Jamani anataka kufia bungeni huyu tumwokoaje??

Mrema wa TLP atangaza kumvaa Kimaro wa CCM Vunjo
Mremalyatonga.jpg
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustino Mrema, anawania kiti cha bunge Vunjo.
broken-heart.jpg
*Kimaro ampuumza asema 'alifulia, atafulia tena'

Na Zaina Malongo

BAADA ya kushindwa kufua dafu mara tatu katika mbio za urais, hatimaye mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustino Mrema amerejea kwenye kinyang'anyiro cha ubunge baada ya kutangaza kuwa atapambana na Aloyce Kimaro kuwania jimbo la Vunjo.

Mrema, ambaye amewahi kugombea urais akiwa na NCCR Mageuzi na baadaye TLP, alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 20 kabla ya kutofautiana na serikali na baadaye kujiunga na upinzani katika miaka ya tisini.

Wakati hali ikionekana kumuendea kombo Kimaro kwenye jimbo hilo, Mrema anaonekana kutaka kutumia mwanya huo kurudi Vunjo ambako TLP ina nguvu kubwa.

Mwenyekiti huyo wa TLP aliliambia gazeti hili jana kuwa baada ya kumtikisa Kimaro katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu ambao chama chake kimeshinda katika vijiji 20 na vitongoji 48 dhidi ya vijiji 47 vya CCM, sasa anajipanga kwenda jimboni humo kugombea ubunge mwakani.

"Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa, sasa namtangazia rasmi Kimaro kwamba mwakani naenda Vunjo kulichukua jimbo langu. Kimaro ameshindwa kuwasaidia wananchi ndio maana wamemzomea," alisema Mrema alipoongea na Mwananchi jana.

Mrema, ambaye alikuwa waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya awamu ya pili, alitoa tamko hilo wakati akizungumzia tuhuma za Kimaro kwamba wanachama wa TLP ndio waliomzomea wakati akihutubia mkutano wa uliofanyika mji mdogo wa Himo ulio kwenye jimbo la Vunjo, Moshi Vijijini Jumatatu iliyopita.

Kimaro alishikwa na maswahibu hayo baada ya kundi la takribani watu 100 wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa chama hicho kumpigia kelele likisema "hatukutaki", muda mfupi baada ya kuwatambulisha wenyeviti wa TLP waliohamia CCM.

Kimaro alidai kuwa kundi hilo ni la watu wachache wa TLP waliotumwa na Mrema kwenye mkutano wake.

“Kundi lilozomea liliandaliwa na Augustino Mrema lililetwa kwenye mkutano wangu na daladala kutoka eneo la Njia Panda, ilipo gesti house na baa yake inayoitwa Twiga. Wao waendelee kuzomea mimi sitishiki na siachi ngozi yangu ngumu nitapambana nao mpaka kieleweke,” alisema Kimaro.
Â
Hata hivyo, Mrema alilieleza gazeti hili jana kuwa Kimaro hakuzomewa na wanachama wa TLP bali alizomewa na wananchi wa jimbo hilo baada ya kuwakera kwa hoja alipokuwa akizungumza jukwaani.

Alisema Kimaro aliwakera wananchi hao kwa kutozungumzia kero ya maji ambayo imekuwa ikiwasumbua kwa muda mrefu na badala yake akaanza kupiga siasa ambazo hazikuwasaidia.

"Mbunge huyo kuzomewa Vunjo si mara ya kwanza," alidai Mrema. "Alishazomewa sana na wananchi sehemu nyingi... alishazomewa Kilema Kaskazini, Kilema Kusini, Marangu Magharibi, leo anashanga nini kuzomewa Vunjo?"

Alisema kutokana na Kimaro kuonyesha kushindwa kuwahudumia wananchi, sasa anaamua kurudi jimboni humo kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwakani.

"Kimaro haliwezi jimbo la Vunjo... ni bora angetafuta jimbo jingine mapema kwa kuwa mimi sasa narudi kumnyang'anya ubunge," alitamba Mrema ambaye baada ya kuondoka CCM alikwenda jimbo la Temeke na kushinda katika uchaguzi mdogo.

Lakini Kimaro hakuonekana kutikishwa na uamuzi huo wa Mrema baada ya Mwananchi kuwasiliana naye kutaka maoni yake.

"Kama anakuja aje, lakini akumbuke yeye ni mtu wa kushindwa tu... kushindwa hakuanza leo; alishindwa mwaka 1995, 2000, 2005 haoni kwamba ni mchovu na kachoka?

