti la Tanzania Daima leo habari hii na imenishangaza sana

Ukweli ni kwamba Kova alikuwa sahihi kabisa kwa kitendo alichofanya na kwa ufafanuzi alioutoa na nimemkubali kwa elimu aliyoitoa kwani kisheria Saluti ni alama ya heshima kwa mkuu au mtu mwenye mamlaka juu yako. Kimsingi nyuma ya Majeshi yote duniani yana raia kama wawezeshaji wakuu wa uwepo wao. Katika mila na desturi za kijeshi Raia wa kawaida hapigiwi saluti isipokuwa kama yafuatayo yatajiri:
i. Akiwa na cheo cha kisiasa ambacho moja kwa moja anamwakilisha Rais , Mfalme, Malkia au Mkuu wa nchi.
ii. Akiwa amefariki ambapo askari au Afisa bila ya kujali cheo chake hata kama ni CDF (Chief of Defence Forces) IGP
au Kamishna anapaswa kusimama kwa heshima na kuupigia saluti mwili kutoa salamu na heshima kwa Raia yule
ambaye kimsingi ndiye aliyekuwa mwajiri wake. Saluti kwa mwili haijalishi umri, jinsia, wala cheo cha marehemu
alipokuwa mzima wala rika la marehemu kulinganisha na anayeitoa saluti hiyo. Kwa maana hiyo askari aliyeiva
sawasawa kama Kamanda Kova na anayejua wajibu wake ataupigia saluti hata mwili wa mtoto mdogo ukiwa
umeandaliwa kwa mazishi au ukiwa safarini kuelekea huko.
iii. Katika nchi za kifalme Malkia na familia ya kifalme hupigiwa saluti.
NB: Ninayeandika haya ni Afisa Mwandamizi Mstaafu aliyehudumia JWTZwa zaidi ya miaka 40 hadi kustaafu miaka kadhaa iliyopita na aliyefanya mafunzo (Na kufundisha) ndani na nje ya nchi hii.
Changamoto: Maafisa na maaskari wa leo ambao awali hamkuwa mkijua hili kama huyo Afisa aliyenukuliwa na gazeti hilo mjifunze kutokana na somo alilolitoa Kova. Bravo Commander Kova.
Hata wewe hujajibu. Kwa ufupi Kova alikuwa sahihi kupiga salute ile ni msingi wake si mwili wa marehemu bali hoja ya kwanza ni kuwa alivaa uniform na pale alikuwepo Makamu wa Raisi na baadhi ya Mawaziri amabao wanapigiwa salute kwa hiyo anapopita pale pamoja na mwili salute inaonyesha utii wa kijeshi kwa wakuu waliokuwapo ktk wale waombolezaji km kusingekuwa na hao heshima kijeshi au kwa askari alovaa unform hawezi bend atakunja mikono na kuinuka kidogo lkn kwa uwepo wa viongozi wale anatoa heshima hiyo kutambua uwepo wao hapo. Tanzania daima nao wakurupukaji
Kipara Kikubwa umechemka, haijalishi kama kuna uwepo wa Rais, Makamu, Waziri Mkuu au hata waziri kwani hata mimi na ujuzi wangu wa kawaida nafahamu ni sahihi kwa askari kutoa heshima ya saluti kwa maiti anapokuwa kwenye sare rasmi. Ufafanuzi wa Luhala ni sahihi na nimeshashuhudia mara nyingi hilo likitendeka si Tanzania tu bali hata nje ambapo bila ya uwepo wa viongozi wakuu wa nchi maafisa waliovalia sare walitenda hivyo kwa maiti ambaye ni raia. Kwa hapa nyumbani nimewaona JWTZ wakifanya hivyo na ni lazima nikiri kwamba nilikuwa sijawahi kumwona Polisi, magereza au uhamiaji wakifanya hivyo ingawa sikushangaa Kova alipofanya hivyo kwani nilidhani mafunzo wanayopata wote ni sawa sawa.
Kwa hiyo kama wewe ni askari au afisa rudi kafanye homework. kwa hiyo naunga hoja za wanaomsapoti Afande Kova.
 
Kwa maoni yangu kamanda Kova hakuwa sahihi kuipigia salute maiti ya Kanumba.

Sababu salute ni salamu au heshima ya kijeshi kwa mtu aliyekuzidi cheo au mamlaka.

Kova anajua miko ya salute lakini nadhani alipitiwa tu.

Mkuu mala ya kwanza nilidhani kama wewe kuwa amekosea,
lakini nimeuliza wataalamu wa mambo ya jeshi wanasema alikuwa sahihi kabisa,
kwa mwanajeshi akiwa amevaa kijeshi salamu yake kubwa ni salute,
Asingeweza kuinama wakati amevaa kijeshi na Salute inaonyesha heshima.
Na ndiyo salute hutolewa kwa uliyemzidi cheo lakini naye anarudisha kwa salute,
kwa hiyo mnapigiana salute mkuu!
 
Huu ni ushenzi/ujinga wa kutojua mamlaka. Najiuliza, Kanumba alikuwa na mamlaka gani Tanzania? Hakuchangia chochote kwenye pato la taifa na hakuitangaza Tanzania kwenye sinema yeyote aliyetoa/kucheza halafu leo hii anapigiwa saluti kana kwamba yeye ni kiongozi wa nchi? Hapa sasa muone jinsi hii nchi ilivyo na viongozi feki. Haya ndiyo matokeo ya kuroga ili upate cheo wakati kazi huijui. Jamani, tutafika kweli?
JF kumbe wengi hamjui na hamtaki kuuliza mnaleta ubishi tuu, tafuteni data jamani!
 
Wewe ndi hujui protocol za kijeshi...kijeshi maiti yeyote inapigiwa salute...sasa wewe raia haya mambo huyajui bora ukae kimya...

Si ndio maana kasema hajui, sasa wewe unayejua umueleweshe sio kumwambie akae kimya.
 
Kama ana heshima ampigie basi Dk. Slaa kama haujasikia another version of story, labda aseme to the late Kanumba was secret service na alikua na cheo kuliko yeye, otherwise babu kachemka mazima
mkuu kila jamii duniani ina jinsi ya kufanya mambo yake pamoja na fikira. Kwa bahati mbaya wengi wetu hapa tz tulikuwa hatujajitambua upeo wetu wa kuangalia mambo lakini kwa hili tunaanza kupata picha kuwa sisi ni 'genius' kiasi gani

 
kova hajakosea.., polisi na jeshi, wote wanapaswa kum-salute marehemu YOYOTE..., awe na cheo asiwe na cheo.., ni heshima anayopewa marehemu..,

haku-salute kwa sbb ni kanumba, amesalute kwa sbb yule ni marehemu na anapewa heshima yake....,

kama hujui kanuni na nidhamu za kijeshi usibishe vitu usivovijua.., lakn ku-avoid kuchanganya watu wasiojua haya mambo ndio maana servicemen wengi wanaenda na civ clothes,

Ile ni nidhamu ya kijeshi kwa marehemu wetu si kwa sbb ni kanumba, nada!
Well said and excellent comment. Tatizo hapa ni baadhi ya watu kuingilia fani wasiyoifahamu sawasawa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom