Mzee wa Rula
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 8,171
- 3,346
Uzi hui umekaa kufurahisha nafsi za watu lakini uhalisia ni mdogo.
Wakijiunga na chadema wote kabisa mpaka wale wenye sifa mbaya, basi ni dhahiri kabisa kwamba chadema itaanguka mwereka wa mende.
Hivi huko bado inatakiwa eeh?
ingikuwa ni pesa tungeifanya fixed accountKaburini
Wakijiunga na chadema wote kabisa mpaka wale wenye sifa mbaya, basi ni dhahiri kabisa kwamba chadema itaanguka mwereka wa mende.
Kuwa makini ndugu yangu, hisia za kidini ni hatari sana kwa amani na ustawi wa taifa lolote lile duniani. Tukianza kuliendesha taifa hili kwa kila mtu kufikiria mustakabali wa dini yake badala ya taifa hatutafika popote. Ni lazima tufikie mahali pa kuweza kutofautisha mambo. Pale panapostahili utaifa tuweke utaifa, na pale panapstahili dini tuweke dini. Tusipeweza kuyatenganisha maeneo haya mawili, itakuwa ni ishara tosha kwamba bado hatujastaarabika kama taifa. Kama kweli kanisa lilipandikiza watu kupitia Nyerere, je! waislamu wengi tulionao leo katika serikali walipandikizwa na nani na kupitia mgongo wa nani? Nafikiri si vizuri kulaumu kundi fulani la watu pasipo kuwa na "concrete evidence" kuhusu lawama zetu. Mwisho nasema, Jihadhari sana kuendekeza hisia za udini, maana madhara yake hayachagui kwamba huyu ni mwislamu na huyu ni mkristo, bali yanawafagia wote.Kilicho najisi mapambano ya uhuru na kuharibu maana ya uhuru wa mwafrika ni kanisa kupandikiza watu watu wake kupitia nyerere. Kilichofuata ni kuanzisha raia wa daraja la pili na la kwanza. CDM isije kudhani waislamu hawakupata fundisho kutoka katika hili, tutaendelea kuwatumia watu wenye nia njema na maslahi ya waislamu waliopo ndani ya CDM.