Jaji Lewis Makame. Mwenyekiti wa NEC amekanusha tuhuma cha Profesa Baregu kwamba NEC imeongoza idadi ya wapiga kura na kufikia milioni 19 ili kuisaidia CCM kupata ushindi! Si kwamba anakanusha idadi ya wapiga kura haijafikia milioni 19 bali alichokanusha ni madai kwamba idadi hiyo imeongezwa isivyo halali-kwamba hawafikii milioni 19! Kimsingi, madai ya Profesa Baregu yana mantiki kwakwa haingii akilini kwamba nchi inayokadiriwa kuwa na wananchi milioni 40 karibu nusu yake wamejiandikisha!
Pamoja na yote hayo, naamini leo hii ukiuliza ni Watanzania wangapi wanamiliki simu za mkononi kwa kuangalia namba zilizosajiliwa basi bila shaka unaweza kukuta wamefikia hata milioni 50 wakati Watanzania wanakadiriwa kufikia milioni 40!!
Mimi binafsi, siamini kama Watanzania waliojindikisha wanafikia milioni 19. Endapo sensa itafanyika(mtu kwa mtu) basi am sure idadi hiyo haifiki! Sasa inawezekana kwamba ni kweli NEC imeongoza idadi ya wapiga kura? Binafsi, sizani endapo wameongezwa ingawaje Jaji Makame ameshindwa kutumia takwimu za kisayansi wakati Profesa Baregu ametumia takwimu za kisayansi kwa kuangalia upande mmoja; nao ni Population Growth Rate! Wakati ametumia Population Growth Rate (PGR), Profesa Baregu ama kwa makusudi ya kisiasa au kwa kupitiwa/kutofahamu ameshindwa kutumia na population Death Rate (PDR) na kisha kufanya mahesabu yake! Ukitumia PGR peke yake, ni kweli idadi ya wapiga kura hawezi kufikia milioni 19 na kama wanafikia basi kuna namna! Lakini si wote ambao walijiandikisha tokea zoezi hili lianze (i think 2004) bado wapo hai duniani na sizani endapo wote waliofariki taarifa zao zimeondolewa kwenye daftari la wapiga kura! Hivyo basi, sina shaka kwamba idadi hiyo ya milioni 19 ndani yake wapo marehemu ambao majina yao bado yamo kwenye daftari la wapiga kura! Pamoja na mapungufu hayo, ni jambo la kawaida kuona Mtu mmoja ana kitambulisho zaid ya kimoja cha kupigia kura ikiwa na maana kwamba amejiandikisha zaidi ya mara moja! Wapo waliojondikisha zaidi ya mara 2! Unakuta mtu hakioni kitambulisho chake hivyo zoezi linapoanza upya na yeye anaenda kujiandikisha a hasemi kwamba alishajiandikisha hapo awali! Ingawje NEC ilishatoa majina ya watu waliojindikisha zaidi ya mara moja, lakini nina uhakika wapo wengi tu ambao wamejiandikisha zaidi ya mara moja na majina yao hayakutolewa kwamba wamejiandikisha zaidi ya mara moja!
Pamoja na yote hayo, bado kuna ukweli mwingine kwamba raia safari hii walihamasika sana kujiandikisha kupiga kura! Si kwamba walihamasika ili watumie haki yao ya kuchagua, bali wengi wao walihamasika ili tu wapate ID!!
Hivyo basi, kwa kuangalia ukweli huu utakuta kwamba hoja ya kwamba NEC imepika idadi ya wapiga kura isiwe na ukweli wowote hivyo hatutarajii wanapinzani, hususani CHADEMA kuifanya hii nayo kuwa ni hoja ya msingi ya kuyatilia mashaka matokeo ya uchaguzi mkuu!