Usipo ona ya Musa utaona ya firauni.Nilishasema,na narudia tena,watanzania tumekwisha, maana tumeshapoteza uwezo wa kujua mema na mabaya kabisa.Ni Diwani,tena aliyechaguliwa na watu,ili awaletee maendelea yao,halafu anakurupuka na kusema machangudoa wapewe leseni kwa vile wataliingizia taifa mapato. Anashindwa hata kujua kwamba hela za machangudoa ni hela chafu, kama zilivyo hela za mafisadi tunaowapigia kelele leo kwa nguvu zetu zote.Diwani anayeshindwa kujua kwamba umalaya ni uwovu mbaya sana katika jamii,ambao kama haukudhibitiwa unaiingiza jamii husika katika laana isiyozungumzika.Hao ndio viongozi tulio nao, mbumbu,wenye mawazo yaliyofirisika.