Jamani bodi ya mikopo toeni majina;watu kujua hatima yao mapema ni jambo muhimu

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Hawa watu wa bodi ya mikopo ni watu wasiojua umuhimu wa kutoa taarifa zao mapema kwa wahusika.Hata kama kuna waliofanya makosa isiwe sababu ya kuchelewesha kutoa majina.TCU wameongeza muda mpaka tfh 07/09/2012,sasa ina maana hawa bodi wataendelea kusubiri kisa kuna makosa yamefanyika?Deadline nyingi za TCU na HELSB zimeshapita lakini hawa bodi hakuna kinachoendelea kuhusu kutangaza majina.Mbona TCU wao wametoa selection zao kwa wale ambao hawakuwa na matatizo?Sasa kwa nyinyi bodi ya mikopo mnashindwa nini?

Najiuliza kulikuwa na umuhimu gani wa kuanza kufanya maombi ya mkopo mapema kama mpaka leo mmeshindwa kuwajulisha waombaji ni kiasi gani watarajie kupata kutoka bodi?Nani asiyejua ugumu wa kutafuta na kupata fedha?Muda uliobaki kwa vyuo vingi kabla ya kufunguliwa ni chini ya mwezi mmoja ila nyinyi mnakuwa kama hamlioni jambo hili!

Jamani kujali muda ni jambo la msingi sana, kwani litaepusha matatizo mengi kwa wanafunzi walioomba mkopo.
 
Mkuu bodi ya mkopo ipo sawa kwasababu wao wanapewa bajeti nzima ya mkopo kila mwaka so lazima majina yakamilike ndio waanze kuchambua wasio jiweza kwanza ndio wengine wafuate,wakigawa kabla ya kupewa majina yote na tcu,wanaweza wakawaacha watu wenye uwezo wa chini kabisa....ila la kulaumu ni ma IT wa tcu hawapo care na muda kabisa,hawajui watu wanaenda chuo mwezi huu,nachohofia ni kwamba hata wakitoa majina ya mkopo hizo pesa si zitatumwa disemba?
 
Mkuu bodi ya mkopo ipo sawa kwasababu wao wanapewa bajeti nzima ya mkopo kila mwaka so lazima majina yakamilike ndio waanze kuchambua wasio jiweza kwanza ndio wengine wafuate,wakigawa kabla ya kupewa majina yote na tcu,wanaweza wakawaacha watu wenye uwezo wa chini kabisa....ila la kulaumu ni ma IT wa tcu hawapo care na muda kabisa,hawajui watu wanaenda chuo mwezi huu,nachohofia ni kwamba hata wakitoa majina ya mkopo hizo pesa si zitatumwa disemba?

Mkuu nimekuelewa ila kwakweli hii ina kera sana.Hii hatua ya TCU kuongeza muda mpaka trh 7 mwezi huu ni matokea ya either system yao kuwa mbovu au tatizo linaweza kuwa ni watu wa IT hapo TCU.
 
Hivi hiyo tarehe 7 si kesho ama??..tulieni bhana kama kitu kipo kipo tu....mbona mwaka jana yalitoka kipindi hichihichi na watu wakaenda chuo hamna kilicho haribika...
 
Nakushauri ujiandae pesa za kulipia ada chuo kama vile mkopo utapata 0% ili bodi wakikukumbuka iwe sehemu ya kukupunguzia mzigo mkubwa uliojiandaa kuubeba. Vinginevyo hutapata muda wa kujiandaa baada ya bodi kutema
 
kuna jamaa yangu namuamini sana kasha nambia kalamba % ngapi so it means kua tayari wamesha allocate loans na hatujui wanasubiri nini ku publish
 
kuna jamaa yangu namuamini sana kasha nambia kalamba % ngapi so it means kua tayari wamesha allocate loans na hatujui wanasubiri nini ku publish

vp wewe? Jamaa hajakutonya umelamba % ngapi
 
hapa ni sawa na kumpigia gitaa mbuzi...kamwe hata cheza,saut wana report tarehe 14/9 sasa sijui hapo inakuaje!! mtu unafika chuo unaambiwa loan status yako ni NIL!!! inashangaza ila ndo bongoland hii...tungoje naiman bado mda mfupi...
 
hapa ni sawa na kumpigia gitaa mbuzi...kamwe hata cheza,saut wana report tarehe 14/9 sasa sijui hapo inakuaje!! mtu unafika chuo unaambiwa loan status yako ni NIL!!! inashangaza ila ndo bongoland hii...tungoje naiman bado mda mfupi...

7days it's not muda mfupi ni much much mfupi hebu nambie mtu unakula NIL and chuo unatakiwa kuripot 14/09 na hela ndo hivyo tena ni katikati ya mwezi! aisee unaweza practice UJAMBAZI
 
7days it's not muda mfupi ni much much mfupi hebu nambie mtu unakula NIL and chuo unatakiwa kuripot 14/09 na hela ndo hivyo tena ni katikati ya mwezi! aisee unaweza practice UJAMBAZI
bora ujambaz mkuu...vp kuhusu dada zetu??? watakua majambazi?? ni aibu....
 
Back
Top Bottom