Jamani eh, Kikwete anaweza kuwa na matatizo yake kama binadamu wengine yeye siyo Malaika/Nabii. Hili la kusema eti kiwanda cha Mbagala cha CEMENT ni cha kwake ni uzushi mtupu - tusilete mambo ya kuweka chumvi wakati mwingine kwa kutafuta public sympathy na publicity STUNT kwa kuwa tunajuwa akitajwa Kikwete tu, basi watu watakuja juu kwa kumlahumu, tusisite kumsema pale anapokosea mambo fulani lakini siyo vizuri kumzulia MAMBO.
Kwa nini nasema hivyo:
Sidhani kama utetezi wako unajitosheleza; Tanga Cement ambayo ni Simba Cement sasa wanapanua kimsingi ni kujenga kingine kando ya kile kilichopo sasa ambacho kipo nje kidogo ya Jiji la Tanga.
My Take; Kivuli cha Tanga Cement kimetumika hapo ili kuficha ukweli halisi wa jambo hili.... Tutege sikio!
Munashangaa hilo, mbona kajenga hoteli (Bilila) kwenye pitio la Wanyama Serengeti na pia amechukua jengo la TANAPA na ameliuza na TANAPA wamepewa miezi 6 kuhama
wanaohusika ni waarabu; hawa jamaa wanaouza mafuta either ni TIOT au OILCOM, na wanashirikiana na wachina. kuna kazi tulishawafanyia huko nyuma around 2007. labda useme JK ana hisa fulani i don't know.
lakini JK anaingia vipi hapo? kama kuna shida zisemwe na zilekebishwe. wananchi wasipoamka hii nchi haitapata maendeleo hata malaika waje watawale. habari za wachangiaji wengine za kusema CDM ikitawala mambo yatabadilika wakati wananchi wamelala hivi ni ndoto za mchana.
lazima wananchi wawe wakali na wawawajibishe viongozi katika kila hatua ndiyo tutaona maendeleo
Jamani eh, Kikwete anaweza kuwa na matatizo yake kama binadamu wengine yeye siyo Malaika/Nabii. Hili la kusema eti kiwanda cha Mbagala cha CEMENT ni cha kwake ni uzushi mtupu - tusilete mambo ya kuweka chumvi wakati mwingine kwa kutafuta public sympathy na publicity STUNT kwa kuwa tunajuwa akitajwa Kikwete tu, basi watu watakuja juu kwa kumlahumu, tusisite kumsema pale anapokosea mambo fulani lakini siyo vizuri kumzulia MAMBO.
Kwa nini nasema hivyo:
- Kiwanda hiki ni mali ya TANGA CEMENT nadhani wakishirikiana na WACHINA au mitambo ya kuzalisha CEMENT imeagizwa kutoka UCHINA, sasa hapo Kikwete anusikana vipi!
- Kuhusu vumbi linalo tokana na uzalishaji wa CEMENT, mimi ningeshauri wakazi wa Mbagala wawashinikize wajenzi wa kiwanda hicho kwamba vumbi hilo liidhibitiwe kwa njia ya ku-spray maji kwenye vumbi hilo kwa pressure kubwa badala ya kuliachia lipitie kwenye Chimney, wakitekeleza hilo basi wakazi wa huko watakuwa SALAMA, na actually athali za vumbi hilo halitakuwa confined Mbagala tu linaweza kusaambaa popote upepo unapo elekea kama hawataweza kulidhibiti kwa njia niliyo eleza hapo juu.
- Wakati wa kuwabana ni sasa hivi kabla hawaja anza kuzalisha CEMENT, mkichelewa tu basi watawaletea visingizio chungu mzima, kumbuka WAZO Hill bado kiwanda chao kinatoa vumbi hewani bila ya udhibitu wowote na sijawahi kusikia wanachukuliwa hatua yoyote na wahusika wa mazingira - chunga sana.
Kwani huyo aliyeleta hii habari anaushaidi? au porojo tu hata kama tunapinga tupinge kwa hoja na ushahidi na si kupandikiza chuki