"Mrema kafulia miaka yote hii kwenye urais, mwache aje atatukute tukimsubiri na atafulia tena.

"Sio Mrema tu, amefulia yeye na TLP yote , TLP sio chama cha kitaifa, ina watu wawili tu; yeye na kiongozi mmoja hapa Vunjo, mbaya zaidi wote wamefulia, mwenyekiti kafulia na chama kimafulia." Kimaro alisema hatishwi na ujio wa Mrema jimboni humo kwa kuwa ushindi wake umeanza kujidhihirisha katika matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambao KImaro alidai CCM ilishinda vijiji 48, TLP 19 Chadema 10 na NCCR Mageuzi kiti kimoja.


Mwacheni huyu mzee. Kusema kuwa amefulia si sahii,Mrema, ni haki yake kikatiba kugombea. kwani wako viongozi wengine wa vyama vingine tangu kuanza kwa uchaguzi wa vyama vingi wana gomea nafasi ya urais lakini hawajafanikiwa.
Mimi naona watu sahii wa kusema huyu mzee hafai ni wapiga kura wake. Kama wanchi wa jimbo lake wanamkubali, basi agombee ubuge. Sisi hatuna sababu sana ya kumjudge. Bungeni wapo wabunge wazee kuliko yeye, na bado wanaendelea kuwepo bungeni,na chama tawala kinaendelea kuwaweka hata kama hawakuchaguliwa na wananchi, basi wanateuliwa.
 
Kwa taarifa yenu wapiga kura wa jimbo la Vunjo bado wanamkubali sana Mrema kutokana na rekodi ya maendeleo aliyowaletea akiwa mbunge wao miaka kumi iliyopita.

Mnaposema kafulia ati hakufanya ufisadi hapo nawashangaa manake mnajichanganya, hamueleweki mko upande gani.

Mrema ameonyesha mfano wa mwanasiasa wa ukweli, anasimamia kile anachokiamini. Akiwa ccm alipanda sana hadi kufikia naibu waziri mkuu, lakini alipoona hawezi kubadilisha usanii wa chama hicho aliondoka na akakubali kuachia maslahi aliyokua anapata. Aliukataa ufisadi kwa matendo tofauti na wapiganaji waliopo sasa.

Afya ya Mrema haionekani kunawiri lakini sio sababu ya kusema ati ataenda kufia bungeni. Kwani ni wabunge wangapi wameanguka mjengoni na hata kufa, hiyo sio sababu. Anaona anaweza na amejitolea kwenda kuwatetea wananchi wake hata ikibidi kufia huko. huo ndio uzalendo, mwacheni.

Karibu mjengoni mzee wa Kiraracha na anaeweza kupambana na wewe aje Vunjo tumuaibishe.
 
Naona yuko sawa kabisa kwani maisha ya bongo siasa ndo inalipa,msishangae kumwona mkapa naye akitaka kugombea huko nanyumbu,siasa za bongo ni upumbafu mtupu!
 
Naona yuko sawa kabisa kwani maisha ya bongo siasa ndo inalipa,msishangae kumwona mkapa naye akitaka kugombea huko nanyumbu,siasa za bongo ni upumbafu mtupu!

hahaaa, sawa na yule ex-mkuu wa majeshi alipoliaibisha jeshi kwa kugombea!!! yaani siasa inakuwa juu ya ukuu wa majeshi!!

Yes kuna haki ya kikatiba, but wait! Huyu mrema watampima afya kwanza??
 
wana JF,

Kwa nini mzee huyu ambaye alishawahi kuwa naibu waziri mkuu anahangaika hivi?

Mimi naona anatupa ujumbe kuwa yeye hakufanya ufisadi/hakujilimbikizia mali. Na kwa kuwa style ya siasa yetu siyo ya kuwalinda viongozi, basi jamaa hana akitu na hana mbele!

Kwa style hii Mrema atakuwa mfano hai wa watu kuendelea kufanya ufisadi kwa madai kuwa ukizeeka kama 'mrema' upumzike!!

Ni ujumbe tosha kuwa wale watu waliowasafi serikalini mwisho wao ni mbaya at the end anakuwa YEYE NA FAMILIA YAKE!!

we need to discuss this in different orientations!

