Elections 2010 Jamani hata Dodoma mnakosa watu

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Mkutano wa Bilal wakosa watu,
Magari yakodishwa kuuokoa

Fukuto la kura za maoni lingali linachemka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiasi cha kuathiri mahudhurio ya wanachama kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Mweza, Dk. Mohammed Gharib Bilal, hali iliyolazimu kusafirisha watu kwa magari baada ya uwanja kuwa mtupu.

CCM ilalazimika kuwasafirisha wanachama wake kwa malori ili washiriki mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza katika kata ya Dodoma- Makuru mkoani Dodoma jana.

NIPASHE ilishuhudia watu waliovaa sare zinazotumiwa na CCM zikiwa na rangi ya kijani, njano na alama ya jembe na nyundo, wakiwa wamebebwa kwenye malori na kushushwa katika uwanja wa mikutano uliopo kwenye kata hiyo.

Miongoni mwa watu waliokuwa kwenye malori hayo ni wasanii wa vikundi mbalimbali vya burudani.

Mkutano huo ulipomalizika, malori yaliyotumika awali, yaliwabeba wasikilizaji wa mkutano huo na kuwarejesha kwenye maeneo tofauti yaliyosemekana kuwa karibu na makazi yao.

Kata hiyo inasadikiwa kuwa ngome ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hasa baada ya mgombea udiwani aliyeshinda katika kura za maoni katani humo, Ally Biringi, kuihama CCM na kujiunga na chama hicho cha upinzani.
 
Si wangewachukua wanafunzi wa shule za sekondari wakajaze idadi!
Alafu mkuu Quinine hiyo avatar yako kila nikiiangaliia huwa nashindwa kujizuia kucheka.
Hebu nikumbushe huyo ni nani na hapo alikuwa anafanya nini viilee??
 
On a very serious note!!
Hizo pesa za kubeba watu na malori zinaingizwa kwenye Gharama za Uchaguzi?
 
Pole pole watanzania wanaanza kupona na ugonjwa wa CCM, huenda wanaogopa kuanguka kama mwenyekiti wao
 
Pole pole watanzania wanaanza kupona na ugonjwa wa CCM, huenda wanaogopa kuanguka kama mwenyekiti wao
What i know Dodoma na Singida ni ngome za CCM kama ilivyo Pemba ya CUF lakini niliposoma habari hii siamini kabisa kama ndiyo yanatokea kwa CCM.
 
On a very serious note!!
Hizo pesa za kubeba watu na malori zinaingizwa kwenye Gharama za Uchaguzi?
Siku hazigandi....
Taratibu, chembe na chembe hawa watu watabadilika!
Wanafahamu taratibu kuwa ccm si ya class yao!
 
Hata Mbuyu huwa unaanguka sembuse CCM watabeba watu kwenye malori na kuwapa pesa,vitenge,skafu,tshirt,kofia nk lakini wataanguka tu tumewachoka ccm wamwafanya wananchi kama mandondocha sasa wananchi wamefunguliwa hakuna rangi watakayo acha kuiona!
 
Mpelekeni Mheshimiwa Said Mzee Said Dodoma naye tuone jinsi atakavyofunika bovu--
 
Mpelekeni Mheshimiwa Said Mzee Said Dodoma naye tuone jinsi atakavyofunika bovu--

04_09_4heph61.jpg


Unaweza sema chochote juu ya hii ndoa?
 
04_09_4heph61.jpg


Unaweza sema chochote juu ya hii ndoa?

I call that political maturity. Being able to sit, talk, and laugh with your opponents. Maintaining civility in our politics. Something folks from Chadema haven't acquired yet. Au unasemaje Mchungaji?
 
I call that political maturity. Being able to sit, talk, and laugh with your opponents. Maintaining civility in our politics. Something folks from Chadema haven't acquired yet. Au unasemaje Mchungaji?

Try again ! Not convinced
 
CCMhaina chake mwaka huu, hiyo ni dalili tosha kuwa ccm imechokwa na watanzania wa sasa HAWADANGANYIKI.
 
Mkutano wa Bilal wakosa watu,
Magari yakodishwa kuuokoa

Fukuto la kura za maoni lingali linachemka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiasi cha kuathiri mahudhurio ya wanachama kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Mweza, Dk. Mohammed Gharib Bilal, hali iliyolazimu kusafirisha watu kwa magari baada ya uwanja kuwa mtupu.

CCM ilalazimika kuwasafirisha wanachama wake kwa malori ili washiriki mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza katika kata ya Dodoma- Makuru mkoani Dodoma jana.

NIPASHE ilishuhudia watu waliovaa sare zinazotumiwa na CCM zikiwa na rangi ya kijani, njano na alama ya jembe na nyundo, wakiwa wamebebwa kwenye malori na kushushwa katika uwanja wa mikutano uliopo kwenye kata hiyo.

Miongoni mwa watu waliokuwa kwenye malori hayo ni wasanii wa vikundi mbalimbali vya burudani.

Mkutano huo ulipomalizika, malori yaliyotumika awali, yaliwabeba wasikilizaji wa mkutano huo na kuwarejesha kwenye maeneo tofauti yaliyosemekana kuwa karibu na makazi yao.

Kata hiyo inasadikiwa kuwa ngome ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hasa baada ya mgombea udiwani aliyeshinda katika kura za maoni katani humo, Ally Biringi, kuihama CCM na kujiunga na chama hicho cha upinzani.

Hivi Bilal aliongea nini sasa? Ahadi ya kuwajengea shule wakati wasikilizaji hawaishi hapo? Haya sasa yamekuwa maigizo!
 
Mkutano huo ulipomalizika, malori yaliyotumika awali, yaliwabeba wasikilizaji wa mkutano huo na kuwarejesha kwenye makazi yao.
Makubwa
 
Hivi Bilal aliongea nini sasa? Ahadi ya kuwajengea shule wakati wasikilizaji hawaishi hapo? Haya sasa yamekuwa maigizo!
yaya njoo ujibu hapa!!!

Bilal kaahidi kuhamishia serikali dodoma!! ameahidi mzee wa meno nje!!
 
yaya njoo ujibu hapa!!!

Bilal kaahidi kuhamishia serikali dodoma!! ameahidi mzee wa meno nje!![/QUOTE]
Anawang'ong'a watu wa ccm walio kwenye mkutano wao, na hivyo atawang'ong'a wote walio karibu yao, Mtu hata mvuto Hana.! Bahati yake tu kaenda shule.!!! LOL sisiem wanachezea akili ya umma Huu wakati kila mmoja ameamka sasa,Octoba lazima kieleweke ili wapate fundisho la milele hawa watu.
 
Back
Top Bottom