Mkaa Mweupe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 654
- 183
Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, majira ya saa 11 jioni ambapo mitaa ya Mbezi Beach ilikuwa imetulia na watu wakiendelea na starehe zao. Mara ghafla likazuka kundi la watu wakimfuata jamaa aliyekuwa mtupu huku wakipiga kelele.
Mimi nilidhani kuwa huyu jamaa alikuwa amechanganyikiwa. Mawazo ya awali yalikuwa huenda huyu mtu kavuta bhangi na imemzingua, kwa sababu ni mtu anayefahamika sana hapa mtaani.
Alipofika kwenye maeneo ya bar mmoja hapa mtaani, aliingia hapo na kuzua tafrani kwa wateja kwani nao walidhani jamaa amekuwa chizi. Jamaa akakaa na kuagiza bia huku angali mtupu. Akasikika akijigamba,"Alidhani mi nitashindwa na hiyo elfu thelathini nimeshakula? Kwani ni mwanamke gani ambaye hajawahi kuiona au haijui?..." Alisikika akijigamba. Kama mtu ambaye yu na nguo akakaa kwenye kiti mguu mmoja juu bila ya wasi.
Baada ya kama dakika kadhaa, akatokea kijana mwingine aliyemletea nguo zake. Huyu jamaa akachukua nguo na kuelekea msalani ambapo baada ya kuvaa alitoka huku lile kundi likiendelea kumshangilia kwa ushujaa wake.
Maswali ya kujiuliza:
1. Hivi watanzania ndo tumefikia huku?
2. Hii hali ya uchumi imetufanya watu tushindwe kufikiri.
3. Hali hii ni kuwa amejidhalilisha yeye tu au jamii nzima?
Waungwana tusaidiane mawazo.
Mimi nilidhani kuwa huyu jamaa alikuwa amechanganyikiwa. Mawazo ya awali yalikuwa huenda huyu mtu kavuta bhangi na imemzingua, kwa sababu ni mtu anayefahamika sana hapa mtaani.
Alipofika kwenye maeneo ya bar mmoja hapa mtaani, aliingia hapo na kuzua tafrani kwa wateja kwani nao walidhani jamaa amekuwa chizi. Jamaa akakaa na kuagiza bia huku angali mtupu. Akasikika akijigamba,"Alidhani mi nitashindwa na hiyo elfu thelathini nimeshakula? Kwani ni mwanamke gani ambaye hajawahi kuiona au haijui?..." Alisikika akijigamba. Kama mtu ambaye yu na nguo akakaa kwenye kiti mguu mmoja juu bila ya wasi.
Baada ya kama dakika kadhaa, akatokea kijana mwingine aliyemletea nguo zake. Huyu jamaa akachukua nguo na kuelekea msalani ambapo baada ya kuvaa alitoka huku lile kundi likiendelea kumshangilia kwa ushujaa wake.
Maswali ya kujiuliza:
1. Hivi watanzania ndo tumefikia huku?
2. Hii hali ya uchumi imetufanya watu tushindwe kufikiri.
3. Hali hii ni kuwa amejidhalilisha yeye tu au jamii nzima?
Waungwana tusaidiane mawazo.