Jaji Mstaafu Kaganda: Baadhi ya Mawaziri hawajajaza Fomu za Maadili mpaka sasa

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,495
2,043
Licha ya mikwara ya kutumbua majipu bado wapo mawaziri hawajajaza fomu ya maadili inayowataka kujaza fomu za mali zao.

Ikiwa kweli Rais JPM amedhamiria kukomesha uzembe na kufanya kazi kwa mazoea nashauri aanze na hao.

Wakati akitoa mada katika semina elekezi ya mawaziri na manaibu mawaziri leo, Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Salome S. Kaganda kwa masikitiko alimweleza Waziri Mkuu kwamba kuna baadhi ya Mawaziri na Manaibu Waziri, ambao hawajajaza fomu za maadili mpaka leo, wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu, Rais Mstaafu Kikwete na Mhe. Rais John Pombe Joseph Magufuli, ameshajaza fomu hizo. Jaji Salome Kaganda, alikabidhi majina ya Mawaziri husika. Sijui wana utetezi gani.

MAONI: Mheshimiwa Rais ni maajabu hawa mawaziri wanashinda kutumbua majipu, wakati kumbe wao pia ni majibu. Ili kuleta somo, mawaziri na manaibu waziri husika wanyang'anywe wadhifa wao.
 
Wapo buzy kutumbua majipu. Huyo mama ni mmbea tu. Aliwapelekea ofisini kwao wakashindwa kusaini? Aliamua kupeleka kwa Rais akasaini, akapeleka kwa PM akasaini. Akataka mawaziri wamfuate ofisini kwake wakati wako buzy kutumbua majipu. Aache umbea huyu mama
 
Wakati akitoa mada katika semina elekezi ya mawaziri na manaibu mawaziri leo, Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Salome S. Kaganda kwa masikitiko alimweleza Waziri Mkuu kwamba kuna baadhi ya Mawaziri na Manaibu Waziri, ambao hawajajaza fomu za maadili mpaka leo, wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu, Rais Mstaafu Kikwete na Mhe. Rais John Pombe Joseph Magufuli, ameshajaza fomu hizo. Jaji Salome Kaganda, alikabidhi majina ya Mawaziri husika. Sijui wana utetezi gani.

MAONI: Mheshimiwa Rais ni maajabu hawa mawaziri wanashinda kutumbua majipu, wakati kumbe wao pia ni majibu. Ili kuleta somo, mawaziri na manaibu waziri husika wanyang'anywe wadhifa wao.
 
Wapo buzy kutumbua majipu. Huyo mama ni mmbea tu. Aliwapelekea ofisini kwao wakashindwa kusaini? Aliamua kupeleka kwa Rais akasaini, akapeleka kwa PM akasaini. Akataka mawaziri wamfuate ofisini kwake wakati wako buzy kutumbua majipu. Aache umbea huyu mama
Hata ukitaka uwe dereva mzuri, sharti uwe na leseni kisheria.
Huwezi kutamba kuwa ni bingwa wa udereva kabla ya kutimiza msharti ya sheria.

Mtoa posti inaelekea hujui kuwa kujaza fomu za maadili ni matakwa ya sheria.
Waziri asiyetimiza masharti ya uongozi na sheria hafai hata kidogo.
 
Wale Majipu Matatu mh. Freeman Mbowe aliyoyataja ameshayashugulikia kwanza au ndio mwendelezo wa Mazingaombwe?
 
Yani hata sielewi hii nchi inaelekea wapi. Walopaswa kupewa semina ndio wanatoa semina. Hivi Angela Kairuki yeye anakuwa miongoni mwa wanaotoa ufafanuzi na maelezo kwa mawaziri wakati utendaji wake tu ni wa mashaka na yeye alipaswa apate semina juu ya namna ya kutumbua majipu.
 
Hawa mawazir ndio walikuwa wanajisifu wanaendana na kasi ya makufuli sasa kama sio mafisadi kwa nini wasijaze fomu ya maadili ambayo ndio kipimo cha maadili hapo ndipo utajua ccm ni Ile Ile majipu ccm ni maji uwezi kuyakimbia ccm ni Ile Ile
 
Kabla ya kufika huko ningependa kujua au kufahamu Waziri aliyetuma ujumbe kuwa flow meter ya mafuta bandarini ifunguliwe kachukuliwa hatua gani???


Wakuu acheni kuchakachua post za wa tu. ..mnaweza kuanzisha nyuzi kuhusiana na hayo maoni yenu.

Hoja ni kuhusu mawaziri ambao hawajajaza fomu ya maadili wakati sheria inawataka wajaze.


Wale Majipu Matatu mh. Freeman Mbowe aliyoyataja ameshayashugulikia kwanza au ndio mwendelezo wa Mazingaombwe?
 
