Mbavu za Mbwa
JF-Expert Member
- Jan 2, 2011
- 303
- 154
Mara nyingi ili mafanikio yawepo lazima kuwe na combination(pacha). Mfano, enzi za urais wa Nyerere, sera na mawazo ya mawaziri wake wote wakuu yalikuwa kwa kiwango kikubwa yanafanana. Nyerere, Kawawa, Sokoine wote walikuwa wajamaa. Mwinyi na Malecela wote walikuwa Liberals. Mkapa na Sumaye, wote walikuwa mabepari. Nadhani hata combination ya JK na EL ilikuwa inafanana. Swali langu ni hili, je Combination ya JK na Pinda ikoje. Wana sera moja(sizungumzii sera ya chama chao).