I submit

Mkuu good observation and nice of you to be objective but you are living out something important. Mshahara wa ubunge halafu na uwaziri unamtohs kabisa mtu kutajirika kihalalai. Hawa viongozi wetu wanaoiba siyo kwamba mishahara na bonus mbali mbali hazi watoshi bali ni wao hawa ridhiki. Haingii akilini mtu aliye kuwa mbunge kwa miaka ishirini mpaka kufikia kuwa naibu waziri mkuu asiwe na pesa na vitega uchumi kisa hakua mwizi. Sasa kama yeye hali yake ni hivyo je wafanya kazi wengine wa serikalini ina kuaje?
 
Ivi hana washauri?
Jamani nasikia eti mama simba alishawai kwenda south kutibiwa maradhi ya kichwa?
 
Lyatonga, tunakumiss bungeni, naamini utarudi tu, maana Wanavunjo wameamua moja, kupeleka jeshi mstaari wa mbele, narudia jambo moja la hakika, A.l. Mrema atashinda uchaguzi ujao. kama mnadhani inahitaji falsafa za kiona mbali kujua hili basi mmepotoka.
mwingine ninayemmiss bungeni ni Thomas Nyimbo, Mbowe,
 
Kwani we ulitaka afie wapi?mwenzako amepiga mahesabu anataka kufia bungeni ila azikwe vizuri kwa heshima kama mbunge na mwanasiasa Mkongwe.Anataka kurudisha hadhi yake kwa kipindi kifupu kilichobaki cha maisha yake.
 
Tatizo la viongozi wengi hawana uchu wa kuwaletea maendeleo ya kweli wana nchi wao ila karibu wote wametanguliza maslahi binafsi.Huyu mzee anataka kurudi bungeni kuboresha maisha yake na si kuwasaidia wananchi wake hata afya naona haimruhusu apumzike tu ni mtazamo wangu tu.

Mvina
Mrema wala hahitaji kuboresha maisha yake kwani anafahamu kwamba ana muda mfupi sana wa kuishi hapa duniani.Anataka kuwa Mbunge ili azikwe vizuri na si vinginevyo.
 
Jamani,ebu tuangalie upande wa pili wa shiliingi,
We voted for this guy mwaka 1995 tena majority votes na aliweza itikisa CCM kwa mara ya kwanza.I can declace kua this guy was good tena sana tu lakini wat happened to him ni makucha ya CCM,CCM crippled him politically,walimuua kisiasa,walipenyeza majungu kipindi kile NCCR halafu TLP hii yote ni kuhakikisha kua wat happened 1995 hakitokei tena,
in short walimuangamiza kabisa,n now here he is,AMEFULIA but coming to another side hyu jamaa kipindi akiwa Waziri tunakumbuka kash kash yake,lets not spit on him but look on wat really happened mpk akawa hapa alipo.
Let him get tht MP thing,tumpe nafasi tena myb he will rise up with smething,n by the way if we can give it CCMz why nt try this guy too?
 
Jamani,ebu tuangalie upande wa pili wa shiliingi,
We voted for this guy mwaka 1995 tena majority votes na aliweza itikisa CCM kwa mara ya kwanza.I can declace kua this guy was good tena sana tu lakini wat happened to him ni makucha ya CCM,CCM crippled him politically,walimuua kisiasa,walipenyeza majungu kipindi kile NCCR halafu TLP hii yote ni kuhakikisha kua wat happened 1995 hakitokei tena,
in short walimuangamiza kabisa,n now here he is,AMEFULIA but coming to another side hyu jamaa kipindi akiwa Waziri tunakumbuka kash kash yake,lets not spit on him but look on wat really happened mpk akawa hapa alipo.
Let him get tht MP thing,tumpe nafasi tena myb he will rise up with smething,n by the way if we can give it CCMz why nt try this guy too?

kumbuka umri na afya yake na ujue hata kingunge kuna wakati alikuwa na busara kabla hajapa ugonjwa wa uzee
 
Bora ya Mrema kuliko Kimaro anaejifanya kupambana na ufisadi wakati hakuna lolote alilowafanyia wananchi wa Vunjo
 
Mwacheni kumsimanga mwingine, kama imekuboa kachukue fomu na wewe ugombee. Alaa
 
Kufia bungeni,si ndio atazikwa na dola,huko TLP mzikaji nani,njaa tupu.
mwaacheni agombee kwani ni haki yake,si mtanzania.Tatizo ni nini,mbona na mimi nataka kugombea kwetu Kyela,mwakyembe kaa mkao wa kula.
 
Acheni kukufuru Mungu, wangapi wazima na wanakufa wanaacha wagonjwa?