Kwa hili ,kwa hili ,kwa hili . Kwa hili patachimbika kama hawa mawaziri magamba wataendelea kukalia viti vyao na kumhujumu Rais wetu na Waziri mkuu wetu.
Watoke tu mana hawafai kabisa.
Tena inabidi mali zao zichunguzwe. Hawa wako pale kulinda maslahi yao binafsi .
Huu ni ujeuri na kiburi wa hao mawaziri kwa mh. Rais.
Kama wanachelewa hata kutekeleza majukumu yasiyohitaji hata nguvu watawezaje kuwatendea wananchi haki kwa wakati ili kutekeleza kauli mbiu ya hapa kazi tu?

Wameshindwa kazi ndogo ya kwenda kujaza fomu zao binafsi wataweza kusema kwa vitendo hapa kazi tu.

Yani mpaka leo ni Zaidi ya siku 115 za uongozi wa mh.JPM bado ndani ya serikali yake kuna watu wanasuasua kujaza kiapo cha kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu?
Je,hao mawaziri hawajawa tayari kuwatumikia wananchi kwa uadilifu au bado wanatafakari kuteuliwa kwao?

Hili ndio tatizo la kuweka kiraka cha Kitambaa kipya kwenye nguo chakavu na kuukuu.
 
Wakati akitoa mada katika semina elekezi ya mawaziri na manaibu mawaziri leo, Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Salome S. Kaganda kwa masikitiko alimweleza Waziri Mkuu kwamba kuna baadhi ya Mawaziri na Manaibu Waziri, ambao hawajajaza fomu za maadili mpaka leo, wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu, Rais Mstaafu Kikwete na Mhe. Rais John Pombe Joseph Magufuli, ameshajaza fomu hizo. Jaji Salome Kaganda, alikabidhi majina ya Mawaziri husika. Sijui wana utetezi gani.

MAONI: Mheshimiwa Rais n maajabu hawa mawaziri wanashinda kutumbua majipu, wakati kumbe wao pia ni majibu. Ili kuleta somo, mawaziri na manaibu waziri husika wanyang'anywe wadhifa wao.
Zimeleta manufaa gani hizo Fomu tangu zianze kutumika Huoni kama nikupoteza muda na Rasilimali
 
Pamoja na msisitizo wenye ukali na dhamira alioutoa Rais Magufu kwa mawaziri siku alipowaapisha.Bado baadhi ya mawaziri na manaibu hawajajaza fomu za maadili ya utumishi wa umma.

Mwenyeki wa tume hiyo ameahidi kumpatia Waziri mkuu Majaliwa majina ya mawaziri na manabu ambao hawajafanya zoezi hilo kwa hatua zaidi.Pamoja na kuwa Rais na waziri mkuu walishatekeleza sheria hiyo.

Kwa jinsi Rais aliwasisitiza Mawaziri wake juu ya suala hili,Ambao hawajatekeleza mpaka sasa wameonyesha kibri cha kiwango cha lami.
 
Na watuambie tunawalipa mishahara kiasi gani.

Maadili ni pamoja na uwazi.

Wanaendesha serikali kwa kutumia kodi zetu ikiwemo kulipwa mishahara na hizo hizo kodi zetu halafu hatujui tunawalipa shilingi ngapi wakati sisi ndo tumewaajiri wao kututumikia.

Huyo Magufuli na aanze kuutangaza mshahara tunaomlipa la sivyo naye atakuwa hana tofauti na waliomtangulia.
 
Waache waendelee na kazi zao hizo form nafikiri hazitusaidii chochote sisi zaidi zitatutia hasira tu!
 
Na watuambie tunawalipa mishahara kiasi gani.

Maadili ni pamoja na uwazi.

Wanaendesha serikali kwa kutumia kodi zetu ikiwemo kulipwa mishahara na hizo hizo kodi zetu halafu hatujui tunawalipa shilingi ngapi wakati sisi ndo tumewaajiri wao kututumikia.

Huyo Magufuli na aanze kuutangaza mshahara tunaomlipa la sivyo naye atakuwa hana tofauti na waliomtangulia.
Rais ni mtatnzania na Katiba ya Tanzania inamlinda ataje mshahara ili iweje? Hebu weka wewe wazi kipato chako hapa Kamii Forum kama unakumbatia suala la UWAZI. Hebu muacheni apumue kidogo!
 
Rais ni mtatnzania na Katiba ya Tanzania inamlinda ataje mshahara ili iweje? Hebu weka wewe wazi kipato chako hapa Kamii Forum kama unakumbatia suala la UWAZI. Hebu muacheni apumue kidogo!

Mimi situnzwi na pesa za walipa kodi. Nafanya kazi kwenye sekta binafsi na bosi wangu anaujua mshahara wangu.

Rais anatunzwa na pesa za walipa kodi. Ni mtumishi wa walipa kodi.

Kwa msingi huo, sisi walipa kodi ndiyo mabosi wake.

Umewahi kuona wapi ambapo bosi haujui mshahara wa mtumishi wake?

Mbona mnakuwa wapumbavu namna hiyo nyie watu? Mnashindwa kuvielewa hata vitu vyepesi namna hii?
 
Back
Top Bottom