BADILI TABIA
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 32,772
- 23,160
sitoenda kwa mganga....mganga ni Mungu peke yake, nitamwomba anitie nguvu na hekima ktk kipindi hicho kigumu, na kuyaacha yote mikononi mwake...
hadithi njoo....
Upo kwenye ndoa na mumeo mna ndoa yenye furaha tele na mmejaaliwa mafanikio yote!Ya kifedha na kiuhusiano!Na pia mmejaaliwa mtoto mmoja tu wa kike na anafanana sana na wewe mama yake!Bahati mbaya baada ya kujifungua mtoto huyo ukapata matatizo ya uzazazi yaliyopelekea ukaondolewa mfuko wa uzazi.Huwezi kuzaa tena. . .Tatizo linakuja mwanao anaanza kuugua sana unampeleka hosptl haponi,hali inakua mbaya zaidi na mtoto anaanza kuwa na mabakamabaka mwili mzima kama nyoka,mnapeleka kuombewa inashindikana,mnaamua kumpeleka hosptl za nje ya nchi;Nairobi,South Africa mpaka India lakini hali inakua mbaya zaidi.Mumeo ni mtu wa dini na ameokoka hataki kusikia mambo ya waganga wa kienyeji.Unaamua wewe mwenye kumpeleka mwanao kwa mganga,mganga anamkagua mwanao na anakwambia anaweza kumtibu lakini kutokana na ugonjwa wa mwanao kwa sababu ni wa kike dawa ile itamtibu mwanao kwa wewe na mwanao kuitumia kwa njia tofauti.Mwanao utamwogesha na dawa ile pamoja na kumnywesha.Wewe utaioga dawa ile lakini pia inatakiwa mumeo aipake dawa ile kwenye uume kisha akuingilie kinyume na maumbile halafu baada ya siku 3 unywe dawa ile!Ungefanyaje?Kuna mwanamke mwenzio anachangamoto hii,jaribu kumsaidia!
Well at least that is what you think you would do. But trust me you do not know that for sure now. YOu will know for sure if you find yourself in that kind of a situation.hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea no matter how long it will take nitastick kwa MUNGU wangu
Watu mnashangaza sana, Hivi mnaleta ubishi hapa kwa kuwa hawa waganga wa kienyeji mnawajua au mnawasikia tu??!!!!!!!!!!! Acheni kabisa hawa waganga wa kienyeji wana masharti ya ajabu mno, mimi nadhani saa nyingine hata shetani mwenyewe huwa anawashangaa.hiyo dawa hakuna duniani, kwahiyo kwanza sikubaliani na post yako
hahhahahahah mkuu nimecheka hadi nimetoa machozi, wewe ni nourma.Baada ya kushindwa Mashart:
Mama: mganga mashart yamekua magumu, hamna jinsi nyingine ya kunisaidia?
Mganga: kakataa?, inamaana hampendi mtoto?, ngoja niongee na mizimu kama ina dawa nyingine!
Mama: nitashukuru sana.
Mganga anapiga mikwara na geresha nyiiingi eti anaongea na majini/mizimu yake
Mganga: mama nenda ukamwogeshe dawa mtoto, mabaki yafunge kwenye chupi ya mumeo, weka chini ya godoro upande wake hlf kesho njoo nayo. usimwambie mtu ulichobeba wala unakoenda
mama unajitahidi kesho unaenda kamili, umefanya hivyo.
Mganga: umefanikiwa?, vizuri sana. kaa hapo.
Anajifunga kutambaa usoni, anapiga mikwara mingi huku hakuoni, anakutaka uvue akupakie dawa kwa kutumia kidole.
unajiaminisha hakuoni utavua na atakupakia dawa kote kote!
Habari ndio hiyo!, kifuatacho.
Samahani,
Msinisute kuchungulia wanawake
Hakuna cha uganga hapo bali ni WIZI MTUPU!!!! Dawa gani hiyo ya kumtibu mgonjwa (mtoto) inatakiwa itumiwe pia na Wazazi kisha Mume amlawiti mkewe!? Mwenyezi Mungu tunusuru na waganga wasanii!!!
​Mamdenyi nakuomba ufute kauli yako.......Mungu hashindwi kituYaliyomshinda Mungu, mganga atayaweza kweli???????
Soma juu ya mistari mzee wa feki utamuelewa Mamdenyi alikuwa anakusudia kusema nini.​Mamdenyi nakuomba ufute kauli yako.......Mungu hashindwi kitu
Ngozi ya mwanangu ina uhusiano gani na maumbile yangu? Ujue ndo maana Mungu katupa wanadamu utashi wa kujua mema na mabaya na hata kutafakari na kujua uhusiano kati ya unachofanya na unachotaka kitokea na ukiangalia hapa hakuna uhusiano wowote