Mrema wala hahitaji kuboresha maisha yake kwani anafahamu kwamba ana muda mfupi sana wa kuishi hapa duniani.Anataka kuwa Mbunge ili azikwe vizuri na si vinginevyo.

We nafikiri ni mgonjwa kuliko mrema. Maisha ya Mrema ni bora kuliko unavyofikiri, na sio kila mwana siasa anafuata kipato bungeni. Wapo kina , Ndesa, Mkono, Silaa na wengine wengi wanaliopo pale kwa sababu wanataka kusimamia kile wanachokiamini. Na hiyo ndo siasa.
 
huyu mzee mbona ashakufa kabla ya kuingia bungeni uoni kama kapigwa manati na rostam...sijui ataongeaje kwenye kampeni...embu ccm kumbukeni waliofika ngazi za juu jamani watatufia njiani....yameshinda babu....loooh haya ndio matatizo ya kushindw akurekebisha maisha ukiwa kazini unataka kurekebisha kwenye pesa za ridandas nani kakwambia pesa za ridandas zinajenga nyumba ...mrema kanyi ruwa oko mndumi ngiseka mpaka ngifa...richa kapsa mbe oko wekunyamala nuichi nkui kolimba,kombe, wakeri ambuya necha mleu kanyi...ulakucha wose

Mazishi yake yalifanyika wapi ?.Wapiga kura wa Vunja waachwe waamue nani wanataka awe mbunge wao 2010.

wana JF,

Kwa nini mzee huyu ambaye alishawahi kuwa naibu waziri mkuu anahangaika hivi?

Mimi naona anatupa ujumbe kuwa yeye hakufanya ufisadi/hakujilimbikizia mali. Na kwa kuwa style ya siasa yetu siyo ya kuwalinda viongozi, basi jamaa hana akitu na hana mbele!

Kwa style hii Mrema atakuwa mfano hai wa watu kuendelea kufanya ufisadi kwa madai kuwa ukizeeka kama 'mrema' upumzike!!

Ni ujumbe tosha kuwa wale watu waliowasafi serikalini mwisho wao ni mbaya at the end anakuwa YEYE NA FAMILIA YAKE!!

we need to discuss this in different orientations!

I submit

Malecela alishakuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais.kwa sasa ni mbunge wa Mtera tayari katangaza atagombea tena 2010 mbona hakuna kelele!!!!!.Mzee wa kiraracha katangaza atagombea mnaaza fitina zenu wakati mnajua waamuzi ni wapiga kura wa Vunjo.


embu nisaidien analipwa ngapi kama pension kwa mwezi??

General Mboma analipwa pension kiasi kwa mwezi mbona alichukua fomu za kugombea ubunge.Mrema kama analipwa pension ndogo au kubwa bado si kigezo cha kumyima haki yake ya kugombea ubunge.

Kwa taarifa yenu wapiga kura wa jimbo la Vunjo bado wanamkubali sana Mrema kutokana na rekodi ya maendeleo aliyowaletea akiwa mbunge wao miaka kumi iliyopita.

Mnaposema kafulia ati hakufanya ufisadi hapo nawashangaa manake mnajichanganya, hamueleweki mko upande gani.

Watanzania wakati mwingine unaweza kupata ugonjwa wa moyo kugundua wanataka nini ?.


Mrema ameonyesha mfano wa mwanasiasa wa ukweli, anasimamia kile anachokiamini. Akiwa ccm alipanda sana hadi kufikia naibu waziri mkuu, lakini alipoona hawezi kubadilisha usanii wa chama hicho aliondoka na akakubali kuachia maslahi aliyokua anapata. Aliukataa ufisadi kwa matendo tofauti na wapiganaji waliopo sasa.

Afya ya Mrema haionekani kunawiri lakini sio sababu ya kusema ati ataenda kufia bungeni. Kwani ni wabunge wangapi wameanguka mjengoni na hata kufa, hiyo sio sababu. Anaona anaweza na amejitolea kwenda kuwatetea wananchi wake hata ikibidi kufia huko. huo ndio uzalendo, mwacheni.

Karibu mjengoni mzee wa Kiraracha na anaeweza kupambana na wewe aje Vunjo tumuaibishe.

Tuko pamoja muze tunamhitaji sana Mzee wa Kiraracha pale mjengoni.
 
Wana saikolojia wansema sisi wote kama binadamu tuna kichaa. Kila mtu ana kichaa chake fulani tangu anakua mtu mpaka unakufa. Mrema ana ukichaa wa kupenda madaraka. Ndio kichaa chake!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom